Watoto wa vigogo na ajira BoT

izihaka

Member
Jan 25, 2008
16
7
Mtawala wa forum hii na wote kwa ujumla napenda kuwapa mada hii iwe kama ni ushahidi mojawapo wa sakata la BoT. Hili suala la watoto wa vigogo kuajiriwa Bot si la uongo kwani

1. Rogers Sumaye alipata ajira hata kabla hajamaliza shule Uk kwani kuna watu walianza kufanya interview za kumsindikiza.
2. Kigoda naye the same
3. Lowasa's the same
4. And many others who have brothers there or relatives

Ishu hapa sio kuwa na sifa za kufanya kazi Bot bali je walipitia usahili na taratibu za ajira serikalini?

Je, ni watu wangapi wenye sifa walifanya interview na kushinda na bado wakapigwa chini?

Inasikitisha kuona kuwa hata Gavana mpya anatetea maovu akiwa ofisini hata mwezi haujaisha ni SHIDA hii

May 30, 2008:
UCHUNGUZI uliofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuhusu ajira za upendeleo kwa watoto, ndugu na jamaa za wakubwa ndani ya Benki Kuu (BoT), umekamilika.

Kukamilika kwa uchunguzi huo kulitangazwa mbele ya waandishi wa habari jana na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu.

Ingawa hakuwa tayari kusema kile kilichomo ndani ya taarifa hiyo kwa maelezo kuwa TAKUKURU ni taasisi inayojitegemea, Gavana Ndulu alisema, tayari BoT imeshaanzisha uchunguzi wake mwingine kufuatilia suala hilo hilo la ajira.

Gavana Ndulu alisema kuwa katika uchunguzi wake, TAKUKURU ilikuwa ikichunguza ajira za watu 14 wanaohusishwa na viongozi waandamizi kulingana na maelezo waliyopewa na ngazi husika.

Alisema baada ya kupata taarifa hiyo ya TAKUKURU, BoT nayo ikaamua kuanzisha uchunguzi wa ajira za wafanyakazi wake wote, ili kuepusha malalamiko kutoka upande fulani pamoja na kuepuka kupelekwa mahakamani.

"Wale TAKUKURU walifanya uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo kulingana na maelezo waliyopewa, lakini sisi tunataka kufanya uchunguzi wa ajira za wafanyakzi wote," alisema Ndulu.

Alisema kuwa ndani ya BoT kila mfanyakazi ni sawa, awe mtoto wa kigogo au wa mkulima, ndiyo maana wameamua kuwashirikisha wafanyakazi wote kwenye uchunguzi huo.

"Unajua leo hii ukifanya uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo pekee, kesho unaweza kujikuta hata hao watoto wa wakulima nao walipata ajira kwa njia zisizokubalika," alisema Ndulu.

Aidha, alisema uchunguzi wao utakuwa tofauti zaidi, kwani wao watafuata sheria ya mwaka 2004 (iliyobadilika), wakati TAKUKURU walitumia sheria ya mwaka 2000.

Ndulu hakuwa tayari kufafanua utofauti wa sheria hizo, lakini alidai kuwa katika uchunguzi huo, TAKUKURU haikutumia sheria iliyotumika kuwaajiri watoto hao.

"Hapa kunaweza kutokea tofauti ya kutokuelewana na jamii ikachukulia vibaya mambo haya, kwani sheria zilizotumika kufanya uchunguzi zilishabadilishwa, sasa sijui itakuwaje," alisema Ndullu.

Aidha, alisema ni vizuri jamii ikavuta subira ya kupata matokeo ya uchunguzi wa BoT kuhusiana na ajira za wafanyakzi wake na asingependa kutoa matarajio ya kazi hiyo mapema.

"Jamani nisingependa kuwaahidi nyinyi au wananchi wengine hivi sasa matarajio ya uchunguzi wetu, bali ninawaomba tungoje hayo matokeo," alisema.

Hivi karibuni, vyombo mbalimbali vya habari vilitoa taarifa na kutaja majina ya watoto wa vigogo ambao wanafanya kazi BoT, wakisadikiwa kuwa walipata kazi hizo kutokana na ushawishi au nafasi za ndugu zao.

Taarifa hizo pia zilinukuu viongozi wa TAKUKURU wakidai wanachunguza ajira za watoto hao wa vigogo kuona kama walipata ajira BoT bila kufuata taratibu zilizotakiwa.

Juhudi za Tanzania Daima kumtafuta Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Edward Hosea, kuthibitisha kukamilika kwa uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo hao ziligonga mwamba baada ya simu yake kutokuwa na majibu.

Taarifa kwamba kulikuwa na ajira za upendeleo ndani ya BoT kwa mara ya kwanza zilisambazwa katika mtandao wa intaneti kabla vyombo kadhaa vya hapa nchini kuripoti taarifa hizo.


CHANZO:
Tanzania Daima

=======
Baadae: Watoto wa vigogo BoT wasafishwa
=======

Oktoba 07, 2012
Ona nchi yetu ilivyo

1. FILBART SUMAYE,
2. PAMELA LOWASA,
3. ZARIA KAWAWA,
4. HERIETH LUMBANGA,
5. SALAMA MWINYI,
6. RECHAL MUGANDA,
7. SALMA MAHITA,
8. JUSTINA MUNGAI,
9. KENETH NCHIMBI,
10. BLASIA W. MKAPA,
11. VAOLETH LUHANJO,
12. LIKU KATE KAMBA,
13. THOMAS MONGELA na
14. JABIRI KIGODA.

HIYO NI TIMU YA WATOTO WA VIGOGO WALIOAJIRIWA BOT BADO KATIKA BALOZI ZETU NJE YA NCHI. NCHI YETU INAFISADIWA NANI WA KUTUOKOA WENGI WAO WAMEGHUSHI ELIMU ZAO

SASA SIJUI KWAMBA NI KUJIVUNIA VIONGOZI WETU KUTUONYESHA KUWA ELIMU NI MSINGI WA MAISHA KWA KUWAPA WATOTO WAO ELIMU BORA AU NI WANANCHI KUONA HUKO NI KUPENDELEANA KATIKA AJIRA ZENYE MASLAHI MAZURI AU NI WIVU WA WATANZANIA TU?

Oktoba 23, 2012
Gazeti la Jamuhuri la October 23, 2012 Limewataja vijana wafuatao kuwa ni watoto wa vigogo waliojazana BOT: Kweli Tanzania ina wenyewe

Salama Ali Hassan Mwinyi
Filbert Tluway Sumaye
Zaria Rashid Kawawa
Blasia William Mkapa
Herriet Marten Lumbanga
Pamela Edward Lowassa
Rachel Muganda
Salma Omary Mahita
Justine Mungai
Kenneth Nchimbi
Violet Philemon Luhanjo
Liku Kate Kamba
Thomas Mongela
Jabir Abdallah Kigoda
 
Weka wazi hayo maovu anayotetea gavana mpya basi, hapa ni JF mkuu, where we dare talk openly...toa dukuduku lako.

To borrow from the old mikingamo radio show "tuambie nani yuko wapi na anafanya nini kulihujumu taifa"
 
Mtawala wa forum hii na wote kwa ujumla napenda kuwapa mada hii iwe kama ni ushahidi mojawapo wa sakata la BoT. Hili swala la watoto wa vigogo kuajiriwa Bot si la uongo kwani
1. Rogers Sumaye alipata ajira hata kabla hajamaliza shule Uk kwani kuna watu walianza kufanya interview za kumsindikiza.
2. Kigoda naye the same
3. Lowasa's the same
4. And many others who have brothers there or relatives
Ishu hapa sio kuwa na sifa za kufanya kazi Bot bali je walipitia usahili na taratibu za ajira serikalini?
Je ni watu wangapi wenye sifa walifanya interview na kushinda na bado wakapigwa chini?
Inasikitisha kuona kuwa hata Gavana mpya anatetea maovu akiwa ofisini hata mwezi haujaisha ni SHIDA hii

KAKA ACHA MAPEPE,UNAJITUNGIA HABARI TU HAPA,KAMA HUNA KIPYA KAA PEMBENI.KWANZA SUMAYE HANA MTOTO ANAEITWA ROGERS,BALI ANA WATOTO WAWILI AMBAO NI FILBERT NA FRANK,PILI FILBERT ALIRUDI NCHINI BAADA YA KUMALIZA MASTERS YAKE YA COMPUTER SCIENCE.NA ALIPORUDI ALIKAA MIEZI NANE AKIFANYA KAZI KTK KAMPUNI BINAFSI NDIO AKAAJILIWA.HUO UZUSHI UMETOA WAPI KAKA?ATA UKIULIZA WATU ALIOSOMA NAO TOSAMAGANGA F 5&6 WATAKWAMBIA JINSI ALIVYO MTU SIMPLE NA WAKUJITUMA.KAZINI KWAKE WANAMTEGEMEA MTAFUTE BOSI WAKE MZEE MASAWE ATAKWAMBIA.PIA WAPO WENYE CPA NA
NK.WIVUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU MBAYA JAMANI
 
Nimekuwa nikizifuatilia kwa karibu hizi mada zinazohusiana na watoto wa vigogo kupata ajira BOT ila kuna wakati inafikia wachangiaji aidha wanachukua haya masuala kuwa personal. Nadhani hii yote ni kutokana na kukosekana kwa vidhibiti vya kutosha kuhusiana na hii ishu kwa ujumla.

Mimi binafsi natambua wazi kwamba hakuna ambae angependa mtoto wake apate shida katika dunia hii wakati yeye kama mzazi anao uwezo mkubwa tu wa kumsaidia > Huu ni ubinafsi ambao upo katika kila binadamu (inherent) kinachogomba hapa nadhani ni procedures na appropriateness ya ajira za hawa watoto wa vigogo kuingia BOT kwa wingi kama inavyoonekana. Na je ni kwa nini walimwagwa BOT pekee kwa sababu nina uhakika hii sio bahati mbaya!?

Kuna mchangiaji mmoja aliwahi kuomba kama kuna mtu anazo data (CV na Position wanazohold BOT) juu ya hawa watu azimwage hapa JF lakini sina uhakika kama kuna mtu alirespond may be hakuna aliyekuwa na access ya hizo data.

Kwa jinsi hii ninavyoona hapa sidhani kama hii mada itaweza kuadd value kama hakuna Evidence ya kutosha kuthibitisha kinachosemekana. Tutakuwa kila siku tukiona watu wakirushiana maneno kwa kuhisi kwamba waanzisha mada wanasumbuliwa na wivu na sio kutaka uadilifu uwepo ktk serikali na vyombo vyake vyote.

Let anyone with these data bring them forward for us to scrutinize!

D
 
Nyie teteaneni, mkizani hiyo nchi Mungu aliwapa nyie na babazenu hao mafisadi, ila patageuka siku moja hapo mtatafuta pa kujificha mtakosa, maana manyumba, migari yenu watu watachoma, msione kam nyie ndo mmebarikiwa kumbe wezi wakubwa na baba zenu, iko siku tu, itafika, sijui utayazungumza haya??
Hongera sana kwa kuwa mtoto wa Fisadi, Umebarikiwa sana
NA HAPO NDIPO MTAKUFA NYINYI NA WAJUKUU ZENU WENGINE TUTAPAA KWENDA ZETU NG'AMBO KUENDELEA KULA MAISHA.NANI ALIEKWAMBIA VITA VYA KONY VINAMGUSA MUSEVEN NA FAMILIA YAKE?
 
Hii kitu mbona imeshazungumziwa jamani. Mwanzishaji wa hii thread inabidi afanye kuperuzi kabla ya kumwaga hizi pumba, zimeshachambuliwa!
 
Kila mzazi angependa mtoto wake apate kazi nzuri na yenye heshima. Kinachotatanisha au kinachotakiwa ni kuwa huyu mtoto anazo sifa sinazotakiwa na anaimudu hiyo kazi?
 
Vigogo watano BoT wasimamishwa kazi
* Ni wanaodaiwa kuhusika na kashfa ya Richmond


Na Ramadhan Semtawa


SAFISHASAFISHA ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeendelea kufuatia vigogo watano wa benki hiyo kusimamishwa kazi.


Hatua hiyo imekuja mwezi mmoja baada ya Gavana mpya wa BoT Profesa Benno Ndulu, kufanya mabadiliko mengine katika ngazi za wakurugenzi wa benki hiyo yakiwamo matawi na makao makuu, isipokuwa Mwanza.


Kwa mujibu wa taarifa zilizofikia gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, vigogo hao walisimamishwa kazi juzi.


Taarifa hizo ziliongeza kwamba, uamuzi wa BoT kuwasimamisha watumishi hao ni sehemu ya mchakato wa kuisafisha taasisi hiyo nyeti ambayo imekumbwa na tuhuma za ufisadi.


BoT chini ya aliyekuwa gavana wake, Daud Ballali imekumbwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi, ikiwemo ujenzi wa majengo pacha (Twin Towers) ya benki hiyo na wizi wa zaidi ya Sh133 bilioni katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).


Taarifa hizo zilifafanua kwamba, kusimamishwa kwa wafanyakazi hao pia kunahusishwa na mapendekezo ya Bunge kuhusu malipo ya ziada ya Sh5 bilioni katika mkataba wa Richmond/Dowans.


Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana jioni Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alisema taarifa za hatua hiyo zimefikishwa kwenye vyombo husika.


Profesa Ndulu ambaye hata hivyo alionekana kutotaka kuzungumza moja kwa moja kuhusu suala hilo alisema kwa sasa si sahihi kuanza kueleza majina na nafasi za waliosimamishwa.


Profesa Ndulu alisema wafanyakazi hao wana haki zao za msingi, hivyo si sahihi kuanza kuwaanika hadharani kupitia vyombo vya habari.


Hata hivyo, alikiri kufikisha ripoti ya wafanyakazi hao katika vyombo husika kwa kufuata mtiririko wa utendaji ndani ya serikali.


"Kuna mambo mengine yanahusu watu, na wao wana haki zao, siwezi kufanya kila kitu na vyombo vya habari," alisema na kuongeza:


"Lakini, tumepeleka ripoti katika vyombo husika kwa kuzingatia mtiririko wa mambo yanavyopaswa kuwa."


Profesa Ndulu aliongeza kwamba, iwapo BoT itakuwa ikifanya kazi kwa kueleza kila kitu hadharani watumishi wanaoachishwa au kuchukuliwa hatua nyingine wanaweza kushitaki.


Alipoulizwa zaidi kwamba, BoT ni taasisi nyeti ya umma ambayo Watanzania wanaifuatilia kwa makini baada ya kukumbwa na tuhuma hizo za ufisadi, sasa iweje, mabadiliko kama hayo umma usijue, alijibu: "Siyo kwamba tunaficha taarifa, isipokuwa ni taratibu na kulinda haki za kila mfanyakazi kama raia na binadamu."
 
Mimi hizi naona kasi za sakafuni haziishi kuzimika.JK alianza na haya mata hivi mara vile leo anakimbia hata maamuzi yake na kujijitea kwamba hakumfukuza Lowasa ila maamuzi cha CC.So mimi sioni jipya . Majina nayo yako wapi ya walio panguliwa na kupigwa chini ?Saabu ni hizi hizi za kashfa ama ?
 
Kama kawaida JF mambo hadharani, waliotimuliwa BoT ni hawa hapa:
1.Imani David Mwakosya
2.Esta Mary Komu
3.Isaack Hubert Kilato
4.Bosco Ndimbo Kimela
5.Elisa Peter Issangya
 
Kwa Tabia ya watanzania ilivyo hawa jamaa waliosimamishwa kazi watarudi tu maana haki na sheria ni tofauti sana (sheria inataka asimame na haki itamtaka arudi kazini) kama watu hawa wamesimamishwa kwa kesi ya EPA au ya RICHMOND wafukuzwe kama ni kesi tofauti na hiyo basi waendelee kusimama, vinginevyo tutumie hoja ya mhesh.Ndesambulo ambae anasema watu kama hawa China wananyongwa maana china hawataki michezo ya ajabuajabu kama hii ya ufisadiufisadi.
 
Kwa Tabia ya watanzania ilivyo hawa jamaa waliosimamishwa kazi watarudi tu maana haki na sheria ni tofauti sana (sheria inataka asimame na haki itamtaka arudi kazini) kama watu hawa wamesimamishwa kwa kesi ya EPA au ya RICHMOND wafukuzwe kama ni kesi tofauti na hiyo basi waendelee kusimama, vinginevyo tutumie hoja ya mhesh.Ndesambulo ambae anasema watu kama hawa China wananyongwa maana china hawataki michezo ya ajabuajabu kama hii ya ufisadiufisadi.


Kizito you have saidi it all . Hapa sasa nashindwa kujua .Je wametimliwa kazi ama wamesimamisha kazi ? Maana mkanganyo huu .
 
Kutimuliwa isiwe mwisho, lazima wawajibishwe; wafunguliwe kesi warudishe walichoiba na jela waende. Na wote wengine wafuate mkumbo huuhuu tukianzia na Balali, Lowassa, Karamagi etc. tuache "kulambwa kisogo" eti wamejiuzulu mara wamesimamishwa then giiiiiii hakuna linaloendelea,,,, wanazidi kupeta tu na pesa za wazalendo, is not fair!!!Inauma sana how the country is robbed kwa kasi ya ajabu!!!!kuna kilichobaki kweli??? I doubt.
 
Kama kawaida JF mambo hadharani, waliotimuliwa BoT ni hawa hapa:
1.Imani David Mwakosya
2.Esta Mary Komu
3.Isaack Hubert Kilato
4.Bosco Ndimbo Kimela
5.Elisa Peter Issangya

Hivi hawa sio vidagaa kweli? Muungwana anachezea maisha ya walalahoi kwa ulaghai kuwa anachukua hatua huku akiendelea kuwapamba mafisadi. Ipo Siku.
 
Tatizo ni kuwa Watanzania tumeshajionyesha kuwa tuko very cheap.They can buy us like a cup of coffee. That is why we are treated cheaply.Tunafanyiwa kidogo tunapiga makofi,lakini naamini tutakapojua thamani yetu na nini tunahitaji kukipata toka kwa watu tunaowachagua(ila sio wanaotununua)then naamini hawatatufanyia mambo nusu nusu.
 
Kama kawaida JF mambo hadharani, waliotimuliwa BoT ni hawa hapa:
1.Imani David Mwakosya
2.Esta Mary Komu
3.Isaack Hubert Kilato
4.Bosco Ndimbo Kimela
5.Elisa Peter Issangya

Hapa hakuna tulichoambiwa maana bado hatujui hawa watu wana nyadhifa gani na wanahusika vipi na hizo tuhuma za ufisadi.
 
Kusimamishwa kazi sio hoja,hatua gani zinachukuliwa zaidi dhidi ya watu hawa. Hawa wamelitia taifa hasara kubwa na tunaimani mpaka wamesimamishwa kuna uchunguzi ambao tayari umefanyika na ndiyo maana hatua hiyo imefikiwa. Sioni sababu kwanini mpaka leo hatuwaoni mahakamani,maana hapa ukawihi kusikia kulitokea techniqual problems wakati wa maamuzi na mtu akarudishwa kazini
 
Kusimamishwa kazi sio hoja,hatua gani zinachukuliwa zaidi dhidi ya watu hawa. Hawa wamelitia taifa hasara kubwa na tunaimani mpaka wamesimamishwa kuna uchunguzi ambao tayari umefanyika na ndiyo maana hatua hiyo imefikiwa. Sioni sababu kwanini mpaka leo hatuwaoni mahakamani,maana hapa ukawihi kusikia kulitokea techniqual problems wakati wa maamuzi na mtu akarudishwa kazini
 
Kama kawaida JF mambo hadharani, waliotimuliwa BoT ni hawa hapa:
1.Imani David Mwakosya
2.Esta Mary Komu
3.Isaack Hubert Kilato
4.Bosco Ndimbo Kimela
5.Elisa Peter Issangya


Samahani, naona watu walikuwa wanauliza majina. Uzuri ni kuwa majina yalishawekwa hapa siku nyingi... tatizo vyombo vyetu vya habari vingekuwa vinakuja hapa wasingeripoti hili wiki kadhaa baadaye. Hatuhitaji watuambie majina, tunawajua.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom