jana nilisoma kigazeti kimoja cha udaku kwamba watu 100 wamefariki btn Machi na April 2011. Baada ya kutoka loliondo. Kusema ni jambo la kawaida, lakini takwimu hizo mbona hazitolewi kila mwezi toka ktk hositali zetu? Mch. hakusema anazuia kifo. ieleweke yeye anatoa tiba tu. Kwanini kuwahesabu watu waliofariki baada ya kutoka loliondo? Mbona hamtoi idadi ya watu waliopona? Acheni hizo. acheni watu waende wapone wapunguze mizigo ya matumizi nyumbani na kwa taifa pia. Kama wewe hukupona jiulize kulikoni mbona wengine wamepona? kuliko kukimbilia kwenye maredio na kujitangaza kuwa dawa hiyo ni feki. Mbona tunapokwenda hatuendi kutangaza redioni kuwa tunakwenda lol? Kifo kipo hata kama angeshuka Muumba mwenyewe akakupatia dawa.