Watu wasiojulikana wamenunua umeme kwenye LUKU yangu

Ulongupanjala

JF-Expert Member
Apr 9, 2013
7,587
12,113
Habari za Mei Mosi,

Nilikuwa napata umeme units 75,kwa chini ya 9200 kwa mwezi.

Mwezi wa nne mwanzoni nilinunua umeme na kupata units 36, baada ya siku 3, watu/mtu asiyejulikana akanununua umeme na kupata units 41,bila mimi kujua chochote.

Jana nikaenda TANESCO kununua umeme wa 4,000 cha ajabu nikapata units 9 tu, nikashtuka sana.

Nikaenda kuuliza ndio nikaambiwa kuwa ndani ya mwezi Aprili nimenunua umeme zaidi ya units 75 za kwenye tariff yangu, hivyo nimepelekwa tariff 4, ambayo nanunua umeme kwa unit 1 kwa Tsh 350.

Naomba kujua nini nifanye ili nirudishwe kwenye tariff yangu ya awali? Maana nyumba ni ya familia tu na hatuna matumizi ya umeme makubwa.

Cc:TANESCO

Asanteni wote.
 
Mtu alinunua umeme kwa kutumia meter number yako ili iweje maana hawezi kutumia popote zaidi ya kwako.

Anyway, ili kurudi kwenye tariff ndogo basi ni kuendelea 'kumaintain' matumizi madogo ndani ya miezi mitatu kama sikosei halafu utaenda tanesco wakurudishe.
 
Ndio hivyo mkuu,vyuma vimebana halafu naambiwa ninunue umeme kwa 350 kwa 1units.
 
Mtu alinunua umeme kwa kutumia meter number yako ili iweje maana hawezi kutumia popote zaidi ya kwako.

Anyway, ili kurudi kwenye tariff ndogo basi ni kuendelea 'kumaintain' matumizi madogo ndani ya miezi mitatu kama sikosei halafu utaenda tanesco wakurudishe.
Sina hakika aliyenunua umeme kwa namba yangu ya LUKU alikuwa na malengo gani au ni bahati mbaya,sina nijualo!!???)))
 
Pole Mkuu, Inamaana Mwezi Mmoja Tu Ukizidisha Matumizi Tanesco Wanaona Ushakuwa Mtumiaji Mkubwa?
Hata mimi nimeshangaa maana ninavyojua ukizidisha kwa mwezi wa kwanza unapigwa faini, ukizidisha mwezi wa pili faini mwezi wa tatu ndipo wanakurudisha kwenye tarrif kubwa.
Halafu mimi nilikuwa nadhani hata ununue unit nyingi hata 200 ndani ya mwezi uweke kwenye luku hawamaindi ili mradi matumizi yasizidi 75 units kwa mwez kumbe inabidi hata kununua usizidi hapo maana nimebadirishiwa tarrif mwez uliopita
 
Mkuu ukitaka kurudi tarrif inabidi uwe unanunua umeme wa 9200 kama mwanzo, hakikisha unanunua umeme wa 9200 ndani ya miezi 3 then units utakazopata zitumike ndani ya mwezi mmoja, ikitokea units zimeisha kabla ya mwezi usinunue tena
 
Silii,nauliza namna mambo yalivyofanyika kwangu ndio kawaida na nn cha kufanya!!
 
Sio umepelekwa tarrif 4,meter yako ilikuwa tarrif 4 baada ya kuzidisha unit ndani ya huo mwezi meter ikajichange tarrif imeenda tarrif 1
 
Kuepuka balaa kama hilo. Watu hugawanya nyumba na kuweka mita za luku mbili tatu. Hasa nyumba za kupanga na zile zenye fremu. Kama nyumba ni kubwa, kaombe mita ya pili.
 
umeme wa tariff 4 umekaa kisiasa, japo inadaiwa ni kusaidiwa wa kipato cha chini. umeme wa tanzania ni aghari, na chombo kithibiti kinapata zaidi unapopanda, hivo ni mzigo kwa mtumiaji.
 
Hata mimi nimeshangaa maana ninavyojua ukizidisha kwa mwezi wa kwanza unapigwa faini, ukizidisha mwezi wa pili faini mwezi wa tatu ndipo wanakurudisha kwenye tarrif kubwa.
Halafu mimi nilikuwa nadhani hata ununue unit nyingi hata 200 ndani ya mwezi uweke kwenye luku hawamaindi ili mradi matumizi yasizidi 75 units kwa mwez kumbe inabidi hata kununua usizidi hapo maana nimebadirishiwa tarrif mwez uliopita[/QUOTEhapana Kila Mwezi Unanunua Umeme Wa Tarif Yako,haijalishi Iwe Umemaliza Unit Au La Ila Tu Ndani Ya Mwezi Huo Usipitilize Unit Ulizopangiwa I.E 75 maelezo Haya Ndo Nayoyafahamu Maana Nlishakuwa Wa Tarrif 4 Kwa Mabweni Ya Wanafunzi Wa Shule Ya Msingi,nlikuwa Nawanunulia Wa 6500 Kila Mwezi Haijalishi Unaisha Au La Kuna Kipindi Unajikuta Unit Zimejiaccumulate Mpaka Mia 300 Huko Lakini Kila Mwezi Lazima Ununue
 
Mi nanunua umeme wa elf9 kila mwezi, matumizi yangu ni napikia jiko la umeme la enegy sever, pasi kila siku, na nina taa tubelight kama 6 zinakesha za nje, nyumba ni family size.sema fridge nawasha mchana tu na usiku inazimwa
 
Habari za Mei Mosi,

Nilikuwa napata umeme units 75,kwa chini ya 9200 kwa mwezi.

Mwezi wa nne mwanzoni nilinunua umeme na kupata units 36, baada ya siku 3, watu/mtu asiyejulikana akanununua umeme na kupata units 41,bila mimi kujua chochote.

Jana nikaenda TANESCO kununua umeme wa 4,000 cha ajabu nikapata units 9 tu, nikashtuka sana.

Nikaenda kuuliza ndio nikaambiwa kuwa ndani ya mwezi Aprili nimenunua umeme zaidi ya units 75 za kwenye tariff yangu, hivyo nimepelekwa tariff 4, ambayo nanunua umeme kwa unit 1 kwa Tsh 350.

Naomba kujua nini nifanye ili nirudishwe kwenye tariff yangu ya awali? Maana nyumba ni ya familia tu na hatuna matumizi ya umeme makubwa.

Cc:TANESCO

Asanteni wote.
Kaka utaki kupanda cheo?Maana hapo kitaamu inaonyesha uchumi wa familia umekua ndio maana hata matumizi yameongezeka.Swala la kusema umenunuliwa umeme na watu wasiojulikana sio kweli
 
Mi nanunua umeme wa elf9 kila mwezi, matumizi yangu ni napikia jiko la umeme la enegy sever, pasi kila siku, na nina taa tubelight kama 6 zinakesha za nje, nyumba ni family size.sema fridge nawasha mchana tu na usiku inazimwa
jini Kisirani Hilo Jiko La Umeme La Energy Saver Ulinunua Wapi Na Sh Ngapi?Ni Yale Makubwa?Yana Oven Pia Na Pasi Ningependa Kujua,hapo Pa Friji Ndo Sitoweza Maana Ninauza Majimaji Mabarafu Kwa Hiyo Lazima Npigike
 
Habari za Mei Mosi,

Nilikuwa napata umeme units 75,kwa chini ya 9200 kwa mwezi.

Mwezi wa nne mwanzoni nilinunua umeme na kupata units 36, baada ya siku 3, watu/mtu asiyejulikana akanununua umeme na kupata units 41,bila mimi kujua chochote.

Jana nikaenda TANESCO kununua umeme wa 4,000 cha ajabu nikapata units 9 tu, nikashtuka sana.

Nikaenda kuuliza ndio nikaambiwa kuwa ndani ya mwezi Aprili nimenunua umeme zaidi ya units 75 za kwenye tariff yangu, hivyo nimepelekwa tariff 4, ambayo nanunua umeme kwa unit 1 kwa Tsh 350.

Naomba kujua nini nifanye ili nirudishwe kwenye tariff yangu ya awali? Maana nyumba ni ya familia tu na hatuna matumizi ya umeme makubwa.

Cc:TANESCO

Asanteni wote.

System imekutoa kwenye huo utaratibu automatically, huna namna!
 
jini Kisirani Hilo Jiko La Umeme La Energy Saver Ulinunua Wapi Na Sh Ngapi?Ni Yale Makubwa?Yana Oven Pia Na Pasi Ningependa Kujua,hapo Pa Friji Ndo Sitoweza Maana Ninauza Majimaji Mabarafu Kwa Hiyo Lazima Npigike
Kuna jamaa wa magari walikuja ofisini kwetu wakauza. Ni mchina la plate moja wanauza 150000. Ila niliyaona bangarole wanauza kama elf 60 za kibongo, na yapo original yake plate2 yanauzwa laki 7 ya kibongo
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom