Watoto wa maofisa wa Magereza wafariki kwa kukosa hewa baada ya kufungiwa kwenye gari

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Vilio na simanzi vimetawala Ukonga Magereza kufuatia vifo vya watoto wawili wa maofisa wa Jeshi la Magereza waliofariki dunia kwa kukosa hewa, baada ya kujifungia kwenye gari la mmoja wa wazazi wao walimokuwa wakicheza
Tukio hilo limetokea juzi jioni katika Kota za Magereza Ukonga wakati wazazi wao wakitengeneza gari hilo

Watoto waliopoteza maisha ni mtoto wa Mrakibu wa Jeshi la Magereza (ASP) Demetrus Masala, aitwaye Mariam (6) ambaye alikuwa darasa la kwanza katika shule ya St. Theresa Ukonga na Sajini Francis, ambaye ni Esther (4) Mwanafunzi wa Chekechea

Kwa mujibu wa mashuhuda ambao hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini, Watoto hao walipoteza maisha katika gari lenye namba za usajili T291 CXR aina ya Toyota Passo, mali ya ASP Masala

Imedaiwa kuwa siku ya tukio gari hilo liligoma kuwaka na ndipo Masala alipokwenda kumuomba jirani yake Francis anayeishi chumba cha pili aje amsaidie kuliwasha. Francis ambaye ni dereva katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, walishirikiana na Masala kuliwasha gari hilo kwa muda mrefu lakini hata hivyo lilishindikana kuwaka

Wakati wazazi hao wakiendelea kulitengeneza gari hilo ndipo watoto hao waliposogelea. Hata hivyo, waliwafukuza lakini kumbe watoto hao waliingia kwenye gari bila wao kufahamu kwa sababu gari hilo lilikuwa na vioo vya giza(Tinted).

Alisema baada ya kushindikana, ndipo Francis alipomwelekeza mwenzake kwa fundi ambaye angeweza kulitengeneza gari hilo
"Kutokana na ushauri huo, Masala aliamua kulifunga gari lake na kuondoka kumfuata fundi bila kufahamu kama watoto wameingia ndani ya gari", kilisema chanzo hicho

Ilidaiwa baada ya kukaa kwa muda mrefu Francis, alibaini watoto hao wawili hawaonekani na ndipo walipoanza kuwatafuta bila mafanikio. Wakati wakiendelea kuwatafuta, kuna kijana akawadokeza kuwa wakati gari hilo likiendelea kutengenezwa, Watoto hao walikuwa ndani ya gari yake

Kauli hiyo inadaiwa ndiyo iliyomshtua Francis na kuamua kuchungulia ndani ya gari hilo ambapo alibaini watoto hao wakiwa wamekaa kiti cha nyuma wamelala fofofo, huku mwingine akivuja damu puani.
Hali hiyo ilisababisha Francis na wengine waliokuwepo eneo hilo kusogea na kuvunja kioo cha gari na kuwatoa watoto hao wakiwa katika hali mbaya

Inadaiwa kuwa kwasababu ya hali hiyo waliyokuwa nayo, waliamua kuwawahisha katika Hospitali ya Kardinali Rugambwa iliyoko Ukonga kwa ajili ya matibabu ya haraka, lakini hata hivyo walibaini mtoto Mariam tayari amefariki dunia

Madaktari walijaribu kumpa huduma ya kwanza mtoto Esther kwa kumwongezea Oksijeni na baadaye walimpeleka katika Hospitali ya Amana iliyoko Ilala na kubaini tayari naye amekufa.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa wa Mwembe Madafu, Deus Nchimbi, alisema kifo cha watoto hao ni pigo kwa familia hizo marafiki.
"Kikubwa ni kuomba amani na kuwaomba marehemu lakini watoto wamekufa kifo cha uchungu kwa kukosa hewa huenda wangekuwa wakubwa wangeweza kufungua gari,"alisema Nchimbi

Alisema kilichobaki ni kuikumbusha jamii kuwa makini na vyombo vya moto na kuwapa uhuru watoto waweze kufahamu aina ya mali zilizopo nyumbani.


Chanzo : JamboLeo
 
Duh ajali ni ajali tu lakini nyingine zinauma sana sanaa asikwambie mtu, nimeumia sana maana nimeiona kama vile ndiio wanangu
 
Askari?? Acheni uchochezi.
Yaani mwanausalama kabisa ashindwe kuona hata mtu akiingia kwenye gari yake na yeye akiwa karibu nayo? Ina maana hata mtikisiko wa kuashiria kuna kitu ndani ya gari haukuwepo au hao watoto waliingia wakalala
Hatari sana..kila kifo kina sababu hawa walipangiwa vifo vya hivi,any way tujifariji tu kwamba wamekufa bado wadogo hawakuyakaribia yale mabaya ya dunia.
 
Huo ni uzembe wa hali ya juu sana!

Kama wameshindwa kubaini kama watoto waliingia ndani ya gari watajua kweli waliko jificha majambazi
 
Vilio na simanzi vimetawala Ukonga Magereza kufuatia vifo vya watoto wawili wa maofisa wa Jeshi la Magereza waliofariki dunia kwa kukosa hewa, baada ya kujifungia kwenye gari la mmoja wa wazazi wao walimokuwa wakicheza

Tukio hilo limetokea juzi jioni katika Kota za Magereza Ukonga wakati wazazi wao wakitengeneza gari hilo

Watoto waliopoteza maisha ni mtoto wa Mrakibu wa Jeshi la Magereza (ASP) Demetrus Masala, aitwaye Mariam (6) ambaye alikuwa darasa la kwanza katika shule ya St. Theresa Ukonga na Sajini Francis, ambaye ni Esther (4) Mwanafunzi wa Chekechea

Kwa mujibu wa mashuhuda ambao hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini, Watoto hao walipoteza maisha katika gari lenye namba za usajili T291 CXR aina ya Toyota Passo, mali ya ASP Masala

Imedaiwa kuwa siku ya tukio gari hilo liligoma kuwaka na ndipo Masala alipokwenda kumuomba jirani yake Francis anayeishi chumba cha pili aje amsaidie kuliwasha

Inadaiwa kuwa Francis ambaye ni dereva katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, wakishirikiana na Masala kuliwasha gari hilo kwa muda mrefu lakini hata hivyo lilishindikana kuwaka

Wakati wazazi hao wakiendelea kulitengeneza gari hilo ndipo watoto hao waliposogelea. Hata hivyo, waliwafukuza lakini kumbe watoto hao waliingia kwenye gari bila wao kufahamu kwa sababu gari hilo lilikuwa na vioo vya giza(Tinted).

Alisema baada ya kushindikana, ndipo Francis alipomwelekeza mwenzake kwa fundi ambaye angeweza kulitengeneza gari hilo

"Kutokana na ushauri huo, Masala aliamua kulifunga gari lake na kuondoka kumfuata fundi bila kufahamu kama watoto wameingia ndani ya gari", kilisema chanzo hicho

Ilidaiwa baada ya kukaa kwa muda mrefu Francis, alibaini watoto hao wawili hawaonekani na ndipo walipoanza kuwatafuta bila mafanikio

Inadaiwa kuwa wakati wakiendelea kuwatafuta, kuna kijana akawadokeza kuwa wakati gari hilo likiendelea kutengenezwa, Watoto hao walikuwa ndani ya gari yake

Kauli hiyo inadaiwa ndiyo iliyomshtua Francis na kuamua kuchungulia ndani ya gari hilo ambapo alibaini watoto hao wakiwa wamekaa kiti cha nyuma wamelala fofofo, huku mwingine akivuja damu puani

Hali hiyo ilisababisha Francis na wengine waliokuwepo eneo hilo kusogea na kuvunja kioo cha gari hilo na kuwatoa watoto hao wakiwa katika hali mbaya

Inadaiwa kuwa kwasababu ya hali hiyo waliyokuwa nayo, waliamua kuwawahisha katika Hospitali ya Kardinali Rugambwa iliyoko Ukonga kwa ajili ya matibabu ya haraka, lakini hata hivyo walibaini mtoto Mariam tayari amefariki dunia

Madaktari walijaribu kumpa huduma ya kwanza mtoto Esther kwa kumwongezea Oksjeni na baadaye walimpeleka katika Hospitali ya Amana iliyoko Ilala na kubaini tayari naye amekufa.

Chanzo : JamboLeo
Sawa
 
Ndio tatizo la kulea watoto kwa kuwadekeza.. Siwezi kumwambia mtoto toka hapa usicheze eneo hili alafu aje tena.. Tuache kudekeza watoto, tulee kiafrika..

Ila nawapa pole wazazi waliopoteza watoto
 
Askari?? Acheni uchochezi.
Yaani mwanausalama kabisa ashindwe kuona hata mtu akiingia kwenye gari yake na yeye akiwa karibu nayo? Ina maana hata mtikisiko wa kuashiria kuna kitu ndani ya gari haukuwepo au hao watoto waliingia wakalala

Hebu soma tena usiwe na haraka ya kuhukumu. Askari ni binadamu tu
 
Askari?? Acheni uchochezi.
Yaani mwanausalama kabisa ashindwe kuona hata mtu akiingia kwenye gari yake na yeye akiwa karibu nayo? Ina maana hata mtikisiko wa kuashiria kuna kitu ndani ya gari haukuwepo au hao watoto waliingia wakalala
Vitu vingine sio vya kuleta siasa, au kwavile ni msemachochote? R.I.p watoto
 
Hajitambui huyo achana naye, hajui kuwa ajali inaweza kutokea bila kutarajia
Hongera yenu mnaojitambua.
Ingelikua ni uzi unaohusu askari kulinda mkutano wa ccm na kuvuruga wa cdm nadhani ungesema askari hawako makini na kazi zao, ila kwenye ulinzi wa watoto bila siasa, unaona wako vizuri.

Watz bwana
 
Back
Top Bottom