Watu kadhaa wahofiwa kufa baada ya kugongana kwa helikopta za kijeshi

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Oct 26, 2018
21,713
35,524
Watu kadhaa wanahofiwa kufa baada ya helikopta ya Jeshi la Marekani kuanguka katika Kaunti ya Trigg, Kentucky. Gavana wa jimbo hilo Andy Beshear alisema ni "habari mbay" na "ripoti za mapema za ajali ya helikopta na vifo vinatarajiwa". Habari za ndani zinasema kuwa tukio hilo lilitokea mwendo wa saa 21:35 saa za huko (01:35 GMT), na huenda watu tisa wamepoteza maisha.

Wanajeshi wa eneo hilo walithibitisha kuwa ni helikopta zao zilizohusika katika ajali hiyo.

Katika taarifa kwa BBC, msemaji wa kambi ya kijeshi ya Fort Campbell alisema helikopta mbili za HH60 Blackhawk zilianguka wakati wa "misheni ya kawaida ya mafunzo". "Hali za wahudumu hao hazijulikani kwa wakati huu," walisema. "Amri kwa sasa inalenga kutunza wanajeshi na familia zao."

Helikopta zinazohusika zinatoka Kitengo cha 101 cha Ndege (Air Assault). Waliongeza kuwa tukio hilo linachunguzwa na taarifa zaidi zitatolewa kadiri zitakavyopatikana.

Screenshot_20230330-133627_Facebook.jpg
 
Hapo ndo wapo ktk tizi la kwenda Ukraine dhidi ya urusi hata kwenye Hali halisi hawajafika wamebamizana hapo usikute rubani kaambiwa ajipange na dog fight vs Russian pilots akatoa jassho hadi kwenye kope mwisho ajali!
 
Back
Top Bottom