Watoto wetu wa Siku hizi 'wamerogwa' au 'wamelaaniwa' na nani hasa kimalezi, kiuwajibikaji na kimaadili?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,468
108,621
Yaani kabisa (Mtoto) Mvulana au Msichana wa Darasa la Tano hadi la Saba anafuliwa Nguo zake, anaamshwa kwenda Shule, akila anaacha Vyombo mezani House Girl avitoe na anaamshwa Asubuhi kujiandaa kwenda Shule?

Na kinachonishangaza na Kunisikitisha zaidi unakuta Wazazi Wao kipindi cha Utoto (Udogo) Wao wamekula mno Msoto wa Kimalezi kutoka kwa Wazazi na Walezi ambao uliweza Kuwajenga vyema Kiakili na Kimaadili hatimaye leo wameyafikia Mafanikio waliyoyapata.

Nawashukuru mno Wazazi na Walezi wangu ambao kiukweli GENTAMYCINE nilipokuwa Mdogo walikuwa wakinipa (wakinifundisha) Majukumu mbalimbali ya Kimaisha (ya nyumbani na maishani) ambapo kwa Udunduna (Ujinga) wangu Kipindi hicho nilikuwa naona hawanipendi na Wananitesa ila nilivyokuwa na mpaka leo hii najiona ni mwenye bahati ya Kupewa Msoto ule na Wao kwani Wamenijenga vyema Kimalezi, Kiutu, Kiuwajibikaji na Kimaadili pia. Mwenyezi Mungu awabariki mno na sana.

Mitoto ya Siku hizi ikipigwa (ikichapwa) tu kidogo inaanza Kulia na Kudeka halafu Mzazi nae anamuacha na kuanza 'Kumbebisha' Mwanae wakati Kudadadeki enzi zangu GENTAMYCINE nikizingua tu 'Home' nilikuwa nakula Kipigo cha Kishalubela (Kitakatifu) kutoka kwa 'Mshua' na kabla sijakaa sawa Kuugulia (Kusikilizia) Maumivu Mjomba au Mzee wa Jirani nae (nao) wakija walikuwa wakinipa 'Vipondo' vile vile kwanini nisinyooke na kuwa na Adabu?

Tuliolelewa Kiukakamavu (Kijeshi) na Wazazi pamoja na Walezi wetu tumepata Faida Kubwa kuliko hawa Watoto (Vijana na Wasichana) wa Siku hizi (wa leo) ambao wanalelewa 'Kimayai' na 'Kivideo' zaidi ambapo tayari tunaokaa na Jamii tumeshaanza kuona Athari zake ambapo wengi wao ni Wapumbavu (Mapopoma) sana, hawana Adabu na wapo wapo tu.

Mitoto ya Siku hizi hata haipelekwi Vijijini (hasa wakati wa Likizo) ili kujifunza Maisha yote na Likizo zote wanabaki Dar es Salaam na kupelekwa tu Kuzurula katika 'Korido' za 'Mlimani City' wakati enzi zetu akina GENTAMYCINE ikifika tu Likizo Kudadadeki Safari Kijijini kwa akina Babu na Bibi na ukifika huko Unalima, Unachunga Ng'ombe, Unafundishwa Kuvua Samaki Ziwani na kuwakwepa Mamba wasikufanye Kitoweo chao cha Siku na unabeba Maji kutoka Mtoni kwa umbali wa Tegeta Nyuki na Mbagala Kipati na Maisha yanaenda hulalamiki.

Kizazi cha sasa 'Kimeharibika' Kimalezi!!!
 
Utaratibu wa maisha huwa unabadilika kutoka enzi kwenda enzi.

Hata hizo enzi ulizosimulia kuwa uliishi wewe, mambo uliyofanya au wazee wako kukuelekeza kufanya yapo tofauti na enzi nyingine nyuma zaidi ya hapo.

Mathalani, zamani zaidi mtu alirithishwa elimu isiyo ya darasani, baadaye kukaja kuwa na elimu ya darasani.

Zamani zaidi hakukuwa na mwingiliano sana baina ya jamii na jamii, wanadamu waliishi kijima lakini baadaye na hata sasa kuna mwingiliano mkubwa sana na hata jamii moja kufanya maisha na jamii nyingine yenye tamaduni tofauti tofauti.

Pia zamani hakukuwa na maendeleo ya mahali watu wanaishi kama ilivyo sasa, umetolea mfano wa namna mlivyokuwa mnaenda mbali kuteka maji. Lakini kwa sasa hili limepungua(bado kuna sehemu ni ishu), maji yanasambazwa na mamlaka na hatua hizi tumezipa jina 'maendeleo'
 
Utaratibu wa maisha huwa unabadilika kutoka enzi kwenda enzi...

Hata hizo enzi ulizosimulia kuwa uliishi wewe, mambo uliyofanya au wazee wako kukuelekeza kufanya yapo tofauti na enzi nyingine nyuma zaidi ya hapo...

Mathalani, zamani zaidi mtu alirithishwa elimu isiyo ya darasani, baadaye kukaja kuwa na elimu ya darasani...

Zamani zaidi hakukuwa na mwingiliano sana baina ya jamii na jamii, wanadamu waliishi kijima lakini baadaye na hata sasa kuna mwingiliano mkubwa sana na hata jamii moja kufanya maisha na jamii nyingine yenye tamaduni tofauti tofauti...

Pia zamani hakukuwa na maendeleo ya mahali watu wanaishi kama ilivyo sasa, umetolea mfano wa namna mlivyokuwa mnaenda mbali kuteka maji. Lakini kwa sasa hili limepungua(bado kuna sehemu ni ishu), maji yanasambazwa na mamlaka na hatua hizi tumezipa jina 'maendeleo'
Umejibu Kisomi sana mpaka nimefufahi Mkuu. Haya Maoni yako yameniongezea Maarifa fulani. Asante mno.
 
Kwenye mabano yako (Vijana na Mabinti).
Ulilenga nini?
Means mabinti sio Vijana?
Nitaomba Wataalam wa Kiswahili watusaidie Kutuelimisha hapa kwani nimekariri Kijana ( Vijana ) huwa ni Wavulana tu ila nimeona nawe hapa Umehoji kuwa je, Wasichana nao siyo Vijana?

Unaweza ukawa uko sahihi Mkuu na Mimi Kukosea ( Kukengeuka ) hivyo namuomba Ndugu Omi Sigala ( Mbobezi wa Lugha ya Kiswahili ) aje kutusaidia / kutuelimisha zaidi katika hili au hata JF Members wanaokijua vyema Kiswahili.
 
Roho mbaya tu hio kwa kina dada wa kazi unataka wale wapi

Inatakiwa ujue huo ndio wigo umeongezeka kwa watu wengine kupata mkate wao

Kama ww huezi kuzalisha huo mkate kwa watu wengine ni wewe na roho yako ya korosho fanya kila kitu ww na familia yako io pesa ijizungushe humo humo ndan kwenye familia yako
 
Roho mbaya tu hio kwa kina dada wa kazi unataka wale wapi
Inatakiwa ujue huo ndio wigo umeongezeka kwa watu wengine kupata mkate wao
Kama ww huezi kuzalisha huo mkate kwa watu wengine ni wewe na roho yako ya korosho fanya kila kitu ww na familia yako io pesa ijizungushe humo humo ndan kwenye familia yako
Mkuu wangu hii Mada yangu na Mimi kuniambia nina Roho Mbaya vinahusiana vipi?

Mola anipe Uvumilivu nisikujibu vibaya.
 
Zamani kulikua na mazingira magumu katika maisha na miundo mbinu yake( kama usafiri, mawasiliano nk) as a result mazingira magumu yakaleta tough people like you Genta na wengine wa enzi hizo

Albert Einstein alisema;

Tough times create strong people, strong people create easy times, easy times create weak people and weak people create again tough times. Ni vicious circle hiyo

Kwa hiyo kama majumbani mwetu tuna mtoto wa std V au VI mpaka aamshwe kwenda shule au binti wa chuo hajui hata kupika chakula chake mwenyewe ba nguo afuliwe hadi chupi ujue you are rising up a looser!
 
Ha ha ha ha ha ha kwanini Mkuu wangu?
Imetoa elimu Kali Sana, nimekusoma kwa sauti, ili huyu mama aelewe haya matoto baadaye yatakuja kutuchinja ama kutunisha sumu, ili yagombanie jasho letu.
Nawapenda wanangu Ila hili la mama yao, eti dada mbona nyumba chafu na mito IPO humo imekaa tu huwa siliafiki, eti dada hujapika wakati mitoto inatakiwa ijue kujipikia na kutupikia!

Wale watoto iko siku nitamsafirisha mama Yao, dada nampa likizo, tubakie sisi, niwape masomo ya ujamaa na kujitegemea! Azimio la Arusha!
 
Imetoa elimu Kali Sana, nimekusoma kwa sauti, ili huyu mama aelewe haya matoto baadaye yatakuja kutuchinja ama kutunisha sumu, ili yagombanie jasho letu.
Nawapenda wanangu Ila hili la mama yao, eti dada mbona nyumba chafu na mito IPO humo imekaa tu huwa siliafiki, eti dada hujapika wakati mitoto inatakiwa ijue kujipikia na kutupikia!

Wale watoto iko siku nitamsafirisha mama Yao, dada nampa likizo, tubakie sisi, niwape masomo ya ujamaa na kujitegemea! Azimio la Arusha!
kizazi cha smary phone hawakawii kumpigia mama yao simu wanateseka
 
kizazi cha smary phone hawakawii kumpigia mama yao simu wanateseka
Mkuu nachanga kibubu, nampiga shule nje ya nchi, miezi 6 tu, akirudi watoto wanajua dunia siyo hii inayoendeshwa na dada! Wazungu watoto wanajitegemea mapema!
Hata wakimwambia atanuna na kususa huko mbali! Yeye pia aone wazungu wanafanya anayofanya yeye??

IST huko wazungu mtoto anakuwa organized tokea chekechea, anajua akifika begi likae wapi, lunchbox wapi water bottle wapi, sisi sante Maria kila kitu wanafanyiwa! Tumekuwa watumwa wa hawa watoto!
Ndiyo maana tunakengeuka na kunatafuta superficial Raha na michepuko!

Akirudi viatu socks uniform na kibezi anacho dada aandae! Visipoonekana dada ajibu!
Mie nawaangalia tu hawajui navyopangilia mapinduzi!
 
Yaani kabisa (Mtoto) Mvulana au Msichana wa Darasa la Tano hadi la Saba anafuliwa Nguo zake, anaamshwa kwenda Shule, akila anaacha Vyombo mezani House Girl avitoe na anaamshwa Asubuhi kujiandaa kwenda Shule?

Na kinachonishangaza na Kunisikitisha zaidi unakuta Wazazi Wao kipindi cha Utoto (Udogo) Wao wamekula mno Msoto wa Kimalezi kutoka kwa Wazazi na Walezi ambao uliweza Kuwajenga vyema Kiakili na Kimaadili hatimaye leo wameyafikia Mafanikio waliyoyapata.

Nawashukuru mno Wazazi na Walezi wangu ambao kiukweli GENTAMYCINE nilipokuwa Mdogo walikuwa wakinipa (wakinifundisha) Majukumu mbalimbali ya Kimaisha (ya nyumbani na maishani) ambapo kwa Udunduna (Ujinga) wangu Kipindi hicho nilikuwa naona hawanipendi na Wananitesa ila nilivyokuwa na mpaka leo hii najiona ni mwenye bahati ya Kupewa Msoto ule na Wao kwani Wamenijenga vyema Kimalezi, Kiutu, Kiuwajibikaji na Kimaadili pia. Mwenyezi Mungu awabariki mno na sana.

Mitoto ya Siku hizi ikipigwa (ikichapwa) tu kidogo inaanza Kulia na Kudeka halafu Mzazi nae anamuacha na kuanza 'Kumbebisha' Mwanae wakati Kudadadeki enzi zangu GENTAMYCINE nikizingua tu 'Home' nilikuwa nakula Kipigo cha Kishalubela (Kitakatifu) kutoka kwa 'Mshua' na kabla sijakaa sawa Kuugulia (Kusikilizia) Maumivu Mjomba au Mzee wa Jirani nae (nao) wakija walikuwa wakinipa 'Vipondo' vile vile kwanini nisinyooke na kuwa na Adabu?

Tuliolelewa Kiukakamavu (Kijeshi) na Wazazi pamoja na Walezi wetu tumepata Faida Kubwa kuliko hawa Watoto (Vijana na Wasichana) wa Siku hizi (wa leo) ambao wanalelewa 'Kimayai' na 'Kivideo' zaidi ambapo tayari tunaokaa na Jamii tumeshaanza kuona Athari zake ambapo wengi wao ni Wapumbavu (Mapopoma) sana, hawana Adabu na wapo wapo tu.

Mitoto ya Siku hizi hata haipelekwi Vijijini (hasa wakati wa Likizo) ili kujifunza Maisha yote na Likizo zote wanabaki Dar es Salaam na kupelekwa tu Kuzurula katika 'Korido' za 'Mlimani City' wakati enzi zetu akina GENTAMYCINE ikifika tu Likizo Kudadadeki Safari Kijijini kwa akina Babu na Bibi na ukifika huko Unalima, Unachunga Ng'ombe, Unafundishwa Kuvua Samaki Ziwani na kuwakwepa Mamba wasikufanye Kitoweo chao cha Siku na unabeba Maji kutoka Mtoni kwa umbali wa Tegeta Nyuki na Mbagala Kipati na Maisha yanaenda hulalamiki.

Kizazi cha sasa 'Kimeharibika' Kimalezi!!!
Jana Nilikuwa na safari ya uongo na kweli toka wilaya moja kwenda nyingine. Nikakaa na mwanamke mmoja kwenye kiti akiwa na Mtoto wake wa kiume miaka 4 hivi. Tukiwa tunaendelea na safari yule Mtoto alikuwa anakunywa juice ya embe. Ilivyofika nusu akatosheka
Akamwambia mama yake, mama akamwambia funga utunze utakunywa baadaye Mtoto akagoma akataka mama ndo afunge. Mama akaona basi zima litamuona mbulura kugomewa na Mtoto, akaamuru Kwa ukali funga hiyo juice. Kilichotokea Hakuna aliyetegemea, Mtoto kachukua kopo la juice kaimwaga chini, kondakta akamkalipia, akapigwa na kopo tupu, abiria kiti cha pili akatia neno akafuatwa atiwe adabu. Kiujumla Hakuna aliyechangia mada ambaye hakufuatwa na "Junior" na kutiwa adabu. Nikiangalia Hali ya mama yule mwenye umri Kati ya 19-21 anaonekana ana maisha ya kawaida Sana na alichonishangaza zaidi alishukia njiani kijijini. Nilibaki na maswali Aina ya malezi ya watoto wa Aina hii tatizo ni Wazazi/walezi au watoto wanaozaliwa siku hizi Wana akili tofauti na wa zamani?
 
Roho mbaya tu hio kwa kina dada wa kazi unataka wale wapi

Inatakiwa ujue huo ndio wigo umeongezeka kwa watu wengine kupata mkate wao

Kama ww huezi kuzalisha huo mkate kwa watu wengine ni wewe na roho yako ya korosho fanya kila kitu ww na familia yako io pesa ijizungushe humo humo ndan kwenye familia yako
Mkuu hata kama kuna Dada wa kazi hapo Nyumbani,lazima na Watoto nao wajuwe kuwajibika au kumsaidia Dada kazi, maana Dada nae ni Binaadamu anaweza uguwa! Je kwa hiyo shughuli za Nyumbani zitasimama hadi Dada apone wakati una vijana hapo Nyumbani!?
 
Back
Top Bottom