Habarini wana JamiiForums
Leo ndio nimejua mjini shule. Asubuh majira ya saa 5 hivi nilikuwa nimepanda basi la G/MBOTO-KIVUKONI nikitokea G/MBOTO. Nilibahatika kupata siti kipindi safari inaendelea, ghafla akapanda mama mmoja hivi kabeba mtoto.
Mara ya kwanza nilitake easy nikijua kuna mtu atampisha, eeh maajabu watu wamekausha utasema hawajamuona vile. Na katika viti idadi kubwa ilikuwa ni akina mama na wadada baadhi, wanaume walikuwa wachache lakini wapi, wale wanawake wakaupiga kimya basi linaenda kasi huku linatikisika mama mkono mmoja kamshika mtoto mkono wa pili kashika bomba. Watu wamekausha, uzalendo ukanishinda ikabidi niinuke nimpishe, ikabidi nisimame safari nzima.
Sasa basi halijafika mbali kaingia mmama tena kabeba mtoto, watu wamekausha. Huyu hakupata kiti ata cha huruma mpaka tulipofika M/MMOJA kuna mtu akashuka ndio akapata nafasi.
Sasa kimbembe kikaja tena jioni kipindi narudi, kuna mmama kapanda basi na mtoto watu wamekausha mpaka nikaanza kusikitika sasa kipindi navuta gia kusimama nimpishe ndio ghafla yeye akamuomba mdada mmoja amshikie mtoto. Kwa bahati nzuri yule dada akaamua kumpisha kabisa.
WATU WA DAR MNAKWAMA WAPI?
Leo ndio nimejua mjini shule. Asubuh majira ya saa 5 hivi nilikuwa nimepanda basi la G/MBOTO-KIVUKONI nikitokea G/MBOTO. Nilibahatika kupata siti kipindi safari inaendelea, ghafla akapanda mama mmoja hivi kabeba mtoto.
Mara ya kwanza nilitake easy nikijua kuna mtu atampisha, eeh maajabu watu wamekausha utasema hawajamuona vile. Na katika viti idadi kubwa ilikuwa ni akina mama na wadada baadhi, wanaume walikuwa wachache lakini wapi, wale wanawake wakaupiga kimya basi linaenda kasi huku linatikisika mama mkono mmoja kamshika mtoto mkono wa pili kashika bomba. Watu wamekausha, uzalendo ukanishinda ikabidi niinuke nimpishe, ikabidi nisimame safari nzima.
Sasa basi halijafika mbali kaingia mmama tena kabeba mtoto, watu wamekausha. Huyu hakupata kiti ata cha huruma mpaka tulipofika M/MMOJA kuna mtu akashuka ndio akapata nafasi.
Sasa kimbembe kikaja tena jioni kipindi narudi, kuna mmama kapanda basi na mtoto watu wamekausha mpaka nikaanza kusikitika sasa kipindi navuta gia kusimama nimpishe ndio ghafla yeye akamuomba mdada mmoja amshikie mtoto. Kwa bahati nzuri yule dada akaamua kumpisha kabisa.
WATU WA DAR MNAKWAMA WAPI?