Watu wa Mombasa wataka kujitenga na Kenya na kurejea kwao Zanzibar

....Na Pemba wakijitenga na unguja watakimbilia kujiunga tena na Tanganyika...Ungujka watabakia peke yao watashangaa....supply zote zikikata unguja itakuja kuwa njaa bei vitu itapanda maana watakuwa wanalipa ushuru tokl bara kuvusha...fujo zikizuka kutakuwa hakutawaliki tena maana wananchi wataanza kulaumu nani alietaka tuvunje muungano!!!mawazo yangu tu ....

Umejuaje kama wapemba wanataka kujitenga Zanzibar? Hizo ni scaremongering tactics za Nyerere ambazo alitumia ubaguzi kuwatawala vizuri Zanzibar. Angelikuwa hai zama hizi za vijana wa Dot com wasingelichelewa kumuuliza wapi umepata kuwa zanzibar ikijitenga pemba watataka kujitenga? Na nani amewaambia wazanzibari wataanzisha fujo? Unasema zanzibar kutakuwa na fujo nikuulize sawa wazanzibari watakuwa na fujo kwasababu vyakula vinatoka kwetu Tanganyika je wewe bandari ya kupakia na kupakua mizigo ya nchini Tanganyika itatoka wapi? Maana zanzibar bandarini zote kubwa za Dar na Mombasa na Mtwara ni eneo la zanzibar. Isitoshe gesi mnayojivunia na mafuta yaliyopo baharini mtakwenda kwa zanzibar kuwasujudia kuwaomba wawasaidie. Acheni dharau mkuu baadhi yetu watanganyika tunawadharau sana wazanzibari ila vitawatokea puani mie sipendi kutengana ila kwa dharau hizi nishasema tangu zamani nawaunga mkono kabisa ili tuone ni kina nani wataumia zaidi baina yetu na wao.
 
Hii inatukumbusha mbali. Wakati ule Zanzibar ilipokuwa Zanzibar. Wakati ule wa Unguja ni njema, atakaye aje. Wakati ule wa baragumu likipigwa Zanzibar, samaki wa maziwa makubwa hucheza. Zanzibar nakupenda. Bonyeza link ifuatayo: <a href="http://www.mzalendo.net/habari/watu-wa-mombasa-wataka-kujitenga-na-kenya-na-kurejea-kwao-zanzibar-2/attachment/harakati-mrc-4" target="_blank">Watu wa Mombasa wataka kurejea kwao Zanzibar.</a>
<br />
<br />
Leo nimeamini kweli kuna nyege za vidole kutamani kubonyabonya.
 
Hii inatukumbusha mbali. Wakati ule Zanzibar ilipokuwa Zanzibar. Wakati ule wa Unguja ni njema, atakaye aje. Wakati ule wa baragumu likipigwa Zanzibar, samaki wa maziwa makubwa hucheza. Zanzibar nakupenda. Bonyeza link ifuatayo: <a href="http://www.mzalendo.net/habari/watu-wa-mombasa-wataka-kujitenga-na-kenya-na-kurejea-kwao-zanzibar-2/attachment/harakati-mrc-4" target="_blank">Watu wa Mombasa wataka kurejea kwao Zanzibar.</a>
<br />
<br />
Leo nimeamini kweli kuna nyege za vidole kutamani kubonyabonya na kuandika.
 
Jamani..
Huenda ki historia likawa ni la kweli ila kwa sasa since it has already happened na huwezi transform past to the present, ila itaendelea kusimulika kama ni historia.
 
Kwa maana hiyo Zanzibar ilikuwa kubwa kiasi hicho! Sasa kama zanzibar kwa sasa ni ndogo kiasi cha watu milioni moja ( na mimi nikiwemo) inawashinda, je wakiongeza na wamombasa?
 
Umejuaje kama wapemba wanataka kujitenga Zanzibar? Hizo ni scaremongering tactics za Nyerere ambazo alitumia ubaguzi kuwatawala vizuri Zanzibar. Angelikuwa hai zama hizi za vijana wa Dot com wasingelichelewa kumuuliza wapi umepata kuwa zanzibar ikijitenga pemba watataka kujitenga? Na nani amewaambia wazanzibari wataanzisha fujo? Unasema zanzibar kutakuwa na fujo nikuulize sawa wazanzibari watakuwa na fujo kwasababu vyakula vinatoka kwetu Tanganyika je wewe bandari ya kupakia na kupakua mizigo ya nchini Tanganyika itatoka wapi? Maana zanzibar bandarini zote kubwa za Dar na Mombasa na Mtwara ni eneo la zanzibar. Isitoshe gesi mnayojivunia na mafuta yaliyopo baharini mtakwenda kwa zanzibar kuwasujudia kuwaomba wawasaidie. Acheni dharau mkuu baadhi yetu watanganyika tunawadharau sana wazanzibari ila vitawatokea puani mie sipendi kutengana ila kwa dharau hizi nishasema tangu zamani nawaunga mkono kabisa ili tuone ni kina nani wataumia zaidi baina yetu na wao.

Mie nataka leo hii watanganyika tujitenge na hao wazenji na hata wapemba kama wakitaka, hakuna kubembelezana hapa, jitengeni, waiteni wale waarbu wenu, mle halwa na gahawa mpaka mvimbiwe, halafu waarabu wawageuzi tena watumwa!
Wazenji wanajidanganya kwamba watakua poa na vimafuta visivyokua na uhakika, wanajiona bora kuliko wabara wakati asili yao ni bara, kisa kuwa watoto wa nje wa masultani!
Tumechoka na kebei zenu, vunjeni muungano, uunganeni na mombasa, kismayu na hata comoro, tuone kama hamtachapana makonde na kukimbilia bagamoyo!
Bure kabisa hawa watu!
 
..kwani mkataba wa Sultani na Muingereza kuhusu eneo la Mombasa unasemaje?

..halafu who can come out in an organized fashion na ku-claim hayo maeneo yaliyokuwa mali ya Sultani?

..je, wale wakazi wa maeneo yaliyokuwa mali ya Sultani ambao hawataki kujitenga na wenzao wa bara wana haki gani ktk shauri hili?
 
sasa kabla muarabu(Sultani) hajaja na kuwaweka ktk nchi ya Zanzibar walikuwa ktk nchi gani? Au hawakuwepo hapo Mombasa kabla ya Muarabu?
 
..kwani mkataba wa Sultani na Muingereza kuhusu eneo la Mombasa unasemaje?

..halafu who can come out in an organized fashion na ku-claim hayo maeneo yaliyokuwa mali ya Sultani?

..je, wale wakazi wa maeneo yaliyokuwa mali ya Sultani ambao hawataki kujitenga na wenzao wa bara wana haki gani ktk shauri hili?

Wakazi wa maeneo ya pwani asili wengi ndio mnawaita waswahili ndio hao waliwauzia ardhi sultani. Isitoshe ipo mikataba ya kuuziana baina ya machifu wa kizaramo, manyema, wadigo, wabahai na wengineo mombasa, na vile vile wamakonde na kadhalika. Mkataba wa sultani na muingereza ulikuwa si kuuziana bali kusimamia upokeaji wa ushuru katika bandari ya mombasa, wajerumani walikuwa pia na mkataba huo huo na bandari ya Tanga na Dar-es-Salaam. Kilichotokea ni ubabe wa wajerumani na waingereza kuamua kuchukua bandari zote kwa faida zao na ukanda wa pwani.

Nilikuomba siku nyingi unipatie sales agreement hujaweka hadi leo.
 
Mdondoaji said:
Wakazi wa maeneo ya pwani asili wengi ndio mnawaita waswahili ndio hao waliwauzia ardhi sultani. Isitoshe ipo mikataba ya kuuziana baina ya machifu wa kizaramo, manyema, wadigo, wabahai na wengineo mombasa, na vile vile wamakonde na kadhalika. Mkataba wa sultani na muingereza ulikuwa si kuuziana bali kusimamia upokeaji wa ushuru katika bandari ya mombasa, wajerumani walikuwa pia na mkataba huo huo na bandari ya Tanga na Dar-es-Salaam. Kilichotokea ni ubabe wa wajerumani na waingereza kuamua kuchukua bandari zote kwa faida zao na ukanda wa pwani.

Nilikuomba siku nyingi unipatie sales agreement hujaweka hadi leo.

Mdondoaji,

..kama unayo mikataba aliyoingia Sultani na watu wa Pwani naomba utuletee.

..tulichotofautiana kati yangu mimi na wewe ni tafsiri ya mkataba kati ya Sultani na Wajerumani.

..kwasababu Sultani alipokea kiasi fulani cha pesa mimi nilielewa kwamba pwani ya Tanganyika iliuzwa kwa Wajerumani. wewe ulielewa vingine and we discussion was stalled.

..mimi nadhani mjadala huu ungekuwa mzuri kama mkataba kati ya Sultani na Muingereza unaohusu Mombasa ungepatikana.

..sasa hawa jamaa wa Mombasa wanataka kurudi kuwa chini ya mamlaka iliyoko Zanzibar?
 
umenirudisha mbali sana na hii ramani, thanx!
Mkuu, ukifuatilia historia vizuri inasema mwambao wa africa mashariki wote ulikuwa uko chini ya Zanzibar hadi 1950.
Mombasa,Lamu,Mafia,Kilwa, Bagamoyo zote hizo ilikuwa ni sehemu ya Zanzibar. Wakati huo Zanzibar haikuwa sehemu ya Tanzania. Hakukuwa na Tanzania bali Tanganyika:clap2:ndipo wazungu wakaja kuleta ushenzi wao na kuliuwa Taifa la Waswahili!!!!
Wee fikiria kwanini hiyo serikali ya wakikuyu Kenya inawabagua wamombasa, ni kwasababu&#65279; wanajua kwamba hawo ni waswahili halisi, kwa mila, desturi, dini lugha hata utamaduni wao ni sawa na Wazanzibari.
Map_Swahili_400.gif
images
 
hao wamombasa zanzibar yao ya wapi, hata wanaijua hiyo zenji, ni mababu wa bubu zao ndo wanaijua zenji wao ni 'wavivu tu flani wanaotaka kukaa wakila harua!
 
Kueni macho hapa wana Jf, ni historia ipi muhimu kwetu? Kuna watu wanaleta mada hizi ili kutugawa ili wapate upenyo wa kurudi tena kutawala. Historia iliyopita na ya sasa zote ni historia tu na kila moja kwa wakati wake hakuna inayozidi nyingine. Ya zamani ni kwa watu wa zamani katika mazingira waliyokuwemo. Hawo waliokuwapo katika historia hiyo ya zamani nao walikuwa na historia yao ya zamani tofauti historia ya zamani inayozungumuzwa leo. Ardhi inaweza kuwa ile ile lakini watu wanabadilika kizazi hadi kizazi kwa sababu ya wenyeji kuzaa na makabira na mataifa mengine. Sisi tunaozungumza hapa inawezekana hatutokani na kizazi halisi cha watu wa enzi hizo na vipi mtu leo uturudishe huko ambapo yeye mwenyewe hana uhalisia wa kizazi cha wakati huo? Kila historia hufaa kwa wakati wake na kama ni mabadiriko yaje kukidhi mahitaji ya sasa kwa hoja lakini si kwa kutumia kigezo cha historia ya zamani pekee.
 
Back
Top Bottom