Kididimo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 3,791
- 3,360
Ni wazi kuwa vitendo vya viongozi hawa dhidi ya raia vilikuwa ni vya kidhalimu sana. Nchi ilitikisika na kupata doa la Kimataifa hata baadhi ya misaada ikasitishwa!
Ili Serikali ionekane haikuwatuma,kuwepo na mahakama huru na ya wazi. Kama ambavyo serikali ya Marekani ilijivua kidunia kuwa haijatuma Askari wake kuua mtu mweusi.
Wananchi wanajiuliza iweje uteue mtu, umsimamie wewe, pia useme ni mchapakazi Bora, ghafla ubadilike tena kwa kushinikizwa kuwa huyo ni jambazi? Vyombo vyote vya dola vilikuwa wapi?
Hakika hii kesi ya huyu jamaa itauweka uongozi wa juu kwenye mtihani mkubwa. Wananchi wanataka uwazi.
Ili Serikali ionekane haikuwatuma,kuwepo na mahakama huru na ya wazi. Kama ambavyo serikali ya Marekani ilijivua kidunia kuwa haijatuma Askari wake kuua mtu mweusi.
Wananchi wanajiuliza iweje uteue mtu, umsimamie wewe, pia useme ni mchapakazi Bora, ghafla ubadilike tena kwa kushinikizwa kuwa huyo ni jambazi? Vyombo vyote vya dola vilikuwa wapi?
Hakika hii kesi ya huyu jamaa itauweka uongozi wa juu kwenye mtihani mkubwa. Wananchi wanataka uwazi.