Watu 18 wafariki na wengine 100 kujeruhiwa baada ya mvua kubwa kunyesha mashariki mwa Uganda

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Mamlaka nchini Uganda imesema watu 18 wamethibitishwa kufariki na wengine 100 kujeruhiwa baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha mafuriko wakati wa usiku kwenye wilaya mbili mashariki mwa Uganda.

Msemaji wa polisi wa eneo la Busoga Bw. Michael Kasadha alisema kuwa watu 13 walifariki kwenye wilaya ya Buyende na wengine watano kufariki kwenye wilaya ya Kamuli usiku wa jumatatu.

Maeneo yaliyoathiriwa vibaya na mvua hiyo yako kwenye uwanda wa chini karibu na mto Kyoga.
 
Ije na huku basi angalau kidogo joto limezidi Sana mpaka bajeti inaharibika kwa kununua maji ya kunywa
 
Back
Top Bottom