"Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza

Wanabodi,
Niko kwenye voluntariy lockdown, hivyo leo nimapata fursa ya kuangalia TV ya Zanzibar, ZBC, Mwandishi wa habari wa CCM Zanzibar, Daudi Ismail anamhoji Makamo wa Rais wa JMT, Mhe. Samia Suluhu Hassan anauzungumzia Muungano, kiukweli huyu Mama Samia anauzumguza vizuri muungano huku akiongea kwa heshima, taratibu, kwa utulivu na unyenyekevu, na anaongea vizuri mpaka raha, na kwa wale wenzangu na mimi wenye udhaifu na macho fulani, kiukweli Mwenyenzi Mungu amemjaalia macho mashaalah, huchoki kumsikiliza, utatamani aendelee tuu kuongea na kipindi kisiishe!.

Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.

Anasema Zanzibar inafaidika sana na muungano, kisiasa, kiuchumi na kijamii, ikiwemo kufaidika kielimu, wakati wa muungano, Zanzibar haikuwa na chuo kikuu chake hivyo Wanzanzibari wote wa enzi hizo waliofika elimu ya vyuo vikuu, wamesomea bara.

Mama Samia amesema watu waachiwe kuujadili muungano kadri watakavyo na hata kutema nyongo kuhusu muungano, na serikali inazitumia hizo hoja zinazolalamikiwa kuimarisha muungano, akasema ni heri watu wafunguke na kusema hivyo kuyatoa madukuduku yao, kuliko kunyamaza na madukuduka ndani yao, siku wakilipuka moto utawaka, hivyo watu waachwe waseme.

Amesema Zanzibar ni visiwa hivyo viko wazi pande zote, hivyo faida kubwa kabisa ya muungano ni ulinzi usalamax amani na na utulivu wa Zanzibar, bila muungano, ilikuwa ni rahisi sana kuivamia Zanzibar na Zanzibar ikivamiwa ni rahisi sana kuivamia bara, hivyo muungano umeimarisha sana ulinzi na usalama, amani na utulivu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kuna kitu Mama Samia amekisema sikuwahi kukijua!. Kumbe Wizara ya Mambo ya Nje ilipokiwa ikiitwa Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ndio ilikuwa ya Muungano iki handle issues zote za Zanzibar kimataifa, lakini , ilipobadilishwa jina na kuitwa Wizara ya Mambo, ya Nje na Ushirikiano wa Africa Mashariki, sasa ina handle mambo ya Zanzibar ndani ya Africa Mashariki tuu, lakini kimataifa, kwa yale mambo ambayo sio ya muungano, SMZ ya Zanzibar imepewa uhuru wa kunegotiate ufadhili, misaada, na mikopo na mikataba ya kimataifa kwaniaba ya Zanzibar, ila kwenye kutiliana saini, anayetia saini ni serikali ya JMT, kwasababu Zanzibar haina sovereignty, sovereignty ni moja tuu ambayo iko kwenye JMT pekee!.

Hili sikuwahi kulijua, hivyo kumbe sasa Zanzibar inaweza kupata misaada na mikopo ya kimataifa, sasa kwavile uwiano wa kugawana misaada ya kutoka nchi wafadhili na wahisani, Zanzibar inastahili kupata asilimia 4.5% ya misaada yote kwa Tanzania, sasa kwa vile Zanzibar nayo inaweza kuomba ufadhili wa kimataifa, jee hii misaada ya kimataifa ya Zanzibar inayoomba, Tanzania bara pia tunapewa ule mgao wa asilimia 95.5% ya misaada ya Zanzibar, au misaada ya Tanzania tuu, ndio Zanzibar inapaswa kugaiwa asilimia 4.5%, lakini kwa misaada ya Zanzibar, then misaada hiyo ni ya Zanzibar pekee?.

Mama Samia amezungumzia kero za muungano na kusema kero nyingi zimeisha tatuliwa ila utekelezaji ndio unasua sua, na kutolea mfano deni lililokuwa la umeme la Tanesco, deni hilo lilisababishwa na double taxation, kwa Tanesco kuwachaji SMZ VAT huku shirika la umeme la Zanzibar, Zesco nalo likiwachaji kodi ya ongezeko la thamani Vat, wateja watumiaji wa umeme zao nao wakilipishwa Vat, kero hiyo imetatuliwa kwa Tenesco hawaichaji tena Vat kwa SMZ, hivyo Zanzibar haidaiwi tena deni lolote la umeme na Tanesco.

Ninachokumbuka kwenye deni la umeme la Zanzibar, lilitokana na Tenesco kuuza umeme kwa bei ya juu kwa Zesco, halafu Zesco wanauza umeme huo kwa bei ya chini Zanzibar, kumbe ilikuwa ni issue ya VAT!.

Pia amezungumzia kero za muungano kadri zinavyotatuliwa, kero nyingine zinaibuka, hivyo issue za kero za muungano ni issue endelevu.

Kuhusu usawa wa kijinsia kwenye uongozi, amesema Mungu aliumba jinsia tofauti kwa maana yake, hivyo ni vizuri wanawake wakajikubali kwa uanawake wao na kutimiza majukumu ya wanawake kama dini na Mungu alivyodhamiria, na wanaume nao watimize majukumu yao, nafasi za kazi au uongozi zisifanye wanawake kujisahau majukumu yao ya kutunza familia, na kuipongeza Tanzania, wanawake na wanaume ni sawa, akatolea mfano kuna nchi wanawake na wanaume wanafanya kazi ile ile lakini wanawake wanalipwa pungufu ya wanaume, na kuna nchi, wanawake ndio wazalishaji mali lakini hawaruhusiwi kupokea mshahara, siku ya mshahara, waume zao ndio wanakuja kuwapokelea. Tanzania mishahara inafanana na wanawake wanaruhusiwa kuingiza kipato.

Alipoulizwa kuhusu malalamiko ya watalii licha ya kuingia Tanzania na passport zao kugongwa entry, lakini wakifika Zanzibar, wanakaguliwa tena na kujaza fomu upya, Mama Samia alisema hizo ni hatua za kawaida za kiusalama, hata yeye kufuatia kuwa na jina la Hassan na kuna nchi alifika na ujumbe wa Tanzania, wengine wote waliruhusiwa yeye akazuiliwa kwa saa kadhaa hadi walioojiridhisha ndipo akaruhusiwa.

Amezungumza mengi na kumalizia kwa kusisitiza Muungano ni jambo jema, tuulinde na kuuenzi.

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Rejea
Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth! - JamiiForums

Siku ya Wanawake Duniani: Je, Tuna Wanawake Wenye Sifa za Presidential Material?! - JamiiForums

Wajue The Top Five Most Prominent Members wa Bunge Maalum la Katiba!. - JamiiForums

New Cabinet: Baadhi ya Majina ni Haya Hapa!. - JamiiForums

Makamu wa Rais, Samia Suluhu aweza kuendana na kauli za Rais Magufuli - JamiiForums
hahahaaa Zamu yake sasa
 
Wanabodi,
Niko kwenye voluntariy lockdown, hivyo leo nimapata fursa ya kuangalia TV ya Zanzibar, ZBC, Mwandishi wa habari wa CCM Zanzibar, Daudi Ismail anamhoji Makamo wa Rais wa JMT, Mhe. Samia Suluhu Hassan anauzungumzia Muungano, kiukweli huyu Mama Samia anauzumguza vizuri muungano huku akiongea kwa heshima, taratibu, kwa utulivu na unyenyekevu, na anaongea vizuri mpaka raha, na kwa wale wenzangu na mimi wenye udhaifu na macho fulani, kiukweli Mwenyenzi Mungu amemjaalia macho mashaalah, huchoki kumsikiliza, utatamani aendelee tuu kuongea na kipindi kisiishe!.

Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.

Anasema Zanzibar inafaidika sana na muungano, kisiasa, kiuchumi na kijamii, ikiwemo kufaidika kielimu, wakati wa muungano, Zanzibar haikuwa na chuo kikuu chake hivyo Wanzanzibari wote wa enzi hizo waliofika elimu ya vyuo vikuu, wamesomea bara.

Mama Samia amesema watu waachiwe kuujadili muungano kadri watakavyo na hata kutema nyongo kuhusu muungano, na serikali inazitumia hizo hoja zinazolalamikiwa kuimarisha muungano, akasema ni heri watu wafunguke na kusema hivyo kuyatoa madukuduku yao, kuliko kunyamaza na madukuduka ndani yao, siku wakilipuka moto utawaka, hivyo watu waachwe waseme.

Amesema Zanzibar ni visiwa hivyo viko wazi pande zote, hivyo faida kubwa kabisa ya muungano ni ulinzi usalamax amani na na utulivu wa Zanzibar, bila muungano, ilikuwa ni rahisi sana kuivamia Zanzibar na Zanzibar ikivamiwa ni rahisi sana kuivamia bara, hivyo muungano umeimarisha sana ulinzi na usalama, amani na utulivu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kuna kitu Mama Samia amekisema sikuwahi kukijua!. Kumbe Wizara ya Mambo ya Nje ilipokiwa ikiitwa Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ndio ilikuwa ya Muungano iki handle issues zote za Zanzibar kimataifa, lakini , ilipobadilishwa jina na kuitwa Wizara ya Mambo, ya Nje na Ushirikiano wa Africa Mashariki, sasa ina handle mambo ya Zanzibar ndani ya Africa Mashariki tuu, lakini kimataifa, kwa yale mambo ambayo sio ya muungano, SMZ ya Zanzibar imepewa uhuru wa kunegotiate ufadhili, misaada, na mikopo na mikataba ya kimataifa kwaniaba ya Zanzibar, ila kwenye kutiliana saini, anayetia saini ni serikali ya JMT, kwasababu Zanzibar haina sovereignty, sovereignty ni moja tuu ambayo iko kwenye JMT pekee!.

Hili sikuwahi kulijua, hivyo kumbe sasa Zanzibar inaweza kupata misaada na mikopo ya kimataifa, sasa kwavile uwiano wa kugawana misaada ya kutoka nchi wafadhili na wahisani, Zanzibar inastahili kupata asilimia 4.5% ya misaada yote kwa Tanzania, sasa kwa vile Zanzibar nayo inaweza kuomba ufadhili wa kimataifa, jee hii misaada ya kimataifa ya Zanzibar inayoomba, Tanzania bara pia tunapewa ule mgao wa asilimia 95.5% ya misaada ya Zanzibar, au misaada ya Tanzania tuu, ndio Zanzibar inapaswa kugaiwa asilimia 4.5%, lakini kwa misaada ya Zanzibar, then misaada hiyo ni ya Zanzibar pekee?.

Mama Samia amezungumzia kero za muungano na kusema kero nyingi zimeisha tatuliwa ila utekelezaji ndio unasua sua, na kutolea mfano deni lililokuwa la umeme la Tanesco, deni hilo lilisababishwa na double taxation, kwa Tanesco kuwachaji SMZ VAT huku shirika la umeme la Zanzibar, Zesco nalo likiwachaji kodi ya ongezeko la thamani Vat, wateja watumiaji wa umeme zao nao wakilipishwa Vat, kero hiyo imetatuliwa kwa Tenesco hawaichaji tena Vat kwa SMZ, hivyo Zanzibar haidaiwi tena deni lolote la umeme na Tanesco.

Ninachokumbuka kwenye deni la umeme la Zanzibar, lilitokana na Tenesco kuuza umeme kwa bei ya juu kwa Zesco, halafu Zesco wanauza umeme huo kwa bei ya chini Zanzibar, kumbe ilikuwa ni issue ya VAT!.

Pia amezungumzia kero za muungano kadri zinavyotatuliwa, kero nyingine zinaibuka, hivyo issue za kero za muungano ni issue endelevu.

Kuhusu usawa wa kijinsia kwenye uongozi, amesema Mungu aliumba jinsia tofauti kwa maana yake, hivyo ni vizuri wanawake wakajikubali kwa uanawake wao na kutimiza majukumu ya wanawake kama dini na Mungu alivyodhamiria, na wanaume nao watimize majukumu yao, nafasi za kazi au uongozi zisifanye wanawake kujisahau majukumu yao ya kutunza familia, na kuipongeza Tanzania, wanawake na wanaume ni sawa, akatolea mfano kuna nchi wanawake na wanaume wanafanya kazi ile ile lakini wanawake wanalipwa pungufu ya wanaume, na kuna nchi, wanawake ndio wazalishaji mali lakini hawaruhusiwi kupokea mshahara, siku ya mshahara, waume zao ndio wanakuja kuwapokelea. Tanzania mishahara inafanana na wanawake wanaruhusiwa kuingiza kipato.

Alipoulizwa kuhusu malalamiko ya watalii licha ya kuingia Tanzania na passport zao kugongwa entry, lakini wakifika Zanzibar, wanakaguliwa tena na kujaza fomu upya, Mama Samia alisema hizo ni hatua za kawaida za kiusalama, hata yeye kufuatia kuwa na jina la Hassan na kuna nchi alifika na ujumbe wa Tanzania, wengine wote waliruhusiwa yeye akazuiliwa kwa saa kadhaa hadi walioojiridhisha ndipo akaruhusiwa.

Amezungumza mengi na kumalizia kwa kusisitiza Muungano ni jambo jema, tuulinde na kuuenzi.

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Rejea
Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth! - JamiiForums

Siku ya Wanawake Duniani: Je, Tuna Wanawake Wenye Sifa za Presidential Material?! - JamiiForums

Wajue The Top Five Most Prominent Members wa Bunge Maalum la Katiba!. - JamiiForums

New Cabinet: Baadhi ya Majina ni Haya Hapa!. - JamiiForums

Makamu wa Rais, Samia Suluhu aweza kuendana na kauli za Rais Magufuli - JamiiForums
kipindi hicho SSH hajajitoa ufahamu na kuungana na akina Kagama , Bokassa, Iddi Amin, Nkurunziza, Moboto, na wenzao .
 
wewe unasema Elimu ya Uraia ni muhimu.Ni muhimu kweli ili watu wafunguke akili.. Nafikiri ni mtu mpumbavu tuu anayekubaliana na muundo wa huu Muungano. Marehemu Mch Christopher Mtikila ndio pekee aliweza kuudadavua huu Muungano unavyoiathiri Tanganyika. Nafikiri Mzee Pascal Mayala unazo akili na unaelewa vizuri Sana kuhusu hii ishu ya Muungano Ila unataka kubase upande.
Mkuu DASM , siku zote humu jf, mimi ni mkweli Daima kwa kuusema ukweli uliopo no matter what. Nimeandika mengi kuhusu muungano, hili ni moja ya mabandiko hayo.
P
 
Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Ni katika kunikumbusha tuu, hotuba ya Rais Samia UN, imezidi kudhihirisha I was dam right nilipoyasema haya!.
P
 
Wanabodi,
Niko kwenye voluntariy lockdown, hivyo leo nimapata fursa ya kuangalia TV ya Zanzibar, ZBC, Mwandishi wa habari wa CCM Zanzibar, Daudi Ismail anamhoji Makamo wa Rais wa JMT, Mhe. Samia Suluhu Hassan anauzungumzia Muungano, kiukweli huyu Mama Samia anauzumguza vizuri muungano huku akiongea kwa heshima, taratibu, kwa utulivu na unyenyekevu, na anaongea vizuri mpaka raha, na kwa wale wenzangu na mimi wenye udhaifu na macho fulani, kiukweli Mwenyenzi Mungu amemjaalia macho mashaalah, huchoki kumsikiliza, utatamani aendelee tuu kuongea na kipindi kisiishe!.

Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.



Mama

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Samia sio president material. Hana ushawishi wa maneno wala wa vitendo. Hata akisimama jukwaani hana nguvu ya kisiasa.

NB: CCM wakitaka waaibike 2025 wamuweke huyu mama. Watapata aibu ya karne.
I'd like to differ, its the other way round,
na 2025...Utashangaa!.

P
 
Wanabodi,
Niko kwenye voluntariy lockdown, hivyo leo nimapata fursa ya kuangalia TV ya Zanzibar, ZBC, Mwandishi wa habari wa CCM Zanzibar, Daudi Ismail anamhoji Makamo wa Rais wa JMT, Mhe. Samia Suluhu Hassan anauzungumzia Muungano, kiukweli huyu Mama Samia anauzumguza vizuri muungano huku akiongea kwa heshima, taratibu, kwa utulivu na unyenyekevu, na anaongea vizuri mpaka raha, na kwa wale wenzangu na mimi wenye udhaifu na macho fulani, kiukweli Mwenyenzi Mungu amemjaalia macho mashaalah, huchoki kumsikiliza, utatamani aendelee tuu kuongea na kipindi kisiishe!.

Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Duh na wewe kumbe ni mnafiki! Sikujua Hilo. Ulimsifu Sana jpm kuwa ni masihi mpaka ukaunga juhudi, Sasa unajiweka Tena kwa Mana akuone. Hivi huiamnj kabisa kuwa unaweza kuishi bila kulamba lamba watu?
Angalia hoja za bandiko hili na angalia tarehe ya bandiko hili.
P
 
Wanabodi,
Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?.

Paskali
Kama una maono kwa nini ujaona na ...
Karibu
P
 
Back
Top Bottom