Watoto huongea na kusikia toka wakiwa tumboni...Tuwasemeshe na kuwakaribisha kabla hawajazaliwa

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,816
image.jpeg


image.jpeg


Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya "Upendo" wa Wazazi na "Uono"(Sight).Ndio maana wazungu walisema "Out of Sight,Out of Mind".

Hata kama leo mzazi/wazazi watakutana na mtoto wao baada ya miaka 10 toka waachane akiwa mdogo, hakutakuwa na ile "bondism" ya Mzazi/Wazazi na watoto,sbb kile kipindi cha kutengeneza hiyo "bondism" kilishapita.

Hii kwa wale wafuatiliaji wa mpira watakuwa wameiona kwa Mario Baloteli(Mchezaji mpira na raia wa Italia mwenye asili ya Ghana),wazazi wake Mario,ambao ni raia wa Ghana walimpa Mzee Baloteli raia wa Italia kumlea Mario akiwa bado mtoto mdogo sana kwa sababu za ugonjwa wa mtoto wao,kiasi Mario ana upendo wa kweli kwa baba wa kufikia kuliko kwa "Biological Parents" wake.Mario hujiona ni wa familia ya Balloteli kuliko ile ya kwake ya asili ya Ghana,hata alipofika umri wa kuchagua team ya Taifa ya kuchezea,aliamua Italia ingawa alikuwa na nafasi ya kuchagua Ghana.

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kukutana na jamaa aliyelelewa na Watawa wa Kikatoliki huko Itigi-Singida,baada ya Wazazi wake kuwa na umasikini kiasi alikuwa na utapiamlo,alikuja kuwaona Wazazi akiwa na mkubwa mwenye akili,akaelewa kuwa wale ni wazazi wake,lakini sababu hakuwa anakaa nao wala kulelewa nao,hakukuwa na "mshikamano" wa kihisia wa moja kwa moja.Siku alipokufa mmoja wa Wazazi wake,hakulia kama alivyolia na kugalagala siku aliyokufa Mtawa aliyemlea.

Na sisi tukumbuke kujinyima na kufanya lolote kwa ajili ya kuwekeza kwa watoto...Hujawahi kwenda kwenye msiba wa mzazi wa mwenzako na ukakuta mtoto ana-behave kama aliyefariki ni jirani na si mzazi??Ni kwa sbb wakati wa umri wa "bondism",ile bond haikushikamana vilivyo.

Vijana wengi sasa wanazaa na mabinti na kuwa mbali nao,wanatuma matumizi tu ya mtoto,hatengenezi "mshikamano" wa kihisia kati yake yeye na mtoto,anafikiri kwa kutuma tu pesa za matunzo,basi ndio wajibu na jukumu la mzazi.

Haya hata kwenye jamii tunayaona,wapo wanaomlaumu mwanamuziki Diamond katika mahusiano na baba yake,wapo waliomsema Mh.Hamis Kigwangala na baba yake,watu walimshangaa mahusiano ya marehemu Kanumba na baba yake.Haya yote yanasema kitu juu ya umri wa "bondism"

"Bond" inaanzia tumboni,unaweza kutenga kila siku asubuhi uamkapo,na jioni ulalapo ukawa unashika tumbo la Mama na kumwambia mtoto maneno ya heri,ukimwambia kuwa unamsubiri kwa hamu aje,unamfurahia kama zawadi na huku ukimsisitiza akuombee heri upate riziki ya kuja kumtunza vyema.


Siku akizaliwa,angali mchanga,unachukua faragha naye na kuongea naye kuwa wewe ni mzazi wake,unamtakia maisha mema ktk dunia,unamtakia heri na afya ili akikua akukute na uone utu uzima wake.Yaani unamsemesha kama vile ni mtu mzima.Hii inakuwa ni "Spiritual Bonding"....Sababu ni mawasiliano ya kiroho kati ya wewe na mtoto.

Baadaye ndani ya miaka 02-06 unaanza kujenga taswira yako ktk ubongo wa mtoto,ndio pale anaanza kukuita baba bila yeye kujua alianzaje kukuita baba.

Miaka 06 -16 ndio haswaa "physical bond" inaimalika.Hapa mtoto anaona kama ni Mama basi anaona ule Umama wako,kama ni baba basi anaona ule ubaba wako,ana-feel ile protection,akipigwa na wenzake anatoka mbio anakuja kusema baba nimepigwa na huyu,kama ni kwa Mama basi anaenda kusema Mama hapa panawasha nikune.

Hii ya Baba nimepigwa inakuja kwako sbb anaanza kujifunza "sense of protectionism" hutoka kwa baba,anasema Mama hapa nimeumia au hapa panawasha,sbb tayari amejifunza kuwa "sense of Sympathy(?) and Care" hutoka kwa Mama.

Ndio maana unaona mara nyingi mtoto akitaka pesa ya kununulia vibama anaenda kwa Mama,lakini hela ya daftari au kalamu anamwambia Baba.Hapo ubongo wa mtoto umekuwa na kujua nani ni nani...!!Ile "Masculine" na "Feminine" iliyo ndani ya baba na Mama inaanza kumkaa na kumjenga.

Wapo "anthropologist" wanaoamini hata hizi "ultrasound" wanazofanya vijana wa siku hizi kujua jinsia ya mtoto kabla ya kuzaliwa,inapunguza "mshikamano" kazi ya mzazi na mtoto.Unaweza kukuta mmoja wao alipenda wafungue uzazi na mtoto wa kike,anapoonekana wa kiume,mtu ananyong'onyea kihisia,sababu hayakuwa matarajio yake.Hali ile ya kutokuridhika humfikia mtoto.Tena kwa mama mwenye mtoto tumboni,ujumbe hufika moja kwa moja,kiasi mtoto hujua kuwa Mama hajafurai jinsi yake.Hii hupunguza "Spiritual bondism" kati ya Mama/mzazi na mtoto tumboni.

Ni somo-asili refu sana...Ambalo sisi tuliozaliwa na Wazee wa 1920's hatukulipata sana,ila sisi tunapaswa kuwapa upendo huu watoto wetu,iwe wa kike au kiume.Tuwe marafiki na watoto wetu,kuna mambo "We have to talk" na watoto wetu,na kuna mambo "We have to ask" ....Siku ya mauti,watulilie kwa uchungu unaosindikizwa na chozi lenye heri,baraka na sala mbele za Mungu.
 
Unamaanisha huyu single mum niachane nae kwakua sikukaribisha mtoto?
 
Nzuri sana. Kizazi hiki kinatengeneza kizazi cha C & P, hiyo hali ilishapotea kwa hao tuowaiga. Maisha ya kisasa na ya wenye vipato vya juu ni typically maigizo kwakuwa wamepata exposure na access ya kuona weupe wanaishije.

Kuna mweupe mmoja aliwahi niambia, katika maisha yake yajayo atapenda azaliwe TZ ili afaidi ile BOND ya mama na mtoto aliyoiona hapa, jinsi mama anavyombeba mwana tangu akiwa mdogo, jinsi anavyomnyonyesha, n.k

Wenye exposure na vipato vikubwa siku hizi wana mashine za kukamua maziwa ya mama na kuhifadhi kwenye friji kwaajili ya kumnywesha mtoto siku za usoni.

Usomi umetupa uwezo wa KUIGA bila kufikiri!
 
Mkuu daaah nice word with strong meseji je katika apllicability tunaweza na haya maisha ye2 ya kukimbizana alfajir umetoka unarud late hrs weekend ndio hvyoo mambo miamia
 
mkuu huu ukweli mkubwa sana.
nakumbuka kuna mzazi mmoja alikufa sikutoa hata chozi, hadi nikawa nalazimishwa alafu nilikiwa katoto kadogo shule ya msingi.

wazazi muelewe ukweli huu.
ubarikiwe mkuu barafu...
 
View attachment 631198

View attachment 631199

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya "Upendo" wa Wazazi na "Uono"(Sight).Ndio maana wazungu walisema "Out of Sight,Out of Mind".

Hata kama leo mzazi/wazazi watakutana na mtoto wao baada ya miaka 10 toka waachane akiwa mdogo, hakutakuwa na ile "bondism" ya Mzazi/Wazazi na watoto,sbb kile kipindi cha kutengeneza hiyo "bondism" kilishapita.

Hii kwa wale wafuatiliaji wa mpira watakuwa wameiona kwa Mario Baloteli(Mchezaji mpira na raia wa Italia mwenye asili ya Ghana),wazazi wake Mario,ambao ni raia wa Ghana walimpa Mzee Baloteli raia wa Italia kumlea Mario akiwa bado mtoto mdogo sana kwa sababu za ugonjwa wa mtoto wao,kiasi Mario ana upendo wa kweli kwa baba wa kufikia kuliko kwa "Biological Parents" wake.Mario hujiona ni wa familia ya Balloteli kuliko ile ya kwake ya asili ya Ghana,hata alipofika umri wa kuchagua team ya Taifa ya kuchezea,aliamua Italia ingawa alikuwa na nafasi ya kuchagua Ghana.

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kukutana na jamaa aliyelelewa na Watawa wa Kikatoliki huko Itigi-Singida,baada ya Wazazi wake kuwa na umasikini kiasi alikuwa na utapiamlo,alikuja kuwaona Wazazi akiwa na mkubwa mwenye akili,akaelewa kuwa wale ni wazazi wake,lakini sababu hakuwa anakaa nao wala kulelewa nao,hakukuwa na "mshikamano" wa kihisia wa moja kwa moja.Siku alipokufa mmoja wa Wazazi wake,hakulia kama alivyolia na kugalagala siku aliyokufa Mtawa aliyemlea.

Na sisi tukumbuke kujinyima na kufanya lolote kwa ajili ya kuwekeza kwa watoto...Hujawahi kwenda kwenye msiba wa mzazi wa mwenzako na ukakuta mtoto ana-behave kama aliyefariki ni jirani na si mzazi??Ni kwa sbb wakati wa umri wa "bondism",ile bond haikushikamana vilivyo.

Vijana wengi sasa wanazaa na mabinti na kuwa mbali nao,wanatuma matumizi tu ya mtoto,hatengenezi "mshikamano" wa kihisia kati yake yeye na mtoto,anafikiri kwa kutuma tu pesa za matunzo,basi ndio wajibu na jukumu la mzazi.

Haya hata kwenye jamii tunayaona,wapo wanaomlaumu mwanamuziki Diamond katika mahusiano na baba yake,wapo waliomsema Mh.Hamis Kigwangala na baba yake,watu walimshangaa mahusiano ya marehemu Kanumba na baba yake.Haya yote yanasema kitu juu ya umri wa "bondism"

"Bond" inaanzia tumboni,unaweza kutenga kila siku asubuhi uamkapo,na jioni ulalapo ukawa unashika tumbo la Mama na kumwambia mtoto maneno ya heri,ukimwambia kuwa unamsubiri kwa hamu aje,unamfurahia kama zawadi na huku ukimsisitiza akuombee heri upate riziki ya kuja kumtunza vyema.


Siku akizaliwa,angali mchanga,unachukua faragha naye na kuongea naye kuwa wewe ni mzazi wake,unamtakia maisha mema ktk dunia,unamtakia heri na afya ili akikua akukute na uone utu uzima wake.Yaani unamsemesha kama vile ni mtu mzima.Hii inakuwa ni "Spiritual Bonding"....Sababu ni mawasiliano ya kiroho kati ya wewe na mtoto.

Baadaye ndani ya miaka 02-06 unaanza kujenga taswira yako ktk ubongo wa mtoto,ndio pale anaanza kukuita baba bila yeye kujua alianzaje kukuita baba.

Miaka 06 -16 ndio haswaa "physical bond" inaimalika.Hapa mtoto anaona kama ni Mama basi anaona ule Umama wako,kama ni baba basi anaona ule ubaba wako,ana-feel ile protection,akipigwa na wenzake anatoka mbio anakuja kusema baba nimepigwa na huyu,kama ni kwa Mama basi anaenda kusema Mama hapa panawasha nikune.

Hii ya Baba nimepigwa inakuja kwako sbb anaanza kujifunza "sense of protectionism" hutoka kwa baba,anasema Mama hapa nimeumia au hapa panawasha,sbb tayari amejifunza kuwa "sense of Sympathy(?) and Care" hutoka kwa Mama.

Ndio maana unaona mara nyingi mtoto akitaka pesa ya kununulia vibama anaenda kwa Mama,lakini hela ya daftari au kalamu anamwambia Baba.Hapo ubongo wa mtoto umekuwa na kujua nani ni nani...!!Ile "Masculine" na "Feminine" iliyo ndani ya baba na Mama inaanza kumkaa na kumjenga.

Wapo "anthropologist" wanaoamini hata hizi "ultrasound" wanazofanya vijana wa siku hizi kujua jinsia ya mtoto kabla ya kuzaliwa,inapunguza "mshikamano" kazi ya mzazi na mtoto.Unaweza kukuta mmoja wao alipenda wafungue uzazi na mtoto wa kike,anapoonekana wa kiume,mtu ananyong'onyea kihisia,sababu hayakuwa matarajio yake.Hali ile ya kutokuridhika humfikia mtoto.Tena kwa mama mwenye mtoto tumboni,ujumbe hufika moja kwa moja,kiasi mtoto hujua kuwa Mama hajafurai jinsi yake.Hii hupunguza "Spiritual bondism" kati ya Mama/mzazi na mtoto tumboni.

Ni somo-asili refu sana...Ambalo sisi tuliozaliwa na Wazee wa 1920's hatukulipata sana,ila sisi tunapaswa kuwapa upendo huu watoto wetu,iwe wa kike au kiume.Tuwe marafiki na watoto wetu,kuna mambo "We have to talk" na watoto wetu,na kuna mambo "We have to ask" ....Siku ya mauti,watulilie kwa uchungu unaosindikizwa na chozi lenye heri,baraka na sala mbele za Mungu.

Somo zuri sana, msimu ujao ntakuwa karbu zaidi.
Shukrani Mkuu ubarikiwe
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom