figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Watu watatu waliokutwa na ndege watatu aina ya Tausi waliokuwa Ikulu wamehukumiwa kulipa fidia ya Sh. Mil 6 baada ya kupatikana hatia katika kesi ya Uhujumu Uchumi kwa kujihusisha na nyara za serikali bila kuwa na kibali.
Pia, washtakiwa hao wameachiwa huru kwa masharti ya kutofanya makosa kwa kipindi cha miezi sita na ndege watatu aina ya Tausi wataifishwe na wapelekwe serikalini.
Washtakiwa hao ni David Graha, Mohamed Hatibu na Mohamed Ally ambao wamehukumiwa ikiwa ni siku tano tangu wafikishwe mahakamani hapo.
Hukumu hiyo imesomwa na Hakimu Mkazi, Salum Ally ambapo amesema mahakama hiyo imezingatia masharti ya makubaliano ya washtakiwa hao wamekubali kuilipa Serikali fidia ya zaidi ya Sh.Mil 6.8.
Pia, washtakiwa hao wameachiwa huru kwa masharti ya kutofanya makosa kwa kipindi cha miezi sita na ndege watatu aina ya Tausi wataifishwe na wapelekwe serikalini.
Washtakiwa hao ni David Graha, Mohamed Hatibu na Mohamed Ally ambao wamehukumiwa ikiwa ni siku tano tangu wafikishwe mahakamani hapo.
Hukumu hiyo imesomwa na Hakimu Mkazi, Salum Ally ambapo amesema mahakama hiyo imezingatia masharti ya makubaliano ya washtakiwa hao wamekubali kuilipa Serikali fidia ya zaidi ya Sh.Mil 6.8.
Watatu kizimbani kwa kuiba tausi wa Ikulu
Serikali imewafikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu watu watatu kwa kosa la kukutwa na tausi watatu wanaodaiwa kuwa wa Ikulu. Washtakiwa hao David Graha, Mohamed Hatibu na Mohamed Ally, wamefikishwa mahakamani hapo leo Ijumaa Oktoba 25, mbele ya Hakimu Mkazi Vicki Mwaikambo. Wakili wa...
www.jamiiforums.com