Watu hawa maarufu kumiliki kadi mbili za vyama maana yake nini?

technically

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
11,955
48,752
Ifuatayo ni wanaomiliki kadi mbili ya vyama tofauti .

1: Lowassa kadi ya Ccm na Chadema
2: Sumaye ya kadi Ccm na Chadema
3: Zitto kadi ya Chadema na ACT
4: Lyatonga kadi ya Ccm na Nccr
5: Kafulila kadi ya Nccr na Chadema
6: Lipumba kadi ya CUF na Ccm
7: Lwakatale kadi ya CUF na chadema
8: Mpendazoe kadi ya Chadema na Ccm
9: Cheyo kadi ya UDP na Ccm.

Na wengine wengi swali linakuja.

Kwanini uwa hawarudishi kadi wanapoondoka chama kimoja kwenda kingine?.

Kwanini wanabaki na kadi zao wakati wameshakimbia vyama ?.
 
mimi sijui kusema kweli

[HASHTAG]#freemaxencemelonow[/HASHTAG]

[HASHTAG]#tunamtakabensaananeakiwahai[/HASHTAG]

[HASHTAG]#freelemanow[/HASHTAG]

[HASHTAG]#MASSIVEandVIGOUROUSevaluationOfAllphDs[/HASHTAG]

be the first to reply

Am privilege

Self declared,

phD holder!
 
Naona hapo CCM zipo nyingi maana yake ni kwamba watu wana imani na CCM ila wapo upinzani kwa maslahi binafsi
Sasa kama mnayajua hayo na hao ni agent wenu, mbona wanakuteshine na nguvu nyingi kuwazuia?
 
Ifuatayo ni wanaomiliki kadi mbili ya vyama tofauti .

1: Lowassa kadi ya Ccm na Chadema
2: Sumaye ya kadi Ccm na Chadema
3: Zitto kadi ya Chadema na ACT
4: Lyatonga kadi ya Ccm na Nccr
5: Kafulila kadi ya Nccr na Chadema
6: Lipumba kadi ya CUF na Ccm
7: Lwakatale kadi ya CUF na chadema
8: Mpendazoe kadi ya Chadema na Ccm
9: Cheyo kadi ya UDP na Ccm.

Na wengine wengi swali linakuja.

Kwanini uwa hawarudishi kadi wanapohama vyama?

Kwanini wanabaki na kadi zao wakati wameshakimbia vyama ?.
bila shaka hizo takwimu zinaweza kukupa jibu kwanini CCM itatawala milele
 
Ukihama chama kadi ya awali kwa kuwa uliilipia ni yako hivyo unaweza kuichana ,kuichoma moto ama kuihifadhi ingawa hauitumii hivyo hao uliowataja na wengineo wenye kadi zaidi ya moja hakuna sheria yoyote inayowabana kwan kila mtanzania ana haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa au asijiunge. Pia hata wakirudisha hizo kadi ww utajua vipi wamerudisha? Kwan ww ndio una mpokea taarifa ya waliochukua kadi mpya na waliorudisha za vyama walivyohama
 
Unapohama chama kimoja kwenda kingine uanachama wako wa chama cha awali unakufa automatically hata kama hujarudisha kadi.
Kuwa na kadi si kigezo cha kuwa mwanachama kuna sifa nyingi za mtu kuwa mwanachama kama kulipia ada ya kila mwaka nk.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom