Wananchi 15 wanaoishi Kitongoji cha Kahomwele,Kijiji cha Doroto,Tarafa ya Itigi,wilayani Manyoni, Mkoa wa Singuda, wameamuriwa kulipa faini ya shilingi 35,000/= kila mmoja kwa madai kuwa walikula chakula kilichobaki ambacho kiliandaliwa kwa ajili mbunge wa jimbo la Manyoni magharibi (CCM) Bwana John Paul Lwanji. Baada ya Mbunge kula na kuondoka wananchi wakachukua chakula kilichobaki Mezani wakala, Chakula hicho kiliandaliwa kwa michango ya wananchi wenyewe kwa ajili ya ziara ya Mbunge. Ila wamegeukwa na Mwenyekiti wa Kijiji na Afisa Mtendaji kuwa wamesababisha uvunjifu wa Amani na kutakiwa kulipa kiasi hicho cha fedha. Kwa mantiki hizo zitachangwa 525,000. Watetezi wa haki za binadamu saidieni hilo huko Singida..