Watoto wa rafiki wa mke wangu ni wangu, nawahitaji

Nimekuwa nikifuatilia thread zako humu jamvini,Wiyelele,naona kama ni za kufikirika sana vinginevyo maisha yako ni great adventure.Otherwise good luck bro.
 
utajua kwanini unakula chakula kizuri alafu unakunya mavi yananuka then unayakimbia kwa harufu mbaya .utashuhudia wakichinjwa kama kuku hao watoto

nivea wll i need is your help. Nataka niondokane na haya matatizo maana yamenisumbua kwa uda mrefu. Nakata niwe mpya niingiapo 2013 Mungu akipenda.
 
Nimekuwa nikifuatilia thread zako humu jamvini,Wiyelele,naona kama ni za kufikirika sana vinginevyo maisha yako ni great adventure.Otherwise good luck bro.

Ndo maana nataka nibadilike na mtu unaweza kubadilika pale ambapo umeona wenzako wanavyoishi kwa raha na fraha na familia zao. Ni yangu ndo maana nasema kama huamini nitembelee home. I am so oepn to everyone who will make me change for the better.
 
mmmmh!kwa hiyo na mama yao atakuwa mkeo wa pili?Naamanisha uta mhalalisha?

Kwa vile ni mke wa mtu, makubaliano hayakuwa kwamba nitamchukua na lahasha sio lengo langu. Hapa tunazungumzia suala la watoto "to legitimise them" ili wanitambue kwamba mimi ndo baba yao na watumie jina langu la Wiyelele
 
Wiyelele punguza porojo; njoo na hoja za kusaidia sisi member of JF kujikwamua kiuchumi
 
Last edited by a moderator:
Wiyelele punguza porojo; njoo na hoja za kusaidia sisi member of JF kujikwamua kiuchumi

Asante sana, mwenye kushiba hajui njaa! Waambie JF waondoe hii area ya Mahusiano ili sisi wenye shida twende Mahakamani au kanisani na huko jamii ikatushangae. Hapa tunapunguza hasira tulizonazo kwa kupata ushauri mbalimbali. Kama unaboreka, ruka juu nenda zako
 
Ndugu, kweli mwenzenu ni na shida na sijui zitaishaje. Juzi tu nilikuwa na tatizo la mke wangu na bado halijakwisha. Likaja hili la GF wangu wa zamani. Lakini, ninao watoto wawili nje ya ndoa kutoka kwa rafiki wa mke wangu. Mmoja ni mtoto wa kike (7 yrs) na mwingine wa kiume (4yrs). Rafiki wa mke wangu ambaye bado ana urafiki na mke wangu, alinililia sana baada ya kukaa miaka 2 bila kupata watoto kwamba wasingeweza kupata mtoto. Baada ya kudhibitika kwamba yeye hakuwa na tatizo la kupata watoto na mme wake ndo mwenye matatizo, aliniomba nizae nae watoto. Mimi niliyaweka kwenye maandishi na yeye akakubali kutia sahihi. Watoto hawa ni wazuri na wana afya njema, jamaa hajui lolote na anawapenda sana watoto hawa. Lakini ili niweze kuwalea watoto wangu vizuri, nimeona sasa wakati umefika niwachukue watoto wangu kwa vile tayali ninaushahidi wa kutosha kwamba ni wangu vikiwepo na vipimo vya vinasaba.

Lakini wasiwasi wangu ni kwamba yule ni mke halali wa mtu! Kisheria, japo sio kosa la jinai kuzaa na mke wa mtu, ni kosa la kawaida ambapo naweza kulipa fidia kubwa sana na pengine kutenganisha hata ndoa yao. Mke anataka nimpatie mtoto wa tatu kutokana na mme wake kuhitaji mtoto wa tatu. Sasa nifanyeje jamani? Nisaidie jamani nifanyeje? Mi nataka watoto wangu na sitaki tena kumpatia mtoto mwingine.

tutalalamika sana ktk nyanja nyingi ila ttz ni u dot com. je wafikir haya mambo hayakuwepo kipindi cha wazee wetu? ni siri tu ndio iliyowasaidia na kutufikisha ktk maisha mazuri ya sasa. sasa ww dot com unataka tujadili habari nzito kama hiyo ndani ya JF!!! toka zako
 
tutalalamika sana ktk nyanja nyingi ila ttz ni u dot com. je wafikir haya mambo hayakuwepo kipindi cha wazee wetu? ni siri tu ndio iliyowasaidia na kutufikisha ktk maisha mazuri ya sasa. sasa ww dot com unataka tujadili habari nzito kama hiyo ndani ya JF!!! toka zako

Hii forum sio ya wazee peke yao! mimi sio kijana, nina hao watoto zangu wana umri sawa na mtoto wako wa kwanza! Kama unaona kwamba huwezi kuijadili hapa, ishia zako na ukifika nyumbani kwako, ondoa TV sebuleni.
 
Ushahidi wa vinasaba unao kweli?? Maana nasikia ili kufika huko kwenye vinasaba (DNA) ni lazima kuwe na kamgogoro kuhusu mzazi halisi wa mtoto/mtoto kamgogoro ambako kimsingi kanatakiwa kuwa kamesajiliwa rasmi katika mamlaka husika au kwa wakili....

Sasa ikiwa ni hivyo uliwezaje kuanzisha kamgogoro hako kalikopelekea ukaenda kupata uhakika wa kuwa watoto ni wa kwako? Hili swali namba moja,

Swali nambari mbili ni Je, alikuhakikishiaje kwamba mumewe ndiye mwenye tatizo na bado ulipompatia zawadi ya ujauzito mume akaupokea na kulea watoto wakati akijijua ana tatizo na hawezi kurutubisha yai la mwanamke?

Msingi wa swali la pili ni kutokana na maelezo yako kwamba mwanamke huyo alikwambia kwamba mumewe ndiye mwenye tatizo, ina maana walienda wote (mke na mume) kupima na wakaambiwa mume ndiye mwenye tatizo?

Swali la mwisho inawezekanaje uzae na rafiki wa mkeo tena watoto wawili "wazuri wenye afya njema" halafu bado unaombwa msaada wa mbegu kwa ajili ya mtoto wa tatu bado mkeo hagundui tuuu, jamani......
 
unataka uchukue watoto wako, hapo hapo unataka kutoa mbegu ya tatu??
Mbegu za maharagwe bwana, hazina shida
 
Asante sana, mwenye kushiba hajui njaa! Waambie JF waondoe hii area ya Mahusiano ili sisi wenye shida twende Mahakamani au kanisani na huko jamii ikatushangae. Hapa tunapunguza hasira tulizonazo kwa kupata ushauri mbalimbali. Kama unaboreka, ruka juu nenda zako
Wiyelele kweli mwanaume mwenye akili timamu unaweza kufanya mkataba wa kuzini na mke wa mtu? Nadhani kuna haja ya kuruhusu zile mahakama za kadhi ziondoe kadhia kama hii ya kwako kwa kubondwa na mawe mpaka wote wawili mfe
 
Last edited by a moderator:
nivea wll i need is your help. Nataka niondokane na haya matatizo maana yamenisumbua kwa uda mrefu. Nakata niwe mpya niingiapo 2013 Mungu akipenda.
if only u need peace in this world maana hata ndugu zako wa damu kbisa hawatakuelewa nakwambia .itazua mtafaruku wa kufa mtu .soits better to kama mlivyoweza kufanya siri ya miaka zaidi ya 7 na kweli haikuvuja ppte.basi na iwe hivo mpaka kufa never mention this as long as watoto wanaishi vizuri kabisa ,kuna movie moja kama hili tukio lako jamaa alisingiziwa hivohivo ila kufika mahakamani wale watoto walimkana real father na mahakama kuamuru waendelee kuishi na huyo bb aliyewalea .tulia kimya na mkeo msomi .lol hivi amejirekebisha ?
 
unataka uchukue watoto wako, hapo hapo unataka kutoa mbegu ya tatu??
Mbegu za maharagwe bwana, hazina shida

Hujanielewa kabisa! Mimi sihitaji mtoto wa tatu kwa vile inaniumiza. What i need ni watoto wangu tu.
 
Wiyelele kweli mwanaume mwenye akili timamu unaweza kufanya mkataba wa kuzini na mke wa mtu? Nadhani kuna haja ya kuruhusu zile mahakama za kadhi ziondoe kadhia kama hii ya kwako kwa kubondwa na mawe mpaka wote wawili mfe

Jamani huu sio mkataba wa kuzini! Hizo Mahakama za Kadhi hata zikija, their jurisdiction will only be limited to people of the Muslim Sect only. Kwa maana hiyo kwangu hazitanikamata. Huoni kwamba nilileta neema kwenye familia?
 
if only u need peace in this world maana hata ndugu zako wa damu kbisa hawatakuelewa nakwambia .itazua mtafaruku wa kufa mtu .soits better to kama mlivyoweza kufanya siri ya miaka zaidi ya 7 na kweli haikuvuja ppte.basi na iwe hivo mpaka kufa never mention this as long as watoto wanaishi vizuri kabisa ,kuna movie moja kama hili tukio lako jamaa alisingiziwa hivohivo ila kufika mahakamani wale watoto walimkana real father na mahakama kuamuru waendelee kuishi na huyo bb aliyewalea .tulia kimya na mkeo msomi .lol hivi amejirekebisha ?

Je nikidai wanitambue tu ila waendelee kuishi na jamaa? Oh ameanza kujirekebisha kidogo maana si umeambiwa hapa nataka kutubu kabisa?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom