Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kumekuwa na imani iliyojengeka na kuenea katika jamii kuwa, RADI ina uhusiano mkubwa na madini kwa maana ya kwamba, madini huvuta radi na kusababisha maeneo yenye madini kuwa na radi za mara kwa mara. Jambo hili lina ukweli wowote kisayansi? Maeneo kama Dodoma ni maeneo kame ambayo hupata mvua chache kwa mwaka, hata hivyo mvua hizo hua zikiambatana na radi kali. Kama madini na radi vina uhusiano huo, nadhani ndicho kinachotokea maeneo ya UDOM kwani chuo hicho kimejengwa kwenye ukanda wa dhahabu unaoanzia maeneo ya kiji cha Nzunguni mpaka katika vilima vya Chimwaga.