Watu wanasema mimi ni nani? Swali alilouliza Yesu linalofungua ubongo wa mwanadamu kujitambua

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,678
106,786
Salute comrades
NB: bandiko hili nimetumia maandiko ya biblia hata kama unaona haikuhusu nakusihi endelea kusoma unaweza pata kitu.

Katika dunia yetu hii tumeona ni sentensi ya maneno kadhaa tu ndio imeubadirisha huu ulimwengu wetu na kuufanya uendelee. Unaweza kuona sentensi kama vile Newton’s laws of motion zilivyochangia maandeleo ya dunia yetu karibia asilimmia 50 ya maendeleo ya ulimwengu yanaweza kuwa yameletwa na hizo sentesi (laws) tatu za mwanasayansi Issac Neawton kiteknolojia, kiuchumi, pia katika mafunzo ya kiroho hizo laws tatu zinafanya kazi. Au unaweza kuona formula ya E= mc2 ya mwanasayansi Albert Einstein ilivyopelekea mauaji ya mamilioni ya watu huko Hiroshima na Nagasaki Japan, aidha mwanasayansi toka ugiriki Archimedes sentsnsi yake kuhusu kuzama na kuelea kwa kitu ilivyoleta maendeleo makubwa kwenye usafiri wa maji nk. Hivyo unaweza kuona kua hua ni sentensi au maneno ya mtu ndio yameleta makubwa hapa duniani baada ya kuchambuliwa na kufanyiwa kazi.

Swali alilouzaYesu wanafunzi wake linavyowasha taa ya kujitambua kichwani mwa binaadamu.

Luka 9:18-21 "Yesu aliwauliza wanafunzi wake kua je makutano hao wanasema ya kua mimi ni nani? Wanafunzi wake wakajibu yohana mbatizaji wengine wanasema wewe ni Eliya lakini petro akamjibu kua Ndiwe Kristo wa Mungu".

lengo la mada yangu ni kufundisha juu ya mtu kujitambua yeye ni nani (to know your identity), katika swali hilo alilouuliza yesu unaweza kuona ni swali rahisi tu lakini likichambuliwa limebeba ufunguo wa kufungua akili ya mtu kujitambua.
Maneno ya muhimu kwenye swali hiyo ni watu wanasema mimi kua ni nani? Yesu alipouliza swali hilo sio kwamba alikua anataka wamwambie jina lake hasha alitaka afahamu je watu wanamjua yeye ni nani, ndipo petro anamjibu kua ni Kristo wa Mungu. Je nawe ushajiuliza wewe ni nani na watu wanasema wewe ni nani? Twende nikupatie majibu.

Mimi ni nani?
Hapo ulipo anza kujiuliza maswali haya na ujijibu mwenyewe,
Je hivi nilivyo ndivyo natakiwa niwe? Yaani ukijiangalia tabia zako, matendo yako ndivyo unatakiwa uwe? Jibu unalo.

Watu wanasema mimi ni nani?
Ulishwahi kuona mtu Fulani akitaka kumchumbia binti Fulani anaanza kwanza kuulizia kwa watu wanaomfahamu kama vile majirani, mrafiki ni kwasababu watu wa pembeni wanakufahamu zaidi, je leo hii wewe memba mwenzangu wa jf mtu akiuyliza jirani zako kua wewe ni nani atajibu vipi? Je unatabia nzuri, unatabia mbaya, mpole, una hekima, mwizi n.k. jibu unalo mwenyewe.

Rafiki na ndugu/ wazazi wangu wanasema mimi ni nani?
Je mtu akija leo hii kwenu akauliza wazaizi wako nao wakasema ukweli kuhusu wewe bila kuficha kitu watasema wewe uko vipi, kuna watu wakiwa mbele za watu wanaficha tabia zao mbaya wakiwa mbali na kwao lakini wakiwa kwao wanatabia chafu. Mfano unaweza kuona msichana akiwa mbele za watu anakula chakula kidogo mno lakini akiwa kwao hadi anagombania chakula na wadogo zake.

Mungu anasema mimi ni nani?
Hivi ulishawahi jiuliza unahisi Mungu wako anafahamu wewe ni nani, je wewe ni mpole, mwenye dhambi, mchaji, mwenye hekima n.k. kumbuka kabla ya kutungwa kwenye mamba ya mama yako ulianza kutungwa kwenye fikra za Mungu kwahiyo anakufahamu zaidi unavyojifahamu. jibu unalo mwenyewe.

Kwanini nipo hapa duniani?
Ushajiuliza kwanini upo duniani nab ado upo hai na mzima wa afya wakati kila siku watu wanafariki na wengine ni wagonjwa hawajiwezi. Upo hapa duniani tumtumikie mungu na kumuabudu. Utafahamu kusudi lako (purpose) mungu kukuumba na kukuweka hapa duniani kwa kumcha na kumuomba Mungu. Zaburi 13.9, muhubiri 7:13

Nilitoka wapi?
Jiullize mimi nilitoka wapi? binnadam origin yake imegawanyika sehemu mbili. Kwanza mwanadamu anatoka kwa Mungu yaani kuumbwa toka kwenye fikra za Mungu hadi kuwekwa kwenye tumbo la mama yake. Pili familia anayotokea ndio chimbuko lake la pili hata akijitambulisha atasema anatoka familia Fulani lakini kiuhalisia anatoka kwa MUNGU. Mwanzo 1-1, Yohana 1:1-5

Je nifanye nini?
Baada ya kujiuliza maswali hayo hapo juu na kuona udhaifu wako ulipo juu ya kujitambua basi fanya haya ili kuwasha taa ya ufahamu ndani ya ubongo wako. Mwalimu wangu alikua ananiambia batani ya kuwasha taa ya kujitambua ndani ya ubongo unayo mikononi mwako uamuzi ni wako kuwasha upate mwanga au uendelee kukaa giza.
Fanya haya :-
Mche na kumuomba mungu​
  • Jiongezee maarifa kwa kusoma vitu mbalimbali kila siku​
  • Kusudia mwenyewe kutaka kujitambua​
  • Tengeneza utofauti wako na watu wengine​
  • Ongeza thamani ya kile unachokifanya​
REFERENCE
Katika kuandika bandiko hili nimetumia rejea mbalimbali kama vuile.​
  1. Biblia ya Gideon Version​
  2. Katekisimu katoliki jimbo la iringa toleo la kumi na mbili 2013​

Written by
Da’Vinci
Jf expert member.​
 
Hongereni

Namshukuru Mungu leo nimetoa mzigo mzito uliokuwepo kichwani toka mwezi wa 2 nilikua nafikiria kuandika hiki kitu japo nimeandika kwa uchache kulinganisha na kile nachofahamu.

Natamani vijana wenzangu wote wapate elimu ya kujitambua ila hawapendi kusoma.

Natamani ningekua nakipaji cha kuzungumza vizuri.
 
Back
Top Bottom