Watu 16 wamekufa, 65 kujeruhiwa, zaidi ya 350 wamekamatwa Uganda

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Polisi nchini Uganda wamesema kwamba watu 16 wamefariki na 65 kujeruhiwa kufuatia vurugu zilizotokea baada ya kukamatwa kwa mgombea wa urais Robert Kyagulanyi maarufu Bobi wine.

Msemaji wa polisi jijini Kampala Patrick Onyango amesema kwamba zaidi ya watu 350 wamekamatwa.

Viongozi wa chama cha Bobi Wine wamesema kwamba polisi wamekataa mtu yeyote kuonana naye anapozuiliwa katika kituo cha polisi cha Nalufenya mjini Jinja, mashariki mwa Uganda.

Nalufenya ni kituo cha polisi chenye historia ya ukandamizaji mkubwa wa haki za kibinadamu, ambapo washukiwa wa makosa makubwa kama ugaidi huzuiliwa.

Barabara kuingia katikatija mji mkuu Kampala zimefungwa huku idadi kubwa ya polisi na wanajeshi wakishika doria.

Waziri wa habari ametoa taarifa inayomsifu Rais Yoweri Museveni, namna anavyokabiliana na waandamanaji na kutoa wito kwa raia kuwatambua watu wanaofanya vurugu, kuwakamata na kuwapeleka polisi.

Msemaji wa polisi Patrick Onyango, amesema kwamba waliokamatwa walikuwa wanaharibu mali, wizi, kuchochea ghasia, kuwapiga polisi mawe na kushiriki maandamano kinyume cha sheria.

Wagombea kadhaa wa urais kupitia vyama vya upinzani wamesitisha kampeni zao hadi Bobi Wine atakapoachiliwa huru.

Wagombea 10 wa urais wanatarajiwa kukutana leo Ijumaa kujadiliana kuhusu hatua ya kuchukua.

Uchaguzi wa Uganda umepangwa kufanyika Januari 14 mwaka ujao 2021.
 
Mseveni hana budi kuja Tanzania kujifunza mbinu nzuri za jeshi letu la polisi ambazo hutumika katika kuhakikisha watu hawaandamani kwa hoja za kipuuzi kama hizi,tofauti na hapo watakufa watu wengi saña
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom