Watu wanasema mimi ni nani? Swali alilouliza Yesu linalofungua ubongo wa mwanadamu kujitambua

Wivu wq kila kitu unao

Ndio mafundisho ya kanisa hayo ??

Sasa tuambie huyu aliyesema maneno haya uliyoyaleta ni nani ??


Luka 9:18-21 "Yesu aliwauliza wanafunzi wake kua je makutano hao wanasema ya kua mimi ni nani? Wanafunzi wake wakajibu yohana mbatizaji wengine wanasema wewe ni Eliya lakini petro akamjibu kua Ndiwe Kristo wa Mungu"
 
Ndio mafundisho ya kanisa hayo ??

Sasa tuambie huyu aliyesema maneno haya uliyoyaleta ni nani ??


Luka 9:18-21 "Yesu aliwauliza wanafunzi wake kua je makutano hao wanasema ya kua mimi ni nani? Wanafunzi wake wakajibu yohana mbatizaji wengine wanasema wewe ni Eliya lakini petro akamjibu kua Ndiwe Kristo wa Mungu"
Bila uvumbuzi wa Copy n Paste maisha yako yangekua vipi.?
 
Luka 9:18-21 "Yesu aliwauliza wanafunzi wake kua je makutano hao wanasema ya kua mimi ni nani? Wanafunzi wake wakajibu yohana mbatizaji wengine wanasema wewe ni Eliya lakini petro akamjibu kua Ndiwe Kristo wa Mungu".

Kumbe yesu ni kristo wa mungu?

Kristo wa mungu vs mungu

Nani muumba hapa???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapendwa kwa muda huu wa kukaa nyumba ni baada ya kazi, soma ujumbe mzuri toka kwa Bwn Yesu.
Utapata nondo na madini aliyomwaga ili mtambue kuwa yeye ni mwana wa Mungu aliye hai.
Yohn: 7: 1~33
The whole chapter.
Yohn : 8:1-59
The whole chapter.
Tuliza akili muombe Mungu akupe ufunuo wa kweli nayo kweli itakuweka huru!!

Thanks Da Vinci.
Kiranga, Graph and CO. see the truth through Jesus the Lord.
 
Wapendwa kwa muda huu wa kukaa nyumba ni baada ya kazi, soma ujumbe mzuri toka kwa Bwn Yesu.
Utapata nondo na madini aliyomwaga ili mtambue kuwa yeye ni mwana wa Mungu aliye hai.
Yohn: 7: 1~33
The whole chapter.
Yohn : 8:1-59
The whole chapter.
Tuliza akili muombe Mungu akupe ufunuo wa kweli nayo kweli itakuweka huru!!

Thanks Da Vinci.
Kiranga, Graph and CO. see the truth through Jesus the Lord.
Mlango 7
1 Na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua.
2 Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
3 Basi ndugu zake wakamwambia, Ondoka hapa, uende Uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama kazi zako unazozifanya.
4 Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu.
5 Maana hata nduguze hawakumwamini.
6 Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu.
8 Kweeni ninyi kwenda kula sikukuu; mimi sikwei bado kwenda kula sikukuu hii, kwa kuwa haujatimia wakati wangu.
9 Naye alipokwisha kuwaambia hayo, alikaa vivi hivi huko Galilaya.Yesu katika Sikukuu ya Vibanda
10 Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye alipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.
11 Basi Wayahudi wakamtafuta kwenye sikukuu, wakasema, Yuko wapi yule?
12 Kukawa na manung?uniko mengi katika makutano juu yake. Wengine wakasema, Ni mtu mwema. Na wengine wakasema, Sivyo; bali anawadanganya makutano.
13 Walakini hakuna mtu aliyemtaja waziwazi, kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
14 Hata ikawa katikati ya sikukuu Yesu alikwea kuingia hekaluni, akafundisha.
15 Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?
16 Basi Yesu akawajibu, akasema, Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka.
17 Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.
18 Yeye anenaye kwa nafsi yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka, huyo ni wa kweli, wala ndani yake hamna udhalimu.
19 Je! Musa hakuwapa torati? Wala hakuna mmoja wenu aitendaye torati. Mbona mnatafuta kuniua?
20 Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua?
21 Yesu akajibu, akawaambia, Mimi nalitenda kazi moja, nanyi nyote mnaistaajabia.
22 Musa aliwapa tohara; lakini si kwamba yatoka kwa Musa, bali kwa mababa; nanyi siku ya sabato humtahiri mtu.
23 Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato?
24 Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki.Huyu ndiye Kristo?
25 Basi baadhi ya watu wa Yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue?
26 Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu wanajua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo?
27 Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.
28 Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi.
29 Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.
30 Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.
31 Na watu wengi katika mkutano wakamwamini; wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu?Maofisa Watumwa Kumkamata Yesu
32 Mafarisayo wakawasikia mkutano wakinung?unika hivi juu yake; basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma watumishi ili wamkamate.
33 Basi Yesu akasema, Bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; kisha naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja.
 
Wapendwa kwa muda huu wa kukaa nyumba ni baada ya kazi, soma ujumbe mzuri toka kwa Bwn Yesu.
Utapata nondo na madini aliyomwaga ili mtambue kuwa yeye ni mwana wa Mungu aliye hai.
Yohn: 7: 1~33
The whole chapter.
Yohn : 8:1-59
The whole chapter.
Tuliza akili muombe Mungu akupe ufunuo wa kweli nayo kweli itakuweka huru!!

Thanks Da Vinci.
Kiranga, Graph and CO. see the truth through Jesus the Lord.
Mlango 8
1 [Walikwenda kila mtu nyumbani kwake; naye Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni.
2 Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.
4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.
5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?
6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.
8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.
10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?
11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]Yesu Nuru ya Ulimwengu
12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
13 Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.
14 Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako.
15 Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu.
16 Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi na yeye aliyenipeleka.
17 Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
18 Mimi ndimi ninayejishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenipeleka ananishuhudia.
19 Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui; kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu.
20 Maneno hayo aliyasema alipokuwa akifundisha hekaluni, katika chumba cha hazina; wala hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.Yesu Atabiri kuhusu Kifo chake
21 Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja.
22 Basi Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja?
23 Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.
25 Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia.
26 Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake, ndiyo ninenayo katika ulimwengu.
27 Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba.
28 Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo.
29 Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.
30 Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamini.Wanafunzi wa Kweli
31 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
33 Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?
34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.
36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.
37 Najua ya kuwa ninyi ni uzao wa Ibrahimu lakini mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halimo ndani yenu.
38 Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo.Yesu na Abrahamu
39 Wakajibu, wakamwambia, Baba yetu ndiye Ibrahimu! Yesu akawaambia, Kama mngekuwa watoto wa Ibrahimu, mngezitenda kazi zake Ibrahimu.
40 Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo.
41 Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu.
42 Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma.
43 Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu.
44 Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.
45 Nami, kwa sababu nasema iliyo kweli, hamnisadiki.
46 Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.
48 Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?
49 Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima yangu.
50 Wala mimi siutafuti utukufu wangu; yuko mwenye kutafuta na kuhukumu.
51 Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.
52 Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng?amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.
53 Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?
54 Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu.
55 Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika.
56 Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
59 Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.
 
Salute comrades
NB: bandiko hili nimetumia maandiko ya biblia hata kama unaona haikuhusu nakusihi endelea kusoma unaweza pata kitu.

Katika dunia yetu hii tumeona ni sentensi ya maneno kadhaa tu ndio imeubadirisha huu ulimwengu wetu na kuufanya uendelee. Unaweza kuona sentensi kama vile Newton’s laws of motion zilivyochangia maandeleo ya dunia yetu karibia asilimmia 50 ya maendeleo ya ulimwengu yanaweza kuwa yameletwa na hizo sentesi (laws) tatu za mwanasayansi Issac Neawton kiteknolojia, kiuchumi, pia katika mafunzo ya kiroho hizo laws tatu zinafanya kazi. Au unaweza kuona formula ya E= mc2 ya mwanasayansi Albert Einstein ilivyopelekea mauaji ya mamilioni ya watu huko Hiroshima na Nagasaki Japan, aidha mwanasayansi toka ugiriki Archimedes sentsnsi yake kuhusu kuzama na kuelea kwa kitu ilivyoleta maendeleo makubwa kwenye usafiri wa maji nk. Hivyo unaweza kuona kua hua ni sentensi au maneno ya mtu ndio yameleta makubwa hapa duniani baada ya kuchambuliwa na kufanyiwa kazi.

Swali alilouzaYesu wanafunzi wake linavyowasha taa ya kujitambua kichwani mwa binaadamu
.

Luka 9:18-21
"Yesu aliwauliza wanafunzi wake kua je makutano hao wanasema ya kua mimi ni nani? Wanafunzi wake wakajibu yohana mbatizaji wengine wanasema wewe ni Eliya lakini petro akamjibu kua Ndiwe Kristo wa Mungu".

lengo la mada yangu ni kufundisha juu ya mtu kujitambua yeye ni nani (to know your identity), katika swali hilo alilouuliza yesu unaweza kuona ni swali rahisi tu lakini likichambuliwa limebeba ufunguo wa kufungua akili ya mtu kujitambua.
Maneno ya muhimu kwenye swali hiyo ni watu wanasema mimi kua ni nani? Yesu alipouliza swali hilo sio kwamba alikua anataka wamwambie jina lake hasha alitaka afahamu je watu wanamjua yeye ni nani, ndipo petro anamjibu kua ni Kristo wa Mungu. Je nawe ushajiuliza wewe ni nani na watu wanasema wewe ni nani? Twende nikupatie majibu.

Mimi ni nani?
Hapo ulipo anza kujiuliza maswali haya na ujijibu mwenyewe,
Je hivi nilivyo ndivyo natakiwa niwe? Yaani ukijiangalia tabia zako, matendo yako ndivyo unatakiwa uwe? Jibu unalo.

Watu wanasema mimi ni nani?
Ulishwahi kuona mtu Fulani akitaka kumchumbia binti Fulani anaanza kwanza kuulizia kwa watu wanaomfahamu kama vile majirani, mrafiki ni kwasababu watu wa pembeni wanakufahamu zaidi, je leo hii wewe memba mwenzangu wa jf mtu akiuyliza jirani zako kua wewe ni nani atajibu vipi? Je unatabia nzuri, unatabia mbaya, mpole, una hekima, mwizi n.k. jibu unalo mwenyewe.

Rafiki na ndugu/ wazazi wangu wanasema mimi ni nani?
Je mtu akija leo hii kwenu akauliza wazaizi wako nao wakasema ukweli kuhusu wewe bila kuficha kitu watasema wewe uko vipi, kuna watu wakiwa mbele za watu wanaficha tabia zao mbaya wakiwa mbali na kwao lakini wakiwa kwao wanatabia chafu. Mfano unaweza kuona msichana akiwa mbele za watu anakula chakula kidogo mno lakini akiwa kwao hadi anagombania chakula na wadogo zake.

Mungu anasema mimi ni nani?
Hivi ulishawahi jiuliza unahisi Mungu wako anafahamu wewe ni nani, je wewe ni mpole, mwenye dhambi, mchaji, mwenye hekima n.k. kumbuka kabla ya kutungwa kwenye mamba ya mama yako ulianza kutungwa kwenye fikra za Mungu kwahiyo anakufahamu zaidi unavyojifahamu. jibu unalo mwenyewe.

Kwanini nipo hapa duniani?
Ushajiuliza kwanini upo duniani nab ado upo hai na mzima wa afya wakati kila siku watu wanafariki na wengine ni wagonjwa hawajiwezi. Upo hapa duniani tumtumikie mungu na kumuabudu. Utafahamu kusudi lako (purpose) mungu kukuumba na kukuweka hapa duniani kwa kumcha na kumuomba Mungu. Zaburi 13.9, muhubiri 7:13

Nilitoka wapi?
Jiullize mimi nilitoka wapi? binnadam origin yake imegawanyika sehemu mbili. Kwanza mwanadamu anatoka kwa Mungu yaani kuumbwa toka kwenye fikra za Mungu hadi kuwekwa kwenye tumbo la mama yake. Pili familia anayotokea ndio chimbuko lake la pili hata akijitambulisha atasema anatoka familia Fulani lakini kiuhalisia anatoka kwa MUNGU. Mwanzo 1-1, Yohana 1:1-5

Je nifanye nini?

Baada ya kujiuliza maswali hayo hapo juu na kuona udhaifu wako ulipo juu ya kujitambua basi fanya haya ili kuwasha taa ya ufahamu ndani ya ubongo wako. Mwalimu wangu alikua ananiambia batani ya kuwasha taa ya kujitambua ndani ya ubongo unayo mikononi mwako uamuzi ni wako kuwasha upate mwanga au uendelee kukaa giza.
Fanya haya :-
Mche na kumuomba mungu
  • Jiongezee maarifa kwa kusoma vitu mbalimbali kila siku
  • Kusudia mwenyewe kutaka kujitambua
  • Tengeneza utofauti wako na watu wengine
  • Ongeza thamani ya kile unachokifanya
REFERENCE
Katika kuandika bandiko hili nimetumia rejea mbalimbali kama vuile.
  1. Biblia ya Gideon Version
  2. Katekisimu katoliki jimbo la iringa toleo la kumi na mbili 2013
  3. Kitabu cha The purpose driven to life by Rick waren
  4. Google

Written by
Da’Vinci
Jf expert member.
Meaning of great thinker

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongereni
Namshukuru Mungu leo nimetoa mzigo mzito uliokuwepo kichwani toka mwezi wa 2 nilikua nafikiria kuandika hiki kitu japo nimeandika kwa uchache kulinganisha na kile nachofahamu.
Natamani vijana wenzangu wote wapate elimu ya kujitambua ila hawapendi kusoma.
Natamani ningekua nakipaji cha kuzungumza vizuri .
Asante Kwa Somo Zuri Nimelipenda Mungu Anisaidie Kujitambua
 
Back
Top Bottom