Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,438
- 3,333
Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mara leo imewahukumu Watuhumiwa wanne wa ujambazi wa kutumia silaha kutumikia kifungo hicho jela
Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Staneley Mwakihaba baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na walalamikaji 12
Mwendesha mashitaka wa Jamhuri, Yese Temba aliiambia Mahakama kuwa Watuhumiwa hao wakiwa na bunduki aina za SMG, Panga na Shoka waliwavamia walalamikaji
Waliwatishia kuwaua na kuwapiga kwa kutumia silaha kisha kuwapora fedha na simu huku risasi moja ikimpiga Janipher Howard na kusababishia ulemavu baada ya kukatwa mguu
Katika tukio hilo lilotokea Desemba 02, 2016 katika kijiji cha Magunga wilayani Butiama mkoani Mara, Daniel Yuda alijeruhiwa kwa risasi katika mguu wake wa kulia
Chanzo: ITV
Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Staneley Mwakihaba baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na walalamikaji 12
Mwendesha mashitaka wa Jamhuri, Yese Temba aliiambia Mahakama kuwa Watuhumiwa hao wakiwa na bunduki aina za SMG, Panga na Shoka waliwavamia walalamikaji
Waliwatishia kuwaua na kuwapiga kwa kutumia silaha kisha kuwapora fedha na simu huku risasi moja ikimpiga Janipher Howard na kusababishia ulemavu baada ya kukatwa mguu
Katika tukio hilo lilotokea Desemba 02, 2016 katika kijiji cha Magunga wilayani Butiama mkoani Mara, Daniel Yuda alijeruhiwa kwa risasi katika mguu wake wa kulia
Chanzo: ITV