Watu 26 wauawa kwa kupigwa risasi kanisani Texas, Marekani

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Watu 26 wameuawa kwa kupigwa risasi na mtu mwenye silaha aliyewafyatulia risasi waumini katika kanisa moja jimbo la Texas wakati wa ibada, maafisa wanasema.

Shambulio hilo lilitekelezwa katika kanisa la First Baptist Church katika mji wa Sutherland Springs, mji mdogo katika wilaya ya Wilson, Texas.

Mshambuliaji, ambaye anadaiwa kuuawa baada ya kutekeleza mauaji hayo, aliingia kanisani na kuanza kuwafyatulia risasi watu mwendo wa saa tano unusu asubuhi (17:30 GMT).

Gavana Greg Abbott amethibitisha idadi ya waliofariki na kusema ndicho kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutekelezwa kwa kutumia bunduki katika historia ya texas.

"Kutakuwa na majonzi na masikitiko mengi kwa wale walioathiriwa," aliambia wanahabari.

Mkuu wa idara ya usalama wa Texas Freeman Martin amesema waathiriwa walikuwa na umri wa kati ya miaka 5 na 72

Maafisa wamesema watu zaidi ya 20 pia walijeruhiwa na wamelazwa hospitalini.

Bw Martin amesema mshukiwa ni mwanamume mzungu wa umri wa miaka 20 ambaye alikuwa amevalia mavazi meusi na fulana ya kujikinga dhidi ya risasi pamoja na kuwa na bunduki yenye uwezo mkubwa.

Alianza kufyatua risasi nje ya kanisa kabla ya kuingia ndani na kuendelea kufyatulia watu risasi.

Mwenyeji "litwaa bunduki yake na kuanza kumfyatulia " risasi mshukiwa kabla ya mshukiwa huyo kutoroka akitumia gari.

Raia huyo alimwandama mshukiwa huyo ambaye aliendesha gari lake na kisha kuliangusha katika barabara wilaya ya Guadalupe.

Polisi waelimpata mshukiwa akiwa amefariki ndani ya gari lake.

Haijabainika iwapo alifariki kutokana na majeraha ya risasi aliyojisababishia mwenyewe au kutokana na mejaraha kutoka kwa raia huyo, Martin ameongeza.

Mshukiwa ametajwa kuwa Devin P Kelley, 26, kwa mujibu wa vyombo vya jhabari Marekani.

Polisi bado hawajathibitisha jina lake.

Mhubiri wa kanisa hilo la First Baptist Frank Pomeroy, ameambia ABC News kwamba binti yake wa miaka 14 kwa jina Annabelle ni miongoni mwa waliouawa.

Sutherland Springs ni mtaa mdogo wenye wakazi wasiozidi elfu moja ambao hupatikana kilomita 50 hivi kusini mashariki mwa mji wa San Antonio mjini Texas.

Maafisa wa FBI kutoka San Antonio wametumwa kufanya uchunguzi lakini kufikia sasa lengo la mshambuliaji halijabainika.

FBI pia wamesema mshambuliaji alikuwa mmoja pekee, lakini bado wanachunguza uwezekano wa iwapo kuna mtu mwingine aliyehusika.

Rais Donald Trump, ambaye yumo ziarani Asia, ameshutumu kisa hicho na kusema ni "kitendo cha uovu" na kusema kwamba Wamarekani watajikwamua na kusalia na umoja.

"Na kupitia kwa machozi na kupitia huzuni hii, tunasalia imara, imara zaidi," ameongeza.

Mauaji hayo yametokea mwezi mmoja tu baada ya mshambuliaji mwingine kufyatulia risasi watu waliokuwa wakihudhuria tamasha ya muziki Las Vegas na kuwaua watu 58 pamoja na kujeruhi mamia wengine, katika kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutumia bunduki katika historia ya Marekani nyakati za karibuni.


Capture.PNG


Chanzo: BBC Swahili
 
Hawa Marekani wanavyo uwa huwa haiwaumi lakini raia wao wakipigwa huwa wanalaani, huko Syria raia wanavyo poteza maisha hakuna anae jali...
Uko sahihi kwa uelekeo mmoja tu! Yaani Asaad hajali kabisa.
 
Seems like those who die are the only victims. Nobody gives a shit...this leaves single mothers, fathers, orphans...hell! This gotta stop. Gun control has turned a song that everybody plays on their sterio...it gotta be real this time. Many have gone tombed in cold blood and the top does no shit about it. America stand together to stop guns in wrong hands. Save lives.
 
Watu 26 wameuawa kwa kupigwa risasi na mtu mwenye silaha aliyewafyatulia risasi waumini katika kanisa moja jimbo la Texas wakati wa ibada, maafisa wanasema.

Shambulio hilo lilitekelezwa katika kanisa la First Baptist Church katika mji wa Sutherland Springs, mji mdogo katika wilaya ya Wilson, Texas.

Mshambuliaji, ambaye anadaiwa kuuawa baada ya kutekeleza mauaji hayo, aliingia kanisani na kuanza kuwafyatulia risasi watu mwendo wa saa tano unusu asubuhi (17:30 GMT).

Gavana Greg Abbott amethibitisha idadi ya waliofariki na kusema ndicho kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutekelezwa kwa kutumia bunduki katika historia ya texas.

"Kutakuwa na majonzi na masikitiko mengi kwa wale walioathiriwa," aliambia wanahabari.

Mkuu wa idara ya usalama wa Texas Freeman Martin amesema waathiriwa walikuwa na umri wa kati ya miaka 5 na 72

Maafisa wamesema watu zaidi ya 20 pia walijeruhiwa na wamelazwa hospitalini.

Bw Martin amesema mshukiwa ni mwanamume mzungu wa umri wa miaka 20 ambaye alikuwa amevalia mavazi meusi na fulana ya kujikinga dhidi ya risasi pamoja na kuwa na bunduki yenye uwezo mkubwa.

Alianza kufyatua risasi nje ya kanisa kabla ya kuingia ndani na kuendelea kufyatulia watu risasi.

Mwenyeji "litwaa bunduki yake na kuanza kumfyatulia " risasi mshukiwa kabla ya mshukiwa huyo kutoroka akitumia gari.

Raia huyo alimwandama mshukiwa huyo ambaye aliendesha gari lake na kisha kuliangusha katika barabara wilaya ya Guadalupe.

Polisi waelimpata mshukiwa akiwa amefariki ndani ya gari lake.

Haijabainika iwapo alifariki kutokana na majeraha ya risasi aliyojisababishia mwenyewe au kutokana na mejaraha kutoka kwa raia huyo, Martin ameongeza.

Mshukiwa ametajwa kuwa Devin P Kelley, 26, kwa mujibu wa vyombo vya jhabari Marekani.

Polisi bado hawajathibitisha jina lake.

Mhubiri wa kanisa hilo la First Baptist Frank Pomeroy, ameambia ABC News kwamba binti yake wa miaka 14 kwa jina Annabelle ni miongoni mwa waliouawa.

Sutherland Springs ni mtaa mdogo wenye wakazi wasiozidi elfu moja ambao hupatikana kilomita 50 hivi kusini mashariki mwa mji wa San Antonio mjini Texas.

Maafisa wa FBI kutoka San Antonio wametumwa kufanya uchunguzi lakini kufikia sasa lengo la mshambuliaji halijabainika.

FBI pia wamesema mshambuliaji alikuwa mmoja pekee, lakini bado wanachunguza uwezekano wa iwapo kuna mtu mwingine aliyehusika.

Rais Donald Trump, ambaye yumo ziarani Asia, ameshutumu kisa hicho na kusema ni "kitendo cha uovu" na kusema kwamba Wamarekani watajikwamua na kusalia na umoja.

"Na kupitia kwa machozi na kupitia huzuni hii, tunasalia imara, imara zaidi," ameongeza.

Mauaji hayo yametokea mwezi mmoja tu baada ya mshambuliaji mwingine kufyatulia risasi watu waliokuwa wakihudhuria tamasha ya muziki Las Vegas na kuwaua watu 58 pamoja na kujeruhi mamia wengine, katika kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutumia bunduki katika historia ya Marekani nyakati za karibuni.


View attachment 625242

Chanzo: BBC Swahili
Trump achunguzwe kwa visa hivi. Mbona tangu aingie madarakani visa hivi vimeongezeka sana?
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom