Watu wengi waliopo kwenye ndoa hawana furaha!

Muzine

JF-Expert Member
May 4, 2017
32,366
60,399
Tupeni mrejesho kama mna furaha kweli!

Leo ukiangalia ndoa nyingi zimepooza na kufunikwa na wingu zito la mizozo kila kukicha

Ukiwauliza wanandoa wengi husema Mwanzoni mwa ndoa yetu tulipendana kwa dhati,lakini shauku na penzi letu siku hizi imepotea.

Hakuna urafiki mzuri kati yetu kama hapo awali wala hatufurahii kuwa pamoja,hata kucheka inakuwa tatizo pamoja na kulala kitanda kimoja na ushirika wao katika mambo mengi.

Ndoa zingine wana ndoa hawawezi hata kujadili matatizo yao kwa pamoja, mbaya zaidi kufanya mapenzi kwao imekuwa kama wajibu badala ya starehe.

Hii ni hatari maana hakuna mtu kati yao anayejisikia shauku ya mapenzi kwa mwenzi wake.

Ukichunguza sio kwamba kuna mtu anatoka nje ya ndoa hapana utawasikia wanasema ndoa yetu haina upendo.

Matatizo ya ndoa yapo mengi na yanatofautiana ndoa na ndoa,lakini vilio vingi vya ndoa vinafanana.

Nyongeza : Ambao hatujaolewa tunatamani kweli Kuingia kwenye ndoa .


Location: Napita kwa huzuni.
 
Tupeni mrejesho kama mna furaha kweli!

Leo ukiangalia ndoa nyingi zimepooza na kufunikwa na wingu zito la mizozo kila kukicha
Ukiwauliza wanandoa wengi husema Mwanzoni mwa ndoa yetu tulipendana kwa dhati,lakini shauku na penzi letu siku hizi imepotea.
Hakuna urafiki mzuri kati yetu kama hapo awali wala hatufurahii kuwa pamoja,hata kucheka inakuwa tatizo pamoja na kulala kitanda kimoja na ushirika wao katika mambo mengi.
Ndoa zingine wana ndoa hawawezi hata kujadili matatizo yao kwa pamoja, mbaya zaidi kufanya mapenzi kwao imekuwa kama wajibu badala ya starehe.

Hii ni hatari maana hakuna mtu kati yao anayejisikia shauku ya mapenzi kwa mwenzi wake.
Ukichunguza sio kwamba kuna mtu anatoka nje ya ndoa hapana utawasikia wanasema ndoa yetu haina upendo.

Matatizo ya ndoa yapo mengi na yanatofautiana ndoa na ndoa,lakini vilio vingi vya ndoa vinafanana.

Nyongeza : Ambao hatujaolewa tunatamani kweli Kuingia kwenye ndoa .


Location: Napita kwa huzuni.

Acha kujitisha mwenyewe mkuu.wewe nenda kaolewe tu.offcourse kuolewa haijawahi kuwa kitu chepesi.ukiiona ndoq ni kitu chepesi basi ndoa yako haitakuwa yenye upendo kama ulivyosema
 

Similar Discussions

15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom