Watu waliokufa kipindi ambacho hata dini ya ukristo na uislam hazijaanzishwa wako wapi kama tunajiaminisha kwa kusema dini humfanya mtu kuona pepo?

Kabla sijakujibu swali lako,naomba unijibu swali hili.

Unaweza kuniambia ni lini haoa duniani hapajawahi kuwa na DINI ?

Ukinijibi swali,hilo nitakuja kukuonyesha vipi ulitakiwa kuuliza swali na nitakuoa majibu pia.
nakujibu kwa kukuuliza hivi kabla adam na hawa pamoja na uzao wao kuumbwa na kuishi katika dunia je palikuwa na dini? Au je walianza kuumbwa wao ndipo ikafuata dunia?
 
Kwny uislam mtume wa kwanza ni nabii Adam (a.s) na ndie binadamu wa kwanza, sasa iweje useme wapo binadamu waliokuwepo kabla ya uislam
sasa huyo adam alikuwa dini gani? Kwa maana ni dhairi mtume muhamadi alikuwa muislam ila nae ni mtume....na ukisema kwamba uislam ulikuwepo kabla ya muhamadi sasa inakuaje mitume na manabii nyuma ya muhamadi hawakunena neno lolote juu ya uwepo wa uislam kama ilivyo nenwa kwa uwepo wa dini ya wayahudi kipindi cha manabii na mitume hao? Na pia je katika uumbaji wa dunia na viumbe vyote ndani yake je Mungu alinena juu ya kuumba dini hiyo ya uislam kipindi cha uumbaji wake?
 
Before Christ (BC), watu waliishi freshi tu kwa imani zao na maisha yalienda!
Haya mambo ya dini tumeletewa tu na wametukamata kwa sasa. Ni bakora nyingine tumeletewa ya kutuchapa!
 
sasa huyo adam alikuwa dini gani? Kwa maana ni dhairi mtume muhamadi alikuwa muislam ila nae ni mtume....na ukisema kwamba uislam ulikuwepo kabla ya muhamadi sasa inakuaje mitume na manabii nyuma ya muhamadi hawakunena neno lolote juu ya uwepo wa uislam kama ilivyo nenwa kwa uwepo wa dini ya wayahudi kipindi cha manabii na mitume hao? Na pia je katika uumbaji wa dunia na viumbe vyote ndani yake je Mungu alinena juu ya kuumba dini hiyo ya uislam kipindi cha uumbaji wake?
hivi kumbukumbu za Muhammad zinaanzia wapi yaani mwaka gani? je ni BC au?
 
Wafia dini wengi ni mambumbumbu..
Akili zao wote wamemkabidhi mbumbumbu mmja wanaomwita mchungaji/nabii/mwalimu/nk

Wanabebana na Vitabu vya natural science (bible/quran)..kama mapambo hata kuelewa kilichomo ndani hawaelewi..nikuvisoma kama story book tuu nakurudia kilichoandikwa
Wewe umefanya tafit au unaropoka km malaya aloshiba pombe
 
Mimi naelewa hivi: Imani ni uhusiano wa ndani (inner relationship) kati ya Mungu na mwanadamu na dini ni 'external expression' (mwonekano wa imani mtu kwa nje). Kwa maneno mengine, uhusiano wa mtu na Mungu (imani) unaonekana kwa nje kupitia dini. Wanadamu wote duniani (hata kwa nchi kama Korea Kaskazini na China) wana imani na dini. Yaani kila jamii ya watu wana idea of God kwa namna yoyote ile na ndiyo maana katika jamii zote za wanadamu yale mambo wanayoyaona ni mema ni mema hata kwa jamii nyingine na yale wanayoyaona ni mabaya ni mabaya pia kwa jamii nyingine. Hii inaonyesha universality ya Amri 10 za Mungu - kila jamii ya wanadamu wanazo na wanaweza kuzi'express' kwa namna tofauti, lakini in essence ni zilezile. Hivyo, wokovu ni kwa wanadamu wote - wale 'watakaoamini wataokoka' na 'wasioamini wataangamia'.
VITU AMBAVYO NI ABSOLUTE NAWEZA SEMA NI COINCIDENCE, KTK RELATIVISM.
 
Naona mmeatuamulia,kwani kila mtu si afanye yake tuacheni wafia dini .......
 
Kuna baadhi ya watu huaminisha watu kuwa dini yao ni ya kweli na bila hiyo dini huwezi ona mbingu na ukiangalia dini na watu cha kwanza ni watu na dini zilikuja kwa baadae sasa je waliokufa kipindi dini hazijaletwa wamekwenda motoni au? tusaidiane kuwekana sawa hapa ila kwa mawazo yangu naamini kwa walio tenda mema wamekwenda peponi ila waovu ni motoni...vipi wewe unasemaje?
Unafikiri ama niseme nilisikia kuna mahali pameandikwa:

''Watahukumiwa kwa kile walichokiamini''

Hata wale wapagani wa Israel na huko Mecca waliokuwepo kabla ya DINI ila walikuwa na IMANI.

Hivyo waliokuwa waaminifu na watenda haki katika Imani hiyo hawatahukumiwa tofauti na wale waliokuwa waasi wasiotenda mema kwa wenzao.

Ndio maana kabla ya Dini hizo kuwepo kulikuwa na IMANI tofauti.



NILIAMINISHWA HILO
 
Ongea point kidogo basi acha kudanganya. Au Quraan inakuambia udanganye? Mwislam wa kwanza alikuwa Muhamad tena according to Quraan yako. Na alieshushiwa hiyo alikuwa Muhamad. Usiongee uongo
Pimbi uliyepindukia nan kakudanganya muislam wa Kwanzaa Muhammad tako ww.
Hatta kuran huijui
 
sasa huyo adam alikuwa dini gani? Kwa maana ni dhairi mtume muhamadi alikuwa muislam ila nae ni mtume....na ukisema kwamba uislam ulikuwepo kabla ya muhamadi sasa inakuaje mitume na manabii nyuma ya muhamadi hawakunena neno lolote juu ya uwepo wa uislam kama ilivyo nenwa kwa uwepo wa dini ya wayahudi kipindi cha manabii na mitume hao? Na pia je katika uumbaji wa dunia na viumbe vyote ndani yake je Mungu alinena juu ya kuumba dini hiyo ya uislam kipindi cha uumbaji wake?
Asee umedanganya kasome surat maryam uondoe ujinga
 
Nadhani swali lako limelenga dini zoote japo hujataka kuwa specific unataja dini gani,kwa kuwa mimi ni kristo nitalijibu swali lako kikriso zaidi kwa kutumia maandiko ya kwenye kitabu cha biblia uwe unakiamini au hukiamini ndio muongozo wetu sisi wakristo kwenye hii safari ya kuelekea peponi,kimejaa majibu yoote yanayohusu dini yetu,na pia wenzangu wa dini zingine watakuja kujibu kwa namna watakavyoona inafaa.
Kwa sisi wakristo katika dini yetu kuna makanisa mawili,kuna kanisa la kwanza lililokuwa chini ya sheria,na kanisa la pili ambalo tupo sasa chini ya neema,kwa lugha nyingine ningeweza kuandika kuwa kuna nyumba mbili,nyumba ya kwanza iliyokuwa chini ya sheria na nyumba ya pili iliyo chini ya neema ndiomaana ndani ya biblia imeandikwa utukufu wa kanisa(nyumba) ya mwisho utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa kanisa(nyumba) la kwanza (HAGAI 2:9)
1.KANISA(NYUMBA) LA KWANZA
Hii inajumuisha watu woote waliokuwepo tangia kuumbwa kwa dunia hadi siku ile ya pentekosti Roho mtakatifu anawashukia mitume,watu waliokuwa chini ya hili kanisa walikuwa chini ya Neema ya Mungu mwenyewe kama wakiwa na imani kwake.
2.KANISA(NYUMBA) LA PILI
Hii inajumuisha watu woote tangia siku ile ya pentekosti Roho mtakatifu kashuka duniani hadi sasa hivi,kanisa la sasahivi linaitwa kanisa la Neema,tunaokolewa kwa kuisikia INJILI, na sio tena zile sheria za torati na manabii, na injili ni rahisi imeandikwa UTUBU,UBATIZWE UJAZWE ROHO MTAKATIFU ndio injili waliyoagizwa mitume hizo ndio habari njema tulizoambiwa.
Huwa sipendi kujibu maswali kwa juu juu ndio maana nimeanza kuelezea kanisa la kwanza na kanisa la pili la leo,sasa nikirudi kwenye swali lako umeuliza kwanza watu kabla ya hii INJILI (DINI) haijaja walikwenda wapi??,Jibu ni hivi woote walikuwa wanakwenda chini kuzimu(Chini ya nchi),! isipokuwa kuzimu ilikuwa imegawanywa kulikuwa na mpaka kati ya watu waliokuwa wamefanya matendo mema kwa mujibu wa imani zao kwa Mungu na watu waliokuwa wamefanya matendo mabaya ambao hawakumuamini MUNGU
Sehemu walipokuwa wanaenda waliotenda matendo mema palikuwa pamepewa jina la "KIFUANI PA ABRAHAM" kati ya hizi sehemu Mbili kulikuwa pametenganishwa na shimo kubwa wa huku hawezi kwenda kule na wa kule hawezi kuja huku rejea mfano wa Yesu (LUKA 16:19-21),Watakatifu wa kanisa la kwanza walikuwa wanakwenda hapa 'kifuani pa ibrahimu" kama sehemu ya kupumzikia sababu wao walikuwa watakatifu ambao dhambi zao zilikuwa zimesafishwa kwa kafara ya wanyama (kama kondoo na ng'ombe') sasa kafara halisi ya Yesu ilikuwa haijaja bado na kwa kuwa Yesu pekee ndio njia ya kwenda mbinguni iliwapasa hawa watakatifu wa kwanza wasubiri kifuani pa ibrahimu hadi Yesu atakavyokuja!.iliwapasa watu waliokufa kabla ya Yesu kuja nao Wasikie/Wahubiriwe INJILI kusudi siku ya mwisho asiwepo mwanadamu ambaye atasema hakuisikia injili kwa kuwa Mungu ni Mungu wa Haki hukumu zake ni za haki! (1Petro 4:1-6)
Yesu alivyokufa aliwaendea wafu waliokuwa wamekufa kabla ya kuja kwake kwenda kuwahubiria injili na hao waliomkubali siku walifufuliwa na wakawatokea watu wengi! (Mathayo 27:51-53),
kumalizia kwa mujibu ya sisi wakristo na hayo maandiko niliyoyaweka hapo,watu woote siku ya mwisho watahukumiwa kwa INJILI sababu woote waliisikia INJILI waliokuwa wamekufa kabla ya INJILI kuja duniani na ambao tupo kipindi hiki cha INJILI na ndiomaana hadi Yesu anakuja mara ya pili INJILI itakuwa imeshahubiriwa kila kona ya DUNIA kila mtu atakuwa kaisikia INJILI
"TUBU,BATIZWA KWA JINA LA YESU KRISTO, POKEA ROHO MTAKATIFU" utaokolewa
Mkuu asante hii nilikua sijui
 
sasa huyo adam alikuwa dini gani? Kwa maana ni dhairi mtume muhamadi alikuwa muislam ila nae ni mtume....na ukisema kwamba uislam ulikuwepo kabla ya muhamadi sasa inakuaje mitume na manabii nyuma ya muhamadi hawakunena neno lolote juu ya uwepo wa uislam kama ilivyo nenwa kwa uwepo wa dini ya wayahudi kipindi cha manabii na mitume hao? Na pia je katika uumbaji wa dunia na viumbe vyote ndani yake je Mungu alinena juu ya kuumba dini hiyo ya uislam kipindi cha uumbaji wake?
Hakua na dini ila alikua akitii maagizo ya Mungu na alipokosa Mungu alimuadhibu.
 
nakujibu kwa kukuuliza hivi kabla adam na hawa pamoja na uzao wao kuumbwa na kuishi katika dunia je palikuwa na dini? Au je walianza kuumbwa wao ndipo ikafuata dunia?

Hujajibu swali kwa kuuliza sababu swali lako ni la uongo.

Adamu ndio kiumbe cha mwisho kuumbwa vipi uulize swalo la kuanza au kufata katika kuumbwa ?
 
Mungu anaujua mwanzo wako n mwisho wako sasa kwanini wakati anajua wewe mwisho wako ni jehanam na alikuumba hivyo hivyo uishi... Kwanini asikuumbe na kukupeleka jehanam moja kwa moja?

Kwani Mungu akikuchoma moto atakua anafaidika na nn? Ama sisi tutajifunza nn maana hatuoni huo moto ukiwachoma zaidi ya kutishana tuu
 
unasema swali la uongo? Yan liwe swali alaf tena liwe la uongo? Jibu bhana kwanza hata kwa uongo kama ni la uongo

Kuna uongo wa kauli na vitendo,na swali lako limeingia katika uongo wa kauli. Fikiria kwanza utaona,hii nafanya hivi ili muwe makini katika kuuliza maswali na kujenga hoja sio una hoji hoji tu kitoto.
 
Kuna uongo wa kauli na vitendo,na swali lako limeingia katika uongo wa kauli. Fikiria kwanza utaona,hii nafanya hivi ili muwe makini katika kuuliza maswali na kujenga hoja sio una hoji hoji tu kitoto.
kiufupi hauna jibu wewe
 
Back
Top Bottom