mabadilikosasa
JF-Expert Member
- Dec 23, 2010
- 379
- 85
Jamani. Inasikitisha. Hawa watoto wadogo kiasi hiki kati ya miaka 2 had 10 katika maeneo ya mnazi mmoja, magomeni, kinondoni, barabara ya ali mwinyi, watakuja kuwa watu wazima wa aina gani??. Unasimamisha gari wanazunguka gari nzima wanaomba msaada!. Je tukiwapa hata hiyo hela watajua kweli matumizi yake? hakuna namna ya kuwapeleka hawa watoto mashuleni wakasoma huko huko na wakala huko?? Hii wazara ya watoto inafanya kazi zipi? au hii wizara haina budget?? Je ccm ina sera zipi za kusaidia hawa watoto. CCM, hizi gharama zote wanazotumia kusafiri mikoani kuelezea kuhusu kujivua gamba (kumbe ni utapeli), na ma V8 yao, sii wangeweza kusaidia hawa watoto ....jamani tuwe na huruma.