Watoto 5 na watu wazima 4 hufa kila siku Hospitali ya Musoma

Mugishagwe

JF-Expert Member
Apr 28, 2006
300
58
Nakuja na habari hii ambayo inasikitisha sana lakini chanzo chake ni uongozi mbaya na rushwa kutawala Musoma na kulindana kuanzia Mkoani hadi Wizarani.

Ndugu zangu, nimekuwa katika hospitali hii kwa muda wa wiki moja sasa, nimekuwa nashuhudia watoto wanakufa kwa wingi, ama wakiwa mapokezi ama wodini, kwa idadi ya wastani ya watoto 5 na watu wazima 4. Leo pekee nimeshuhudia Mwalimu mmoja wa shule moja hapa Musoma anakufa, na maiti yake kubebwa na ndugu zake kupelekwa Mortuary, na wagonjwa wengine ambao sikupata taarifa zao.

Hospitali ya Mkoa wa Mara inaongoza kwa rushwa na uongozi mbovu ambao unakumbatiwa na Mkubwa mmoja Wizarani na Acting Katibu Tawala wa Mkoa huu anaitwa Mulemwa. Inasemekana kuna Dkt. Muniko ambaye yeye ameshindikana kuondoka, na yeye ni Mganga mfawidhi hapa. Rushwa kwake ni sehemu ya maisha yake, na huhamishia madawa katika hospitali iliyopo Mtaa wa Iringo hapa Musoma iitwayo Manga.

Huhamisha wagonjwa na kuwapeleka kwake kwa consultation pekee ni Tshs 5000 na huu ni mradi wake. Mganga Mkuu ndugu Bangi yupo tu, na inasemekana naungana na wenyeji kula mlungula bila ya wasiwasi. Nimeshuhudia matukio madhaa ambayo hata Nurse alifikia kutamka kwamba wao ma Nurse na ma daktari wao siri ni moja na hakuna wa kuwafanya lolote.

PCCB ya Hosea hapa Musoma ina ubia na hawa wakubwa, hakuna lolote wafanyalo maana wao huingia hapo na kulambishwa.

Kuna mengi ya kueleza hapa, lakini baada ya hapa juu nadhani kama kuna mtu ana access na Wizara ya Afya, basi anitafute chemba anipe info zaidi ili niende Dar kuelezea hali ilivyo, maana hata mimi nimeombwa rushwa kwa uwazi, ikabidi nimwite Mganga Mkuu na kumuuliza uhalali ule. Hakuna risiti baada ya malipo, na pia kila Nurse huomba rushwa wazi wazi, maana wanajua ubaya wa Uongozi, kwa kuwa wote wanakula na hakuna wa kumfukuza mwenzake. Vifo Musoma vinatawala, maana kama huna pesa kwanza, basi utawekwa hadi pesa ije. Hata kupata shule inakubidi kulipa 2000 na kusukuma mgonjwa pia malipo achilia mbali adha za ndani ya wodi.

Wenyeji wanasema kwamba ukitaka kuijua Musoma, fika Wodi ya watoto na namba 6 huko, utajua taabu zaidi.

Nimechukua hatua. Je, nianzie wapi, maana Wizarani Dkt. Muniko ana mtu wake na kuondoka Musoma imekuwa ngoma. Watu wanakueleza kwamba Muniko na Meneja wa Uwanja wa Karume hapa Musoma hawawezi kuondolewa na wana mizizi minene. Je, Prof. Mwakyusa, haya ndiyo maisha bora kwa wananchi wa Mkoa wa Mara, hasa kwenye huduma?

Muniko hata haki za watumishi anazima na vifaa vya hospitali, ikiwamo TV nk anahamishia kwake. Marupurupu Musoma ni ndoto, na ukichonga mbele Muniko unaondolewa kama Mbwa mwizi.
 
Nakuja na habari hii ambayo inasikitisha sana lakini chanzo chake ni uongozi mbaya na rushwa kutawala Musoma na kulindana kuanzia Mkoani hadi Wizarani.
Ndugu zangu nimekuwa katika hospitali hii kwa muda wa wiki moja sasa nimekuwa nashuhudia watoto wanakufa kwa wingi ama wakiwa mapokezi ama wodini kwa idadi ya wastani ya watoto 5 na watu wazima 4.Leo pekee nimeshuhudia Mwalimu mmoja wa shule moja hapa Musoma anakufa na maiti yake kubebwa na nduguze kupelekwa Mortuary na wagonjwa wengine ambao sikupata taarifa zao .

Hospitali ya Mkoa wa Mara inaongoza kwa rushwa na uongozi mbovu ambao unakumbatiwa na Mkubwa mmoja Wizarani na Acting Katibu Tawala wa Mkoa huu anaitwa Mulemwa. Inasemekana kuna Dr.Muniko ambaye yeye ameshindikana kuondoka na yeye ni Mganga mfawidhi hapa.Rushwa kwake ni sehemu ya maisha yake , na huhamishia madawa katika hospitali iliyopo Mtaa wa Iringo hapa Musoma iitwayo Manga .

Huhamisha wagongwa na kuwapeleka kwake kwa consultation pekee ni Tshs 5000 na huu ni mradi wake . Mganga Mkuu ndugu Bangi yupo yupo tu na inasemekana naungana na wenyeji kula mlungula bila ya wasi wasi . Nimeshuhudia matukio madhaa ambayo hata Nurse alifikia kutamka kwamba wao ma Nurse na ma dokta wao siri ni moja na hakuna wa kuwafanya lolote .

PCCB ya Hosea hapa Musoma ina ubia na hawa wakubwa hakuna lolote wafanyalo maana wao huingia hapo na kulambishwa .

Kuna mengie ya kueleza hapa lakini baada ya hapa juu nadhani kama kuna mtu ana access na Wizara ya Afya basi anitafute chemba anipe info zaidi ili niende Dar kuelezea hali ilivyo maana hata mimi nimeombwa rushwa kwa uwazi ikabidi nimwite Mganga Mkuu na kumuuliza uhalali ule . Hakuna risiti baada ya malipo na pia kila Nurse huomba rushwa wazi wazi maana wanajua ubaya wa Uongozi kwa kuwa wote wanakula na hakuna wa kumfuza mwenzake .Vifo Musoma vinatawala maana kama huna pesa kwanza basi utawekwa hadi pesa ije . Hata kupata shula inakubdi kulipa 2000 na kusukuma mgonjwa pia malipo achilia mbali adha za ndani ya wodi .

Wenyeji wanasema kwamba ukitafa kuijua Musoma fika Wodi ya watoto na namba 6 huko utajua taabu zaidi .

Nimeakua kuchukua hatua .Je nianzie wapi maana Wizarani Dr.Muniko ana mtu wake na kuondoka Musoma imekuwa ngoma . Watu wanakueleza kwamba Muniko na Meneja wa Uwanja wa Karume hapa Musoma hawawezi kuondolewa na wana mizizi minene. Je Prof. Mwakyusa haya ndiyo maisha bora kwa wananchi wa Mkoa wa Mara hasa kwenye huduma ?

Muniko hata haki za watumishi anazima na vifaa vya hospitali ikiwamo TV nk anahamishia kwake .Marupueupu Musoma ni ndoto na ukichonga mbele Muniko unaodolewa kama Mbwa mwizi .

Mugishangwe,

asante sana kwa kujulisha JF members hili. Kuna waandishi wa habari hapa na ninahakika watafuatilia hii na kuandika (kama itawezekana).

Hapa kuna kazi sana ingawa wananchi wa Musoma itabidi waaamue siku moja kufanya kitu kuhusu hili. Watetezi wa serikali watasema kuwa sio kila jambo ni kazi ya serikali kuu kufanya.

Ninavyofahamu mimi huduma za afya bado ziko serikali (nakubali kukosolewa katika hili). Hizi documentation inabidi zitunzwe ili marafiki zetu wakituuliza (namquote mwalimu hapa ) tuseme kuwa sababu, nia na uwezo wa kuwatoa mafisadi madarakani tunavyo...
 
ukitaka kujua tanzania kuna matatizo kila mahali ni pale unapopatwa na shida,kila kona ya nchi ni matatizo.

kuhusu matibabu sio musoma pekeyake ni hospitali zote za serikali matatizo yao yanafanana.
niliuliza hapa siku moja hivi toka tupate uhuru serikali imejenga hospitali ngapi?
lakini tunasoma waziri ananunuliwa gari lenye thamani ya milion 100,hivi hizi pesa tunaweza kujenga wodi ngapi za kitanzania na kuweka vitanda ?
 
ukitaka kujua tanzania kuna matatizo kila mahali ni pale unapopatwa na shida,kila kona ya nchi ni matatizo.

kuhusu matibabu sio musoma pekeyake ni hospitali zote za serikali matatizo yao yanafanana.
niliuliza hapa siku moja hivi toka tupate uhuru serikali imejenga hospitali ngapi?
lakini tunasoma waziri ananunuliwa gari lenye thamani ya milion 100,hivi hizi pesa tunaweza kujenga wodi ngapi za kitanzania na kuweka vitanda ?

I agree with u.
 
1-Maisha bora kwa kila mtanzania
2-Kasi mpya nguvu mpya ari mpya
3-Majuu kila kukicha, nikirudi nuymbani ni ziara mikoani tu,
hapokwanini uchumi wangu usipae?

Hao wanosema watu wanakufa wana wivu tu, hawataki mwenzao afaidi.
 
lakini inasikitisha sana hali ya shule zetu,hosptali,barabara,huduma za jamii huku serikali ikifanya manunuzi na ufisadi mkubwa mfano wa kununulia mawaziri ,manaibu,makatibu,wakurugenzi na uchochoro wa maofisa wa serikali mashangingi yanayozidi milioni mia kila gari na mafuta yakilipiwa....hawa watu ni wabaya sana na hawajali chochote zaidi ya maslahi yao...naomba tusiwapigie kura maana ndio zawadi bora tutakayoweza kujipa wenyewe.
 
siku moja nilikuwa nasikiliza hotuba ya PM,G.Brown ktk mkutano wa chama chake,alisema hivi(Alipokuwa na umri wa miaka 16 alikuwa anacheza rugby na wenzake shuleni lakini kwa bahati mbaya mwenzak
e alimgonga kwa bahati mbaya usoni na kumsababisha maumivu ktk macho yake,kwa hiyo aliumia,lakini kwa jitihada za madktari waliweza kuokoa jicho moja na ndilo analotumia)hiyo ndio siri inayomsukuma kila mwaka kwa yeye kuipa kipaumbele bajeti ya NHS.
Tukirudi bongo viongozi wote wanatibiwa nje ni nani anakumbuka kuweka mazingira bora ktk hospitali zetu.Ndio maana siku hizi wakifa wanaifadhiwa lugalo baada ya kuona muhimbili pananuka,wangekuwa na uwezo basi hta mochwari zingetumika za ulaya. wakiumwa hata tumbo tu utawakuta wanalazwa MOI,wakati pale ni sehemu ya wagonjwa wa mifupa.
 
Wakati Kikwete akiendeleza uvasco da gama na kuvumbua dunia upya kwa safari zake nje ya nchi na ujumbe wako mzito unaotumbua mabilioni ya pesa chache zilizopo hazina, watoto zaidi watakufa kwa magonjwa yanayotibika huko Tanzania!
 
ukitaka kujua tanzania kuna matatizo kila mahali ni pale unapopatwa na shida,kila kona ya nchi ni matatizo.

kuhusu matibabu sio musoma pekeyake ni hospitali zote za serikali matatizo yao yanafanana.
niliuliza hapa siku moja hivi toka tupate uhuru serikali imejenga hospitali ngapi?
lakini tunasoma waziri ananunuliwa gari lenye thamani ya milion 100,hivi hizi pesa tunaweza kujenga wodi ngapi za kitanzania na kuweka vitanda ?

Katibu tarafa, unayoongea ni pointi tupu. Waafrika tuna matatizo makubwa ya "prioritization" Yaani unaweza kujiuliza usipate majibu. Nadhani tumelaaniwa
 
Wakati Kikwete akiendeleza uvasco da gama na kuvumbua dunia upya kwa safari zake nje ya nchi na ujumbe wako mzito unaotumbua mabilioni ya pesa chache zilizopo hazina, watoto zaidi watakufa kwa magonjwa yanayotibika huko Tanzania!

Mimi nakwambia ni pata shika nguo kuchanika. Vurugu mtindo mmoja. Yaani kuzaliwa afrika tabu kwelikweli.
 
siku moja nilikuwa nasikiliza hotuba ya PM,G.Brown ktk mkutano wa chama chake,alisema hivi(Alipokuwa na umri wa miaka 16 alikuwa anacheza rugby na wenzake shuleni lakini kwa bahati mbaya mwenzak
e alimgonga kwa bahati mbaya usoni na kumsababisha maumivu ktk macho yake,kwa hiyo aliumia,lakini kwa jitihada za madktari waliweza kuokoa jicho moja na ndilo analotumia)hiyo ndio siri inayomsukuma kila mwaka kwa yeye kuipa kipaumbele bajeti ya NHS.
Tukirudi bongo viongozi wote wanatibiwa nje ni nani anakumbuka kuweka mazingira bora ktk hospitali zetu.Ndio maana siku hizi wakifa wanaifadhiwa lugalo baada ya kuona muhimbili pananuka,wangekuwa na uwezo basi hta mochwari zingetumika za ulaya. wakiumwa hata tumbo tu utawakuta wanalazwa MOI,wakati pale ni sehemu ya wagonjwa wa mifupa.

Dr.Watson akitueleza ukweli, tunavimba. Hii intelligence ya viongozi wetu wa afrika iko wapi hasa.
 
Dr.Watson akitueleza ukweli, tunavimba. Hii intelligence ya viongozi wetu wa afrika iko wapi hasa.

Mwanamalundi,

Ndio maana nilisema somewhere kuwa ninaelekea kukubaliana na Ngabu kuwa: kama viongozi wetu ni reflection yetu na hiki ndicho wanafanya and yet tunawachagua over and over again! then kuna something wrong somewhere!
 
siku moja nilikuwa nasikiliza hotuba ya PM,G.Brown ktk mkutano wa chama chake,alisema hivi(Alipokuwa na umri wa miaka 16 alikuwa anacheza rugby na wenzake shuleni lakini kwa bahati mbaya mwenzak
e alimgonga kwa bahati mbaya usoni na kumsababisha maumivu ktk macho yake,kwa hiyo aliumia,lakini kwa jitihada za madktari waliweza kuokoa jicho moja na ndilo analotumia)hiyo ndio siri inayomsukuma kila mwaka kwa yeye kuipa kipaumbele bajeti ya NHS.
Tukirudi bongo viongozi wote wanatibiwa nje ni nani anakumbuka kuweka mazingira bora ktk hospitali zetu.Ndio maana siku hizi wakifa wanaifadhiwa lugalo baada ya kuona muhimbili pananuka,wangekuwa na uwezo basi hta mochwari zingetumika za ulaya. wakiumwa hata tumbo tu utawakuta wanalazwa MOI,wakati pale ni sehemu ya wagonjwa wa mifupa.

Ni kwasababu Tanzania tunaona wajanja ni wale wanaosoma shule za maana, wanaotibiwa nje au hospitali za maana, wanaoendesha magari ya nguvu nk. Wenzetu hapa wanaamini tofauti, ndio maana mwanasiasa kutibiwa hospitali za serikali ni kitu cha kumwongezea kura.

Kwa Tanzania watakuita mjinga, umezubaa, umeshindwa kutumia nafasi. Hayo sio maneno ya wanasiasa, ni maneno ya sisi wapiga kura.

Bila kubadili hiyo culture ya kufurahia vitu tusivyo na uwezo navyo, tutaendelea kutengeneza mafisadi wengi tu.

Kuna jamaa yangu serikalini, alipokuwa nje alikuwa anapinga kama akina Mtanzania tu, karudi, kapewa ulaji, baada ya muda nikaona na Shangingi, kumuuliza ndugu yangu kulikoni? Anasema wenzake walikuwa wanamcheka kwenye mikutano maana kila mtu na shangingi wakati yeye na gari la kawaida.

Niliishiwa nguvu, ndio maana siku hizi siwaamini Watanzania kwenye masuala ya utawala bora, labda mpaka nione mtu anafanya kwa vitendo. Haya ya kuongea hapa JF, asilimia zaidi ya 90 ni kama huyo jamaa yangu tu.

Wengi tunasema kwasababu hatujapata nafasi ya ulaji.

Hata kwa pesa ndogo zinazotolewa hospitalini, ilitakiwa watu wasife hivyo lakini, ufisadi sasa sio kwa wanasiasa tu na ni mpaka wafanyakazi wa ngazi za chini.
 
...

Wengi tunasema kwasababu hatujapata nafasi ya ulaji.

Hata kwa pesa ndogo zinazotolewa hospitalini, ilitakiwa watu wasife hivyo lakini, ufisadi sasa sio kwa wanasiasa tu na ni mpaka wafanyakazi wa ngazi za chini.

NO hapana mtanzania,

usikatishe tamaa watoto walioko vyuoni wanaosoma sasa hivi kwa matumaini ya kuwa watu safi na watendaji wema. Mimi naamini kuwa kuna vijana wanasoma mlimani au vyuo vingine bongo ambao wakipewa nchi wataiongoza vizuri kwa uadilifu na wema.

Thats my take
 
Mwanamalundi,

Ndio maana nilisema somewhere kuwa ninaelekea kukubaliana na Ngabu kuwa: kama viongozi wetu ni reflection yetu na hiki ndicho wanafanya and yet tunawachagua over and over again! then kuna something wrong somewhere!

Bwana wee, when you start thinking about this, it is hard to think about anything else. I know some people would say, NO, this is bullshit!! But in reality the truth hurts.
 
NO hapana mtanzania,

usikatishe tamaa watoto walioko vyuoni wanaosoma sasa hivi kwa matumaini ya kuwa watu safi na watendaji wema. Mimi naamini kuwa kuna vijana wanasoma mlimani au vyuo vingine bongo ambao wakipewa nchi wataiongoza vizuri kwa uadilifu na wema.

Thats my take

Mwafrika wa Kike,

Mimi sijakata tamaa wala sikatishi tamaa wengine ila nawaambia ukweli. Mimi mwenyewe watu wengi tu wananiita mjinga kwasababu nikiwa TZ kila kitu nafanya kwa utaratibu, matokeo yake kitu cha kufanya siku moja wakati mwingine inachukua wiki. Watu wanashanga, una pesa ya kutoa lakini hutaki?

Mimi nampa mtu pesa baada ya kumaliza kazi yangu na nikaridhika na alivyoifanya basi nitatoa asante kwasababu najua wengi wanafanya kazi kwenye mazingira magumu. Ile ilani ya TANU bado naikumbuka "Sitatoa wala kupokea rushwa"

Kama nilivyoandika mara nyingi, mimi niko kwenye vijiwe vya kwenye Internet toka miaka ya 90, tumegongana na watu wengi sana ambao sasa ndio vigogo wetu. Zaidi ya asilimia 90 yao, utendaji kazi wao ni mbovu tofauti na walivyokuwa wanasema walipokuwa Europe.

Tunahitaji msaada wa mungu kutuokoa na majanga ya hawa viongozi wetu.

Ndio maana muda wote mimi nashauri tujiangalia kila mtu mahali alipo, je anatoa haki kwa wale wanaotegemea haki yake? Kama una uhakika juu ya hilo basi angalau una right ya kuwarushia mawe mafisadi.
 
Mwafrika wa Kike,

Mimi sijakata tamaa wala sikatishi tamaa wengine ila nawaambia ukweli. Mimi mwenyewe watu wengi tu wananiita mjinga kwasababu nikiwa TZ kila kitu nafanya kwa utaratibu, matokeo yake kitu cha kufanya siku moja wakati mwingine inachukua wiki. Watu wanashanga, una pesa ya kutoa lakini hutaki?

Mimi nampa mtu pesa baada ya kumaliza kazi yangu na nikaridhika na alivyoifanya basi nitatoa asante kwasababu najua wengi wanafanya kazi kwenye mazingira magumu. Ile ilani ya TANU bado naikumbuka "Sitatoa wala kupokea rushwa"

Kama nilivyoandika mara nyingi, mimi niko kwenye vijiwe vya kwenye Internet toka miaka ya 90, tumegongana na watu wengi sana ambao sasa ndio vigogo wetu. Zaidi ya asilimia 90 yao, utendaji kazi wao ni mbovu tofauti na walivyokuwa wanasema walipokuwa Europe.

Tunahitaji msaada wa mungu kutuokoa na majanga ya hawa viongozi wetu.

Ndio maana muda wote mimi nashauri tujiangalia kila mtu mahali alipo, je anatoa haki kwa wale wanaotegemea haki yake? Kama una uhakika juu ya hilo basi angalau una right ya kuwarushia mawe mafisadi.

Mhhhh hapa umenena!

Mtanzania 1 mwafrika wa kike 0

I knew kuwa kuna point unataka kumake na nikazidi kuchokoa ili niipate. Maveterani kama nyie mnahitajika sana hapa JF na kwa kweli mtanzania nina hakika wengi wanaosoma hapa watazingatia hili.

Kwa kweli itahitaji msaada wa MUNGU maana wakati mwingine inatisha kabisa hata kufikiria. Ninaamini watoto wa Buzwagi na kanda ya ziwa ambao utajiri wao umechukuliwa hivi mbele ya macho yao wataamuka siku moja na kusema kuwa inaf iz inaf!
 
niliandika nikiamini kuwa viongozi wetu kweli hawapapendi muhumbili nikafikiri huyu atatutoa kimasomaso kumbe patupu,hivi osterbay na muhimbili au lugalo ni wapi karibu? basi watutangazie tu kuwa hospitali ya lugalo ni ya viongozi iliwatu tujue.
 
niliandika nikiamini kuwa viongozi wetu kweli hawapapendi muhumbili nikafikiri huyu atatutoa kimasomaso kumbe patupu,hivi osterbay na muhimbili au lugalo ni wapi karibu? basi watutangazie tu kuwa hospitali ya lugalo ni ya viongozi iliwatu tujue.

katibu tarafa hilo ni swali zuri sana?

Kuna mwanaJF hapa alitoa data kuwa gharama ya kuleta daktari wa nje (kama ndio wanaaminiwa na serikali) kuja kutibu Tz ni only 5% ya gharama wanazotumia kupeleka viongozi wa serikali nje ya nchi kutibiwa!
 
siku nane zimepita kuanzia mugishangwe aweke hii thread hapa!

kwa speed hii, kuanzia tarehe 21, watoto 40 na watu wazima 32 wamekufa katika hospitali ya musoma!

Kikwete endelea tu kuchoma mapesa kwa safari zako mwaya!
maisha ya hawa watoto hayana thamani kama ziara yako ya kwenda kuiona timu ya mpira ya spain! au kuangalia soccer UK!
 
Back
Top Bottom