Watoto kuwa mizigo, wazazi mna mchango hasi

Nsimbi

JF-Expert Member
Sep 27, 2014
1,091
1,202
Ni muhimu sana kuzingatia uzazi wa mpango siku hizi kwani kutokana na kuporomoka kwa maadili, baadhi ya watoto wamekuwa ni mizigo badala ya hazina katika familia.

Watoto hawawezi kuwa tofauti sana na wazazi wao yaani baba na mama. Mchongoma hauwezi kuzaa machungwa na mtoto wa simba si wa chura.

Mtoto aliyetoka kwenye damu ya 'viroba' hawezi kuwa sawa na mtoto wa baba aliyekunywa mbege!!
Kuna wimbo unauliza mdudu ndani koko la embe kaingiaje? Ni wazi mdudu huyo huingia na kuanza kuharibu tunda hilo likiwa katika hatua ya maua. Na mdudu huyo hulifanya embe lioze.

Wanasema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Kama mtoto amedekezwa tangu mdogo atakuwa na tabia mbaya hadi akiwa mkubwa.
Mzazi akiwa mvivu na mtoto atakuwa mvivu tu. Mzazi akiwa na tabia ya kutoa matusi mtoto ataiga.

Wazazi wanakosea sana kufanya mambo ya ovyo mbele ya watoto. Kwa mfano baba kumtukana mkewe au mke kumjibu vibaya baba mbele ya watoto hupanda mbegu mbaya.

Na mzazi akizoea kuvaa mavazi yasiyoendana na maadili it's likely mtoto naye atakuwa akivaa nguo za ajabu ajabu.
Baba ukiwa unavaa mavazi au vitu vya kike mtoto wako wa kiume ataiga tu!

Watoto wengi siku hizi hawana adabu kwa sababu walidekezwa sana na wazazi wao.
Akiitwa na baba au mama yake anavuta mdomo kisa anachatii. Kutwa kwenye tv na kazi hawataki kufanya. Akina mama wengi siku hizi kazi zote wanawaachia house girls.

Matokeo yake ni kwamba watoto hawawezi hata kuosha vyombo, kufagia, kupika au hata kufua nguo zao. Ukweli ni kwamba Watanzania wengi wameanza ku lose control ya watoto wao. Malezi imekuwa kazi ngumu.

Katika baadhi ya familia watoto ndio wanawa control wazazi kwa kufanya wanavyotaka almost with impunity!!

Hakuna kazi wanayofanya watoto wengi siku hizi zaidi ya kuchati kwenye simu na ku bet.

Wazazi wengi wanawalea watoto kama mayai na hawawafundishi stadi za maisha. Inakuwaje mtoto binti wa miaka 15 ashindwe kufua nguo zake au kijana wa miaka 17 ashindwe hata kufyeka majani au kulisha mifugo?

Baadhi ya watoto hasa wavivu na wasio na heshima ni mizigo kwa wazazi wao, jamii na taifa kwa ujumla.

Wengi wanasingizia kuwa busy na masomo lakini hii si kweli kwani wanafunzi wengi hawazingatii shule na ikifika wakati wa mitihani baadhi ya wazazi wao huhangaika 'kununua' mitihani.

Wazazi wanachangia nchi kutengeneza kizazi cha watu wanaotaka njia za mkato kimaisha. Wazazi waongeze ukali kidogo kwa watoto wao vinginevyo wanawapoteza.

Wawafundishe kufanya kazi, mila na desturi nzuri, adabu kwa wakubwa na upendo kwa binadamu wote.

Watoto wapunguze kuchati kwenye simu na ikiwezekana wazazi msiwanunulie vijana wenu cm. Wengi wanaangalia mambo ya ovyo yanayozidi kuwapumbaza.

Cm na mitandao inaharibu vijana wetu na wazazi tusipoziba ufa.........
 
....tutajenga ukuta,.ili Taifa liwe imara lazima misingi bora na imara ijengwe kuanzia kwenye ngazi ya familia,..familia mbovu ndiyo inayozaa jamii na Taifa bovu vilele,.wazazi,walezi wenyewe kutwa tunapigana vikumbo na vijembe mitandaoni SAA ngapi utaangalia mustakabali wa watoto?..ndoa zitadumu?kazi zitafanyika kwa ufasaha?watoto watakuwa kwenye maadili ya kupendeza SAA ngapi wakati na wao wako gugo,IG,fb,wanajifunza namna dunia imavyoenda hawana mwalimu kiongozi wafanyaje sasa??....kuna mambo lazima tukubali kuyafanya kwa kiasi kuepusha lawama ambazo mwisho wa siku sisi wenyewe ndio chanzo,.

"Mchuma janga siku zote hula na wakwao" kila MTU asimame kwenye nafasi yake.
 
Inawezekana ila siku hizi unaweza lea mtoto vizuri ila makundi katika shule na vyuo ndiko wanakoharibikia sana sana yaani nimeshuhudia mtu analelewa fresh akifika chuoni anaanza kucopy mambo ya ajabu kutokana na marafiki zake mfano kunywa pombe, kutumia bangi na unga kutafuta mabwana wenye pesa ( ingawa kwao wanapesa na anatumiwa za kumtosheleza) yaani kwa mifano hai nimeshuhudia
Muhimu ni kujua rafiki za watoto wako ni kina nani
 
Umeongea vyema sana "... majority ya vijana wengi huwa wanaharibika kutokana na mifumo hasi ya malezi waliyopitia toka kwa wazazi/walezi wao "... kuna haja ya dhati " tukiwa kama jamii ya wazazi kujitathmini " ili tuweze kubaki kwenye misingi chanya inayo chochea uadilifu " hii itachangia kutusaidia wazazi kuweza kuvuna mazao bora yatakayo tokana na mbegu hii bora tuliyo ipanda kwenye ardhi yenye rutiba iliyokuwa haija nyimwa maji na pembejeo (malezi bora) ....

lakini pia ni vyema sana vijana nao wakawa wanajifunza mambo mbali mbali ambayo yanatija toka kwa watu wanao wazunguka katika Jamii Yao " hii itawapa motisha/hamasa/morali Ya kuweza kuwa na kiu ya mafanikio ya namna yoyote" ile ( ifahamike kuwa hata Kuwa na busara/hekima ni sehemu ya mafanikio ambayo yamewashinda wapumbavu). Mtu kama cristiano ronaldo hana history nzuri alipo kuwa utotoni " Baba yake mzazi alikuwa ni moja ya walevi maarufu katika Mji wanao ishi ".. hatimae baba Yake alikuja kufa kwa maradhi yaliyo sababishwa na ulevi ".... lakini hiyo haikuwahi kuwa excuse kwa Christiano kuweza kusababisha ashindwe kuishi maisha ya ndoto yake "... haikuwa excuse ya kumfanya ashindwe kuwa miongoni mwa ma- icon wa football player " duniani ...

by the way role model wa kwanza kwa mtoto/watoto ni wazazi/walezi ndugu " jamaa kisha Jamii inayo mzunguka" wazazi ama walezi tunapaswa kuwa na ustadi bora na ustaarabu bora " unaopaswa kuigwa na vizazi vyetu mpaka kwa Jamii nzima inayo ambatana nasi



KARIBUNI TUJADILI
 
....tutajenga ukuta,.ili Taifa liwe imara lazima misingi bora na imara ijengwe kuanzia kwenye ngazi ya familia,..familia mbovu ndiyo inayozaa jamii na Taifa bovu vilele,.wazazi,walezi wenyewe kutwa tunapigana vikumbo na vijembe mitandaoni SAA ngapi utaangalia mustakabali wa watoto?..ndoa zitadumu?kazi zitafanyika kwa ufasaha?watoto watakuwa kwenye maadili ya kupendeza SAA ngapi wakati na wao wako gugo,IG,fb,wanajifunza namna dunia imavyoenda hawana mwalimu kiongozi wafanyaje sasa??....kuna mambo lazima tukubali kuyafanya kwa kiasi kuepusha lawama ambazo mwisho wa siku sisi wenyewe ndio chanzo,.

"Mchuma janga siku zote hula na wakwao" kila MTU asimame kwenye nafasi yake.

Bingo ... woooww
 
Akina mama hakikisheni watoto wenu wanafanya kazi zote za nyumbani. Asiachiwe house girl tu. Mtoto anashindwa hata kutoa vyombo mezani?! Mambo gani haya!
 
Binti yangu wa miaka akimaliza kula ananishukuru, kaka yake wa miaka minne akimaliza kula anashukuru watu wote, kisha anatoa vyombo. Ole wake kipasuke hata kimoja, namuomba Mungu awaongoze mwenyewe!
 
Inawezekana ila siku hizi unaweza lea mtoto vizuri ila makundi katika shule na vyuo ndiko wanakoharibikia sana sana yaani nimeshuhudia mtu analelewa fresh akifika chuoni anaanza kucopy mambo ya ajabu kutokana na marafiki zake mfano kunywa pombe, kutumia bangi na unga kutafuta mabwana wenye pesa ( ingawa kwao wanapesa na anatumiwa za kumtosheleza) yaani kwa mifano hai nimeshuhudia
Muhimu ni kujua rafiki za watoto wako ni kina nani
Umeongea point mkuu .
Ila nadhani mtoto akishakuwa na misingi imara kuanzia chini hata swala la kufata mikumbo hull mavyuoni halitakuwepo .

Misingi imara ni pamoja na kujiamini .
Wazazi mjitahidi kuwajengea watoto wenu kujiamini wenyewe .
 
Binti yangu wa miaka akimaliza kula ananishukuru, kaka yake wa miaka minne akimaliza kula anashukuru watu wote, kisha anatoa vyombo. Ole wake kipasuke hata kimoja, namuomba Mungu awaongoze mwenyewe!

Kazi kulea

Safi sana. Kuwapenda watoto ni pamoja na kuwafundisha adabu na tabia njema pamoja na 'kuwachapa' wanapokosea.

Kuwarudi wanapokosea ni sehemu ya malezi. Unajua kuna tofauti kati ya kulea na kutunza. Kutunza ni kuwapatia watoto chakula, malazi, nguo, vifaa vya shule nk.

Kulea ni kumfundisha mtoto tabia njema na hivyo kumuandaa kuwa mke/mume bora hapo baadae n above all, kuwa raia mwema.

Kila unapomwadhibu au kumkanya mtoto kuhusu jambo lolote baadae mwambie kwa upendo kwa nini umemwadhibu! Atakuelewa tu.

Off course the rest tunamwachia Mwenyezi Mungu lakini mzazi please timiza wajibu wako kwani wewe ndio mwalimu Na 1 wa mtoto.

Always avoid portraying any bad examples before the child. Na kama ukifanya ujinga wowote mbele yake kwa bahati mbaya, tafuta muda wa kumfafanulia na ikibidi muombe radhi.

Wanasema kazi sio kuzaa. Kazi kulea!!!! ( Hawajasema kazi kutunza!!!!! 😀)
 
Back
Top Bottom