Watu Muhimu katika Historia ya Nchi yetu

Hii Maneno?? alisalitiwaje? ebu tupe Habari yake imekaaje?
Kumbuka miaka ile bingwa huyu wa utabiri alifanya kazi zake sana nchini Kenya na nchi nyengine kadhaa za kusini mwa Afrika. Akiwa maeneo yote hayo alihakikisha kuwa Polisi wa siri wa Nyerere(mashushushu) walipata taarifa zote wanazozitaka na huyu Mwijage (Jamaa wa Kihaya kule Bukoba sijuwi yupo wapi siku hizi aliishi uhamishoni siku nyingi) alikumbana naye nchini Swaziland alipokuwa anamkimbia Nyerere na wauwaji wake, Bingwa wa utabiri huyu akajifanya kumsaidia na yaliyofuata hapo, ni kuishi kizuizini mwaka mmoja na ushee bila ya kufunguliwa mashitaka na mateso juu ya mateso.
 
halafu inaelekea kweli hatufikiri. Nyie huyu nyerere kasoma lini? Halafu nyie mmemvika hiyo suruali au sijui, nani wa kuvikwa suruali? Nyerere kasoma kabla hata hamjaanza kudai uhuru; au kwa sababu kafa ndiyo mnaanza uongo? Wakati ule elimu yake tu ilibidi kuwa yeye awe kafunguka zaidi ya hao mnaowasema. Hivi hao wazee wote na ile population ya dar wkati ule ilmshindwa mtu mmjoa aitwaye nyerere? La, huyu jamaa alikuwa intelligent kuwazidi wengi wakati huo, na mie naamini kwa wakati ule wengi walimwona wa maana.

Unajua tena always kuna wale big fish wanaotaka kuwa big fish kwenye "small pond" ndiyo wanajitokeza sasa kuongea hayo! At that time nyerere was a big fish in a big pond na akaendelea hadi kafariki.

Historia hapo ishakwisha, mngesimama wakati anaishi mie ningewaona ni big fish! Tena mapapa au nyangumi!!
nyerere aliambiwa mchana kweupe na akakabidhiwa kitabu cha maelekezo haya akiwa hai.akabaki kimya katoa macho.
Soma kitabu cha untold history of the muslims in tanzania. Au life and times of abdulwahid sykes.
Na wapo watu walimkabili nyerere kumueleza haya. Tutamoumba michuzi atuwekee picha za nyerere na kikaputula.
 
Historia nzuri ni inayotusadia kuona mbele na si ile inayoturudisha nyuma. Nina maana ingawa si kosa lakini haitusaidii sana kuzama kwenye historia za miaka 40 iliyopita.

Kwa maendeleo ya nchi na ili tujue tunakokwenda tungalie historia ya miaka kumi au kumi na tano iliyopita.hapo ndo tutajua tuna wana historia gani na wa mazuri na mabaya gani ambayo tunaweza kujifunza mengi.

Ukweli ni kuwa kuna watu wengi wamechangia historia ya nchi ila hawajulikani sababu hawakuwa wanasiasa.

Karen hii sio ya kuzama sana kwenye historia ambazo zinamtazamo wa kiukombozi, kiuhuru. karne hii tunahitaji historia za kisayansi na teknolojia.

Historia nzuri ni zile zitakazo saidi kuleta maendeleo na si malumbano nani alikomboa nchi. ncho ihskombolewa kilichobaki ni maendeleo.

Historia nzuri na mbaya ni kama iliyoandikwa na Edward Lowasa kwa kujiuzulu uwaziri mkuu . Historia nzuri iliyonadikwa ni kama ya Asha Rose migiro na mama Tibaijuka kuchaguliw anafasi za juu kwenye umoja wa mataifa. kuna historia kama za wanamichezo kina ikangaa na kiasi fulani matumla family.nk ziko historia za watu au familia zinazoweza kutuweka kwenye track ya kuwa taifa na wanachi wenye vision.


Historia kama hizi zikitumika mashuleni kujua wahusika walipataje au walihusika vipi kwenye matukio fulani. Au waliweza vii kupanda na kushuka kwenye nafasi mbali mbali za kiuongozi na walifanya nini.

sio kwamba napuuza michango ya mashujaa na wanaharakati mbali mbali . ila haisadii sababu miaka 40 baada ya uhuru tumeimba hizi hitoria na hazijatusaidia. tubadilishe mtazamo wa historia gani tuzimulike zaidi ya zile za kisiasa.
 
Ndugu wanamtandao,

Huu mjadala unaweza ukawa mzuri sana endapo wanaukumbi watatuliza vichwa na kutoa michango ya kiistarabu.

Mchango wangu mimi katika mjadala huu nawaomba wanaukumbi waingie "Index Kenya Project Gamble and the birth of a new nation" - Gonga Google itakupa khabari za watu muhimu katika historia ya kudai uhuru wa nchi yetu.

Lugha za masimango za kuvaa kaptula nk. si uungwana na wala kaptula halikuwa vazi dhalili kwa wakati ule. Lilikuwa vazi la Waingereza na wasomi wa enzi hizo pamoja na kaptula au suruali kipande wakivaa na stocking.

Tutulie ndugu zangu tujadiliane tusibughudhiana wala kutukanana ili tupate faida. Msomi mmoja alipata kusema maneno haya: Mie naweza kupambana na hata watu mia kwa hoja lakini mjinga mmoja tu akanishinda."

Mohamed Said

Hapa
 
Ndugu wanamtandao,

Huu mjadala unaweza ukawa mzuri sana endapo wanaukumbi watatuliza vichwa na kutoa michango ya kiistarabu.

Mchango wangu mimi katika mjadala huu nawaomba wanaukumbi waingie "Index Kenya Project Gamble and the birth of a new nation" - Gonga Google itakupa khabari za watu muhimu katika historia ya kudai uhuru wa nchi yetu.

Lugha za masimango za kuvaa kaptula nk. si uungwana na wala kaptula halikuwa vazi dhalili kwa wakati ule. Lilikuwa vazi la Waingereza na wasomi wa enzi hizo pamoja na kaptula au suruali kipande wakivaa na stocking.

Tutulie ndugu zangu tujadiliane tusibughudhiana wala kutukanana ili tupate faida. Msomi mmoja alipata kusema maneno haya: Mie naweza kupambana na hata watu mia kwa hoja lakini mjinga mmoja tu akanishinda."

Mohamed Said

Hapa

Karibu sana Mohammed Said !
 
nitapenda kuwakumbuka Machifu 9 wa iliyokuwa Pare Native Authority. pamoja na kwamba napinga Uchifu, lakini nitaeleza kwanini ninawaenzi Machifu hawa pamoja na mapungufu waliyokuwa nayo.

baada ya vita kuu ya pili Muingereza aliweka lengo kwa koloni la Tanganyika kuandikisha 36% ya watoto shule ya msingi. Tanga Province ambako wilaya ya Pare waliweka lengo kwamba mpaka kufikia mwaka 1956 wawe wamefikia 50%. Machifu wa Pare Native Authority waliweza kuhamasisha wananchi wao na ilipofika 1952 waliweza kuandikisha 90% ya watoto shule ya msingi.

pia vipo VIKUNDI VYA ELIMU YA WATU WAZIMA katika maeneo mbalimbali kama Usangi, Mbaga, Same, Ugweno. wakinamama hawakuwa nyuma katika kuanzisha vikundi vya kujifunza kusoma. mwamko huo wa kinamama kujifunza kusoma ktk utu uzima ndiyo uliochochea elimu ya mtoto wa kike katika maeneo hayo. historia inapaswa kuwakumbuka kinamama hao.

kampeni ya elimu ya watu wazima ilipelekea kuanzishwa kwa GAZETI lilloitwa HABARI ZA UPARE. gazeti lilianzishwa 1951 na kuna kipindi lilikuwa likitoa makala 2000 kwa mwezi. nitatafuta makala ya gazeti hilo na kuwawekea mlisome.

shule nyingi za msingi haswa zile za WALUTHERI, SDA, na WAISLAMU, na hata SERIKALI, zilijengwa kwa mwamko wa kujitolea wa wananchi wenyewe. wananchi wa maeneo kama Usangi na Ugweno kwa miaka karibu 14 bila msaada wa fedha au utaalamu walishiriki ujenzi wa barabara za milimani kuwaunganisha na mji wa Mwanga. wananchi wa Chome, Mamba,Vudee, nao hawakuachwa nyuma katika ujenzi wa barabara kwa njia ya kujitegemea.

Machifu au Wafumwa 9 ninaowakumbuka ni Chifu/Mfumwa Sabuni wa Usangi, Mfumwa Kibacha Singo wa Same, Mfumwa Manento Sekimanga wa Mamba, Joseph Mamphombe wa Mbaga, Kigono Chuma wa Gonja, Folong'o Makange wa Chome, Minja Kukome wa Ugweno, Yoeli Mtindi wa Hedaru.
 
Ndugu wanamtandao,

Huu mjadala unaweza ukawa mzuri sana endapo wanaukumbi watatuliza vichwa na kutoa michango ya kiistarabu.

Mchango wangu mimi katika mjadala huu nawaomba wanaukumbi waingie "Index Kenya Project Gamble and the birth of a new nation" - Gonga Google itakupa khabari za watu muhimu katika historia ya kudai uhuru wa nchi yetu.

Lugha za masimango za kuvaa kaptula nk. si uungwana na wala kaptula halikuwa vazi dhalili kwa wakati ule. Lilikuwa vazi la Waingereza na wasomi wa enzi hizo pamoja na kaptula au suruali kipande wakivaa na stocking.

Tutulie ndugu zangu tujadiliane tusibughudhiana wala kutukanana ili tupate faida. Msomi mmoja alipata kusema maneno haya: Mie naweza kupambana na hata watu mia kwa hoja lakini mjinga mmoja tu akanishinda."

Mohamed Said

Hapa

Karibu Bingwa ulikuwa wapi siku zote? lakini mie sikubaliani nawe, Nyerere katuvalisha kaptula wanafunzi hadi alipokuja mzee Mwinyi ndio suruali zikaruhusiwa mashuleni.

naomba unipe picha ya wasomi wazungu au wanasiasa wa ulaya waliokuwa wakivaa kaptula?jee ni CHURCHILL?AU TONY BLAIR?
TENA INGEKUWA VYEMA KAMA MWALIMU MIGUU YAKE INGEKUWA IMEJAZIA.ILIKUWA KAMA KICHEKESHO KWA FITO ZAKE KUVAA KAPTULA.
 
Mkandara,
Umeleta mada ngumu kweli ambayo kama wadau watakubaliana na ukweli itasaidia kufumbua macho watu wengi, kuna watu hata wasomi ukiwauliza kwanini kuna wodi ya kibasila au sewa haji pale Muhimbili hawezi kukwambia, au watu kama Selemani Mamba, Nkosi Chabruma Tawete wa Gumbiro na mashujaa chungu nzima waliomwaga damu na jasho lao ili mm na ww tuwe watu huru leo, hawatajwi kabisaaa.
Hili ni tatizo la nchi kuwa katika utawala wa kikandamizaji kwa muda mrefu. Honestly blame it to Baba wa taifa ambaye alijali umaarufu wake tu wengine a a a!!!

Nia ya Mhe. Mkandara ni njema kabisa lakini ndugu yetu Junius naona umeenda nje ya mstari. Unamlaumu Baba wa Taifa eti alijali umaarufu wake tu wengine aaa! You are being very unfair to him! Did you expect him kusimama jukwaani na kutoa orodha ya wale alioshirikiana nao katika kupigania Uhuru? Ama ulitaka pamoja na makujumu mazito ya kuliongoza taifa basi aketi chini awaandikie historia. Kazi hiyo ni yenu wasomi na hata wale wasio wasomi kuandika historia ya nchi hii kwa kuwafuata wanasiasa na wananchi ambao bado wako hai wanaojua kilichotokea miaka hiyo. Hata hivyo Mwalimu did justice to his fellow wapiganaji kwa sababu amewahi mara kadhaa kuwataja watu kama akina Mzee Tambaza, Sykes, Rupia na wengine wengi tu katika hotuba zake wakati akisimulia juu ya harakati za kupigania Uhuru. And for your information baada ya kustaafu wapo Watanzania waliokuwa wakionana naye na na kupata simulizi na mengi yaliyotokea katika historia ya nchi hii. I assure you, he wasn't all that mean kama unavyotaka kutuaminisha Junius!

Kwa uzoefu wangu, naona wengi wanaomkandia Mwalimu na kumshutumu kwa namna moja ama nyingine ni wale ambao kama si wao basi 'ancestors' wao waliguswa na 'fimbo' ya Mwalimu katika mambo kadha wa kadha.
 
nitapenda kuwakumbuka Machifu 9 wa iliyokuwa Pare Native Authority. pamoja na kwamba napinga Uchifu, lakini nitaeleza kwanini ninawaenzi Machifu hawa pamoja na mapungufu waliyokuwa nayo.

baada ya vita kuu ya pili Muingereza aliweka lengo kwa koloni la Tanganyika kuandikisha 36% ya watoto shule ya msingi. Tanga Province ambako wilaya ya Pare waliweka lengo kwamba mpaka kufikia mwaka 1956 wawe wamefikia 50%. Machifu wa Pare Native Authority waliweza kuhamasisha wananchi wao na ilipofika 1952 waliweza kuandikisha 90% ya watoto shule ya msingi.

pia vipo VIKUNDI VYA ELIMU YA WATU WAZIMA katika maeneo mbalimbali kama Usangi, Mbaga, Same, Ugweno. wakinamama hawakuwa nyuma katika kuanzisha vikundi vya kujifunza kusoma. mwamko huo wa kinamama kujifunza kusoma ktk utu uzima ndiyo uliochochea elimu ya mtoto wa kike katika maeneo hayo. historia inapaswa kuwakumbuka kinamama hao.

kampeni ya elimu ya watu wazima ilipelekea kuanzishwa kwa GAZETI lilloitwa HABARI ZA UPARE. gazeti lilianzishwa 1951 na kuna kipindi lilikuwa likitoa makala 2000 kwa mwezi. nitatafuta makala ya gazeti hilo na kuwawekea mlisome.

shule nyingi za msingi haswa zile za WALUTHERI, SDA, na WAISLAMU, na hata SERIKALI, zilijengwa kwa mwamko wa kujitolea wa wananchi wenyewe. wananchi wa maeneo kama Usangi na Ugweno kwa miaka karibu 14 bila msaada wa fedha au utaalamu walishiriki ujenzi wa barabara za milimani kuwaunganisha na mji wa Mwanga. wananchi wa Chome, Mamba,Vudee, nao hawakuachwa nyuma katika ujenzi wa barabara kwa njia ya kujitegemea.

Machifu au Wafumwa 9 ninaowakumbuka ni Chifu/Mfumwa Sabuni wa Usangi, Mfumwa Kibacha Singo wa Same, Mfumwa Manento Sekimanga wa Mamba, Joseph Mamphombe wa Mbaga, Kigono Chuma wa Gonja, Folong'o Makange wa Chome, Minja Kukome wa Ugweno, Yoeli Mtindi wa Hedaru.
Muongo mkubwa,wapare aliyewasaidia ni Cleopa Msuya kama uchifu apewe msuya.ni kabila dhariri sana mbele ya wachagga,kutokana na manyanyaso hayo ndio Msuya akawasukuma kimaendeleo.labda history hii umetunga wewe.
 
hivi watu wengine mnavyo andika kitu mnakuwa mmekunywa au kuvuta au ndio hivyo tena kuandika ili uonekane umeandika. kama unajua historia tanu ilianzishwa na kuasisiwa nyerere akiwa tayari katika harakati za kuleta uhuru, sasa hiyo ya kusema ilikuwepo tokea akiwa ana nyonya si ni kujidanganya wewe mwenyewe? au ndio huko kutokujua historia go back to you history books uone tanu ilianzishwa lini. au ndio hivyo shule less halafu unataka kupewa uongozi, na ukishindwa unasema una hujumiwa.
Mkuu kwa heshima kubwa na taadhima kweli darasa langu mwisho la saba mie, ww uliefika chuo kikuu na p.h.d yako umeshindwa kabisa kutofautisha maneno rahisi ya kiswahili ya "kuasisiwa" na "kuanzishwa".
Mkuu mm sikusema kama Nyerere hakushiriki kuanzisha TANU,sharti tuelewane hapa,nilichosema na kumaanisha ni kuwa hakuwa muasisi wa TANU. Kwa mujibu wa historia yangu ya darasa la saba(ww wa chuo kikuu unaweza kunirekebisha) ni kuwa asili ya chama cha TANU ni TAA(Tanganyika Africans Association) kilichoasisiwa mwaka 1929,wakati huu Nyerere ni Mtoto wa miaka 8 tu(alizaliwa April 13,1922)ataasisi kitu gani hapa??,TAA ilihamisha malengo yake kutoka kudai haki za wakulima mpaka kudai mabadiliko ya kisiasa mwaka 1948, wakati huo Nyerere ni kijana mwanafunzi anajitayarisha kwenda masomoni Endinburg, Scotland, kuanzia hapo TAA iliendeleza harakati zake za kudai uhuru wa Tanganyika wakati Nyerere yupo Ulaya bado, aliporudi mwaka 1953, alikuta tayari TAA ni chama kikubwa tu cha siasa na kila mtu anaimba uhuru, kumbuka kipindi hiki Watanganyika walichagizwa na harakati za Mau Mau kule Kenya, Nyerere alipojiunga na TAA mwaka 1954(ilikuwa strategic move for TAA) alichaguliwa kuwa rais wake na akashiriki kubadili muundo wake kuelekea TANU, hii ndo asili ya TANU ambayo Nyerere hakuhusika kuiasisi bali kuiendeleza tu.
 
Mkuu kwa heshima kubwa na taadhima kweli darasa langu mwisho la saba mie, ww uliefika chuo kikuu na p.h.d yako umeshindwa kabisa kutofautisha maneno rahisi ya kiswahili ya "kuasisiwa" na "kuanzishwa".
Mkuu mm sikusema kama Nyerere hakushiriki kuanzisha TANU,sharti tuelewane hapa,nilichosema na kumaanisha ni kuwa hakuwa muasisi wa TANU. Kwa mujibu wa historia yangu ya darasa la saba(ww wa chuo kikuu unaweza kunirekebisha) ni kuwa asili ya chama cha TANU ni TAA(Tanganyika Africans Association) kilichoasisiwa mwaka 1929,wakati huu Nyerere ni Mtoto wa miaka 8 tu(alizaliwa April 13,1922)ataasisi kitu gani hapa??,TAA ilihamisha malengo yake kutoka kudai haki za wakulima mpaka kudai mabadiliko ya kisiasa mwaka 1948, wakati huo Nyerere ni kijana mwanafunzi anajitayarisha kwenda masomoni Endinburg, Scotland, kuanzia hapo TAA iliendeleza harakati zake za kudai uhuru wa Tanganyika wakati Nyerere yupo Ulaya bado, aliporudi mwaka 1953, alikuta tayari TAA ni chama kikubwa tu cha siasa na kila mtu anaimba uhuru, kumbuka kipindi hiki Watanganyika walichagizwa na harakati za Mau Mau kule Kenya, Nyerere alipojiunga na TAA mwaka 1954(ilikuwa strategic move for TAA) alichaguliwa kuwa rais wake na akashiriki kubadili muundo wake kuelekea TANU, hii ndo asili ya TANU ambayo Nyerere hakuhusika kuiasisi bali kuiendeleza tu.
SWADAKTA HUKU ndiko KUMKOMA NYANI GRADI.
 
Kwa uzoefu wangu, naona wengi wanaomkandia Mwalimu na kumshutumu kwa namna moja ama nyingine ni wale ambao kama si wao basi 'ancestors' wao waliguswa na 'fimbo' ya Mwalimu katika mambo kadha wa kadha.
Mada ni "watu muhimu katika historia yetu", masuala yamekuja juu ya kusahaulika umuhimu wao licha ya kuwa wengine wanatajwa tajwa. Nilichosema kuna mambo kadhaa yametajwa wachangiaji wengine yaliyopelekea kusahaulika kwao, mm nilitaja moja tu kati ya mambo hayo kuwa ni utawala wa kikandamizaji wa Mwalimu Nyerere, au unakataa kuwa Mwalimu hakuwa dikteta au autocratic ruler at the same time?
Kuhusu kumshutumu na kumkandia Mwalimu, mimi sipo huko kabisa, najua anamchango wake katika maendeleo ya taifa hili na kudumaa kwake vilevile. Hiyo unayoita "fimbo" ya Mwalimu, kweli imenigusa, mpaka leo najuwa Nyerere aliishi na baadae akafa, kaburi lake nalijuwa lilipo(Butiama), Lakini kwa "fimbo" yake hiyo, mm mpaka leo sijuwi kaburi la wazee wangu lipo wapi, ambao mara ya mwisho walikuwa pamoja naye(Nyerere) na yeye anawajuwa walipopotelea.
 
Nia ya Mhe. Mkandara ni njema kabisa lakini ndugu yetu Junius naona umeenda nje ya mstari. Unamlaumu Baba wa Taifa eti alijali umaarufu wake tu wengine aaa! You are being very unfair to him! Did you expect him kusimama jukwaani na kutoa orodha ya wale alioshirikiana nao katika kupigania Uhuru? Ama ulitaka pamoja na makujumu mazito ya kuliongoza taifa basi aketi chini awaandikie historia. Kazi hiyo ni yenu wasomi na hata wale wasio wasomi kuandika historia ya nchi hii kwa kuwafuata wanasiasa na wananchi ambao bado wako hai wanaojua kilichotokea miaka hiyo. Hata hivyo Mwalimu did justice to his fellow wapiganaji kwa sababu amewahi mara kadhaa kuwataja watu kama akina Mzee Tambaza, Sykes, Rupia na wengine wengi tu katika hotuba zake wakati akisimulia juu ya harakati za kupigania Uhuru. And for your information baada ya kustaafu wapo Watanzania waliokuwa wakionana naye na na kupata simulizi na mengi yaliyotokea katika historia ya nchi hii. I assure you, he wasn't all that mean kama unavyotaka kutuaminisha Junius!

Kwa uzoefu wangu, naona wengi wanaomkandia Mwalimu na kumshutumu kwa namna moja ama nyingine ni wale ambao kama si wao basi 'ancestors' wao waliguswa na 'fimbo' ya Mwalimu katika mambo kadha wa kadha.

Mama Ntilie:

Huu uzoefu wako hauko ukamili. Wakati TAA inabadilika na kuwa TANU 1954, wimbi la kudai uhuru tayari lilikuwepo barani Africa. Na haitawezekana kwa watanzania kuanza kudai uhuru mwaka 1954, hii itakuwa ni kutotendea haki struggle za wananchi zilizokuwepo kabla.

Phenomena unayoiona hapa, imetokea karibu katika nchi zote za kiafrika. Wananchi walianzisha vyama, lakini baadaye waliwapa nafasi vijana waliotoka masomoni Ulaya.

Kwa mfano Kwame Nkrumah alikuwa yupo uingereza hana mpango wowote. Lakini kwa sababu alikuwa amesoma watu walimrudisha Ghana na kumpa madaraka.

Kamuzu Banda, Jomo Kenyatta na wengine wengi tu walikuta watu wameweka misingi mizuri ya vyama vya kudai uhuru. Na hawa ndio walioandikwa kwenye historia.
 
kanda2 said:
Muongo mkubwa,wapare aliyewasaidia ni Cleopa Msuya kama uchifu apewe msuya.ni kabila dhariri sana mbele ya wachagga,kutokana na manyanyaso hayo ndio Msuya akawasukuma kimaendeleo.labda history hii umetunga wewe.

kanda2,
Wachaga,Wazigua,na Wasambaa, walitunyanyasa sana Wapare kabla hatujawa na mfumo madhubuti wa utawala. kwa asili Wapare walikuwa vikundi vidogo vidogo vya wahamiaji toka maeneo ya Utaita, na Ukamba. baadaye wamekuja kuchanganyika na Wachaga,Wazigua,Wasambaa, Wagweno,Wambugu etc etc. usishangae leo ukisikia kuna Minja Wachaga na wengine Wapare. pia wako kina Tenga Wachanga wengine Wapare. Kilonzo wanapatikana Ukambani na Upareni. Mwanzia wako Utaita na Upareni. kwa hiyo ni kweli kabisa katika kuhama hama kwetu tulikuwa dhalili sana mbele ya Wachaga waliokuwa wakipora mali zetu, na Wasambaa na Wazigua waliokuwa wakituuza utumwani. pia tuliwahi kutawaliwa na maakida wa Kizigua na Kisambaa waliosimikwa na Wajerumani.

CHAANGAJA Cleopa David MSUYA asili yake ni North Pare. sasa huko uchifu wao ni ulikuwa kwenye koo za Wasangi na Wambaga. kuna historia ya vita kati ya clan hizo mbili, lakini Mfumwa wa maarufu wa mwisho wa North Pare alikuwa Mfumwa Sabuni ambaye ni Mmbaga ambao kwa asili walihamia toka South Pare.

Msuya ameendeleza pale walipoachia wale waliomtangulia kama hao Machifu niliowataja, na marehemu Chediel Mgonja "kaghembe" ambaye ni mbunge wa kwanza wa wilaya ya Pare baada ya uhuru. barabara za Ugweno na Usangi kuunganisha na mji wa Mwanga zilijengwa kwa nguvu ya wananchi kuanzia kuanzia 1922 mpaka 1936. wakati huo Chaangaja Cleopa Msuya alikuwa ama hajazaliwa au ni mtoto mdogo.

napenda kukueleza kuwa wazee wetu walikuwa na makini sana katika shughuli za kujitolea MSARAGAMBO. waliweza kutunga sheria na faini za kuwadhibiti watega kazi na watoro.

kanda2, siyo kosa lako kwamba historia ya Upare unaoijua wewe inaanzia na Cleopa Msuya. pia inajumuisha wakati wilaya zetu zikiwa ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. wilaya ya Pare, sasa Mwanga na Same, miaka ya michache kabla na baada ya uhuru ilikuwa chini ya jimbo la Tanga. kabla ya hapo kulikuwa na North Pare iliyokuwa chini ya North Province na South Pare iliyokuwa chini ya Tanga Province.

harakati zetu za kujiamulia mambo yetu wenyewe zilianza na mashujaa kama Mavura wa Mbaga aliyebigana na Wazigua na Wasambaa waliokuwa wakituteka utumwa. inaendelea mpaka karibu na Uhuru ambapo wanachama wa WAPARE ASSOCIATION waliunganisha nguvu zao na TAA na TANU. viongozi wa Wapare Association kama MANASE KANIKI, SAMUEL MSHOTE na ELIAS KISENGE walikuwa mstari wa mbele kuhamasisha kwa niaba ya TANU katika maeneo ya Upare na Tanga Province.

Elias Kisenge alikuwa Executive Secretary wa Pare Council, katibu wa Tanu na Wapare Association. baadaye alipanda ngazi na kuwa Katibu wa Tanu jimbo la Tanga, kabla hajahamishiwa makao makuu ya Tanu kuwa Katibu Mwenezi.

pia kuna kipindi Wapare walitaka kuanzishwa mfumo kama wa Wachaga wa kuwa na Paramount Chief. Elias Kisenge alikuwa kati wa wananchi waliofikiriwa kuchukua nafasi hiyo.
 
Ebwana huyu ni MOhamed Said Mwenyewe au zuga?

ama mohammed said mwenyewe basi nashauri wana ukumbi aeni mkao wa kula na mtakula mpaka hapo Mods na Admin watakapo boa na kuhamisha thread

Otherwse watu wakituliza vichwa basi mjue kuwa mtakula historia na mtaona watu mbali mbali wanarudi tar-tiiiibu
 
Waliopigania uhuru ni Waswahili bwana,kwa maana ya wasilamu na wakristo maskini.Mwazna alikuwapo Huseni Majaliwa,Bukoba alkuwapo Ali Migeyo,Kahama Ali Saidi Maswanya,Paulo Bomani,Mwananyolo na Gerevas waliokubali mseto na kuitwa wapumbavu.Lakini wale waliokuwa wamejikita katika Misheni na kuwa karibu sana na wakoloni walikuja kurukia tu kama Lyanyantika Masha na wengineo walikuja kupewa kazi na nyerere.
Kule darisalam ambako ndiko kulikuwako na vuguvugu kubwa ni wale wazee wa kipwani walikuwa wanampelekesha mkoloni.Nyererr yeye alilpelewka na kapputula yake na kasela bantu hadi kwa kina sykes na kutambulishwa huko.
 
Wanasiasa wa JF . Nashukuru kwa haya majadiliano. Nina maswali mawili naomba mnisaidie kuyajibu.

Kwanza ni nini mchango wa Wolfgang Dourado? ( Kama alikuwa na mchango wowote)

Pili, kunako miaka ya mwanzoni ya sitini, kama 1963 au 64 kulikuwa na chama fulani cha wafanya kazi kikiitwa TUPA au labda TUPE. wanachama wake walikamatwa wakahojia halafu wakaachiliwa, nina uhakika wa wanachama wa wilayani Mpwapwa, walikamatwa wakapelekwa Dodoma nadhani kuhojiwa halafu wakaachiliwa. Nataka kujua kama hiki chama kilikuwa Mpwapwa tu? Je kuna Watanzania wengine wenye habari na hiki chama? Je ni chama cha wafanyakazi kilichokatishwa tamaa kwa njia moja au nyingine au vipi? Mtu wa karibu na mimi aliyehusika ameisha kufa ningeweza kumuuliza yeye.
 
Karibu Bingwa ulikuwa wapi siku zote? lakini mie sikubaliani nawe, Nyerere katuvalisha kaptula wanafunzi hadi alipokuja mzee Mwinyi ndio suruali zikaruhusiwa mashuleni.

naomba unipe picha ya wasomi wazungu au wanasiasa wa ulaya waliokuwa wakivaa kaptula?jee ni CHURCHILL?AU TONY BLAIR?
TENA INGEKUWA VYEMA KAMA MWALIMU MIGUU YAKE INGEKUWA IMEJAZIA.ILIKUWA KAMA KICHEKESHO KWA FITO ZAKE KUVAA KAPTULA.
Kanda2,
Acha uwongo ndugu yangu. Mimi nilisoma Aga Khan, siku hizi inaitwa Tambaza. Tulivaa suruali za kijivu na shati nyeupe kama uniform zetu. Uwongo mbaya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom