Watoa rushwa wakipitishwa CCM tutaupigia upinzani

Chonde chonde Wajumbe wa Vikao vya kupitisha majina ya wagombea Ubunge, tunawatahadharisha mapema, mkiwabeba watoa rushwa kwa kisingizio cha funika kombe mwanaharamu apite au eti wagombea walizidiana kura Tunawapigia Wapinzani.

CCM Suala la Rushwa tumeutangazia ulimwengu kuwa tunapambana nal. Leo iweje rushwa ndani ya chama tushindwe kupambana nayo?

Watanzania wote wanajua jinsi wagombea wa CCM walivyoshinda kwa rushwa kwenye majimbo yao, je wakati wa kampeni wananchi tutawambia nini juu ya vita dhidi ya rushwa wakati sisi wenyewe ni watoa na wapokea rushwa?

Agenda ya rushwa wapinzani wataitumia kwa nguvu zao zote. Watoa rushwa wasipitishwe kugombe ubunge au udiwani wamekichafua chama.

Mkuu umetoa angalizo zuri sana. Hata hivyo kwani ccm wanategemea kura kutangazwa washindi au madaraka ya rais? Taasisi zote ikiwemo Takukuru wanaamini kuwa wanawajibu wa kuibeba ccm, ndio maana badala ya watoa rushwa kupelekwa mahakamani, wanawapeleka kwenye kamati ya ccm. Hapo unajiuliza Takukuru kazi yao ni nini iwapo wajibu wao wanawakabidhi wanasiasa. Iwapo rais ataendelea kuachwa bila kushitakiwa, na kupewa madaraka makubwa kama ilivyo sasa, rushwa haitakaa iishe nchi hii.
 
Mkuu takukuru ni kama wamewaogopa sisiemu, wamesema suala hilo wanaliachia chama kuamua
TAKUKURU wamekasimisha majukumu yao kwa Bashiru na Pole pole?Wajiuzulu kama taasisi na kuiachia kazi hiyo kwa CCM tufahamu kuwa hampo kutusaidia kutokomeza rushwa.
 
Hivi mwenyekiti ataanzaje kuwatuhumu, wagombea kwa kutoa rushwa wakati yeye na timu yake wametoa rushwa ya vyeo, na pesa kwa wapinzani ili waunge mkono juhudi

Kabisa, mwenyekiti wa ccm ndio aliyeiongoza kwa kutoa rushwa kwenye project ya kuungwa mkono juhudi, ndio maana Takukuru hawana nguvu yoyote maana wanajua fika hakuna vita yoyote serious ya rushwa.
 
Chonde chonde Wajumbe wa Vikao vya kupitisha majina ya wagombea Ubunge, tunawatahadharisha mapema, mkiwabeba watoa rushwa kwa kisingizio cha funika kombe mwanaharamu apite au eti wagombea walizidiana kura Tunawapigia Wapinzani.

CCM Suala la Rushwa tumeutangazia ulimwengu kuwa tunapambana nal. Leo iweje rushwa ndani ya chama tushindwe kupambana nayo?

Watanzania wote wanajua jinsi wagombea wa CCM walivyoshinda kwa rushwa kwenye majimbo yao, je wakati wa kampeni wananchi tutawambia nini juu ya vita dhidi ya rushwa wakati sisi wenyewe ni watoa na wapokea rushwa?

Agenda ya rushwa wapinzani wataitumia kwa nguvu zao zote. Watoa rushwa wasipitishwe kugombe ubunge au udiwani wamekichafua chama.

Mbona woote mnao like ni chadema na wewe mtoa post,
Hata wakipitisha asiyetoa bado hutampigia kura, sasa hapa unadanganya nani
 
Bila ya kumsahau yule wa pale Kawe aliyejitambulisha tu jina kisha akarudu kukaa. Sijui ni nanii wa nani vile?.
 
Ambaye hakupata kura hata moja yaani 0. Huyo ndo hakutoa Rushwa kwa upande wa CCM. Kila mjumbe aliyetoa kura yake alilipwa na hakuna ambaye aliitoa bure
Je ikitokea watia nia wote walitoa rushwa lakini kila mjumbe alipiga kura mmoja tu matokeo yake zikazaliwa zero ,1 na 150,320 utafuta uchaguzi au utafanya upendeleo wa kiana?
 
Mary Mwanjelwa naibu waziri anaye shughulikia rushwa naye yasemekana katoa rushwa. Kuna clip zake ziko hewani
 
Suala hili ni tete mno na linahita hikima ya hali ya juu. Kwanza wako walioingia kwenye mkumbo wa rushwa kwasababu anaona wengine wanatoa na wajumbe wanamwambia mkono mtupu haulambwi.

Pili uko mfumo wa hovyo sana. Wabunge kwa vile wao ni watunga sheria wanajipa kiinua mgogongo kila baada ya miaka mitano. Haijalishi ataendelea au haendelei. Hizi fedha za kiinua mgongo cha Wabunge ni moja ya kichocheo kikubwa sana cha rushwa wakati wa uchaguzi. Tufikie mahali iwe Mbunge anayepewa kiinua mgongo ni yule aliyesema anastaafu na atakaye shindwa kwenye uchaguzi tu. Wanaoendelea wasipewe wasubirie mwisho wa safari yao, kutafutwe kikokoteo kitakacho husisha muda aliotumikia kama Mbunge. Hii itakuwa ngumu kidogo kwasababu ya msigano wa maslahi na wabunge ndio watunga sheria lakini Mkuu wa nchi au hata jopo la watu wanaoheshimika katika jamii wapewe kisheria Veto juu ya Bunge.

Hiki kinua mgongo cha wabunge kwa staili hii ya sasa ni dhuluma hata kwa wafanyakazi wengine, si haki hata kidogo ni kama wamejipendelea flani hivi kila baada ya miaka mitano unachukua kinua mgongo halafu unarudi kwenye kazi hiyohiyo miaka mingine mitano.

Pia tufike mahali tuachane na huu utaratibu wa Waziri lazima awe Mbunge. Hili ni tatizo jingine. Unakuta waziri ni mahiri katika utendaji wake na Rais anataka aendelee naye. Kwenye mchakato wa ubunge katoa rushwa. Na takukuru wamejua hilo, watafanyaje zaidi ya kuwarudishia chama wa amue maana Rais ni Mkt wa chama.

Yako mengi ngoja niache kwanza. Hapa Nakasukari Lupaso tetemeko halikusikika sana lilokuwa ni manyumanyu tu.
Naunga mkono hoja 100%
 
Ujajua CCM wameishafanya timing yao kiasi wakitoa majina ya wagombea wapinzani watakuwa wameishacukua fomu hivyo itakuwa vigumu kwao kuhamia vyama vingine.Vinginevyo wahamie vyama vidogo visivyo na nguvu.
 
Chonde chonde Wajumbe wa Vikao vya kupitisha majina ya wagombea Ubunge, tunawatahadharisha mapema, mkiwabeba watoa rushwa kwa kisingizio cha funika kombe mwanaharamu apite au eti wagombea walizidiana kura Tunawapigia Wapinzani.

CCM Suala la Rushwa tumeutangazia ulimwengu kuwa tunapambana nal. Leo iweje rushwa ndani ya chama tushindwe kupambana nayo?

Watanzania wote wanajua jinsi wagombea wa CCM walivyoshinda kwa rushwa kwenye majimbo yao, je wakati wa kampeni wananchi tutawambia nini juu ya vita dhidi ya rushwa wakati sisi wenyewe ni watoa na wapokea rushwa?

Agenda ya rushwa wapinzani wataitumia kwa nguvu zao zote. Watoa rushwa wasipitishwe kugombe ubunge au udiwani wamekichafua chama.
Waliopitishwa manyara, Kilimanjaro,Mara,dar,mbeya arusha.nitapeleka Kura yangu upinzani
 
Asilimia tisini ya wabunge wa CCM wamepita kwa rushwa takukuru wenyewe wanajua ,Kuna wabunge wamepitishwa mapaka unashangaa yaani mbunge watu hawataki hata kumuona unashangaa eti kashinda kura za Maoni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom