Wateule wa Rais wanawanyanyasa viongozi wa kuchaguliwa na wananchi

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Katika mfumo wa uongozi wa Taifa letu kuna viongozi wa aina 2 ambao ni Viongozi wa kuteuliwa na Rais na viongozi wanaochaguliwa na wananchi.

Viongozi wa kuteuliwa na Rais ni kama vile maDC, maRC, maDED japo kwa kutaja kwa uchache na viongozi wa kuchaguliwa na wananchi ni kama vile madiwani, wabunge na mameya.

Kwa upande wa viongozi wa kuteuliwa na Rais kama hao maDC na maRC ndiyo pia wenyeviti wa Kamati za ulinzi na usalama wa maeneo yao kwa maana hiyo vyombo vya usalama kwenye maeneo hayo huwa vinapokea maagizo kutoka kwa maDC na maRC hao.

Hata hivyo kumekuwa kukitolewa maoni na wananchi wengi kuwa kwa mfumo wa nchi yetu kuwa wa mfumo wa vyama vingi, hawaoni sababu za kuendelea kuwa na mfumo wa kuwa na maDC na maRC kwenye maeneo husika wakati kwenye maeneo hayo tuna watumishi wa Umma wenye nafasi za wakurugenzi wa miji/majiji ambao wanafanya kazi zinazofanana na hizo za hao maDC na maRC.

Tatizo lingine kubwa ambalo limejitokeza ni kuwa ingawa hao maDC na maRC nafasi zao hizo wanatakiwa kutekeleza majukumu yao wakiwa watumishi wa Umma bila kutumbukiza ushabiki wa kisiasa, kwa bahati mbaya sana maDC na maRC wetu wametumbukiza 'ukereketwa' wao wa wazi kabisa kwa chama tawala cha CCM.

Ndiyo maana tumeshuhudia kwa yale maeneo ambayo wananchi wamechagua viongozi wao kutoka vyama vya upinzani wakifanya shughuli zao katika wakati mgumu sana kutokana na vikwazo wanavyowekewa na wateule hao wa Rais.

Tumeshuhudia kwenye maeneo ambayo yana viongozi wa upinzani mara nyingi wakikamatwa na vyombo vya dola wakituhumiwa mathalani kufanya mikutano ya kisiasa ambayo haikutolewa vibali na Polisi!

Hata hivyo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 3(1) inabainisha wazi kuwa nchi yetu itakuwa na mfumo wa vyama vingi na vyama hivyo vya kisiasa vinatakiwa vifanye shughuli zao vikiwa Huru.

Wakati viongozi wa vyama vya upinzani wakipata wakati mgumu sana wa kufanya shughuli zao za kisiasa kwenye maeneo yao, hali ni tofauti kabisa kwa yale maeneo ambayo yana viongozi wa kuchaguliwa kutoka chama tawala cha CCM, ambapo maDC na maRC wa maeneo hayo husika huwa hawawanyanyasi hata kidogo viongozi hao wa kuchaguliwa kutoka chama tawala cha CCM.

Tumeshuhudia pia maDC na maRC hao kwenye maeneo ambayo wananchi wamechagua viongozi wa upinzani wakitumia sheria kandamizi ya kuwaweka ndani viongozi wa upinzani kwa masaa 'yao' 48 kwa kile ambacho huwa wanadai viongozi hao wa upinzani wametoa kauli za uchochezi ambao unaweza kuleta kuvunjika kwa amani kwenye eneo hilo husika.

Mfano halisi wa matumizi hayo mabovu ya sheria hiyo kandamizi ni namna DC wa Kinondoni, Ally Hapi alivyomweka ndani Mbunge wa Kawe kwa kile alichokiita kuwa ametoa kauli za kumtukana Rais Magufuli.

Ubovu mwingine wa sheria hiyo ni kuwa inamnyima natural justice mtuhumiwa ya haki ya kusikilizwa na DC au RC huyo anakuwa ndiye anayetuhumu, ndiye Polisi anayepeleleza kesi na wakati huo huo anakuwa Hakimu wa kuhukumu kesi!

Kwa mazingira yanavyoonekana ni kama vile miongoni ya 'job descriptions' za maDC na maRC hao ni kuwanyanyasa viongozi wa kuchaguliwa wa vyama vya siasa vya upinzani kwenye maeneo husika.

Mazingira pia yanaonyesha kuwa unyanyasaji huo wa maDC na maRC kwenye maeneo ambayo yana viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani yana all blessings kutoka kwa Mkuu wa nchi mwenyewe.

Kwa kuwa kama Mkuu wa nchi angekuwa habariki vitendo hivyo viovu ya hao maDC na maRC tungeshuhudia kutumbuliwa kwa maDC na maRC wa maeneo husika kutokana na matendo yao maovu.

Mfano wa wazi ni kwa vipi kwa mfano RC wa Dar, RC wa Arusha, DC wa Kinondoni,DC wa Meru na DC wa Hai waendelee kuwepo kazini wakati imethibitika beyond reasonable doubt kuwa utendaji wao wa kazi umelenga zaidi kuwanyanyasa na kuwadhalilisha viongozi wa kuchaguliwa kwenye maeneo yao husika?

Kwa hiyo nadhani wananchi tunapaswa tuipiganie Katiba mpya ya nchi ambayo itazifuta nafasi hizi za maDC na maRC ambazo hazina maslahi kwa Taifa badala yake zipo tu kwa ajili ya kukilinda chama kilichoko madarakani na kuleta chuki na uhasama miongoni ya viongozi wa Chama tawala na wale wenzao wa vyama vya upinzani
 
Yaani ukiyanena hayo mbele ya kazi tu, ukaonekana kuwazubaisha watu kwa kuyaneno yaliyo bayana ,ujumbe ukapenya na kupenyeka, utakuwa umetekeleza uzoroteshaji wa kazi
 
Ccm imebaka madaraka haitaki kuondoka, wapinzani bila ya kupigania haki yao na kuwa pamoja na wananchi wao. Ccm itabaki madarakani mpaka wapinzani watakapo amka kutoka usingizini.




Ndukiiiii

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
 
Hayo mambo hayo ndio maana sasa hivi kibiti sio salama tena

Sent from my Infinix NOTE 3 using JamiiForums mobile app
Halafu ndiyo Mkulu huyo huyo huwa anajinadi kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa yeye ni Rais wa wote bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Wakati katika hali halisi kivitendo tunaona namna viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, ingawa vyama hivyo vipo kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu, lakini tunaona viongozi hao wakati mwingine wanavyokuwa treated kama vibaka!

Halafu Mkuu huyo huyo kila siku anatuomba watanzania tuendelee kumwombea kwa Mungu.

Hivi yeye hajui kuwa Mungu wetu ni mpenda haki na huwa hapokei maombi ya mtu ambaye hatendi haki hadi pale mtu huyo atakapoitubu dhambi hiyo na kukiri kuiacha?
 
Halafu ndiyo Mkulu huyo huyo huwa anajinadi kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa yeye ni Rais wa wote bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Wakati katika hali halisi kivitendo tunaona namna viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, ingawa vyama hivyo vipo kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu, lakini tunaona viongozi hao wakati mwingine wanavyokuwa treated kama vibaka!

Halafu Mkuu huyo huyo kila siku anatuomba watanzania tuendelee kumwombea kwa Mungu.

Hivi yeye hajui kuwa Mungu wetu ni mpenda haki na huwa hapokei maombi ya mtu ambaye hatendi haki hadi pale mtu huyo atakapoitubu dhambi hiyo na kukiri kuiacha?
Never in your whole life TRUST a politician who is in POWER

Sent from my Infinix NOTE 3 using JamiiForums mobile app
 
Never in your whole life TRUST a politician who is in POWER

Sent from my Infinix NOTE 3 using JamiiForums mobile app

Wenye akili wameachamlie lie tu,mkieleweshwa akili zenu zinagoma.Mpuuzi mmoja kasema ya Kibiti chanzo chake ni kama ya mjadala huu.Huyu ni mpuuzi.

Nawauliza je kwa kuwa nchi ni ya vyama vingi ni halali wapinanzani kusema chochote mahali popote ila i haramu kwa watawala kusema chochote mahali popote? Wabunge ukumbi wao ni bungeni,madiwani mahali pao ni baraza la madiwani na kampeni ni kipindi cha uchaguzi.

Mnataka nini wana kudeka? Jakaya aliwabeba kwa mbereko mkamdhihaki na kuchana mbereko hamkutosheka mkaanza na kumchana kwa viwembe mgongo aliowabebea.Akawaonyesha kuwa mjiini mmemkuta,mbadala wake mtoto wa shamba,usipokwenda shamba hakuna kula na mboko utapata.Ukikulia mtaani huchagui cha kusema wala mahali pa kusemea,ukilelewa vema unachagua cha kusema na mahali pa kusemea.

Nitawakumbusha tena kauli ya waliotutawala mnaoamini kuwa ni kielelezo cha demokrasia "what matters is not what you say but how you say it"
 
Wenye akili wameachamlie lie tu,mkieleweshwa akili zenu zinagoma.Mpuuzi mmoja kasema ya Kibiti chanzo chake ni kama ya mjadala huu.Huyu ni mpuuzi.

Nawauliza je kwa kuwa nchi ni ya vyama vingi ni halali wapinanzani kusema chochote mahali popote ila i haramu kwa watawala kusema chochote mahali popote? Wabunge ukumbi wao ni bungeni,madiwani mahali pao ni baraza la madiwani na kampeni ni kipindi cha uchaguzi.

Mnataka nini wana kudeka? Jakaya aliwabeba kwa mbereko mkamdhihaki na kuchana mbereko hamkutosheka mkaanza na kumchana kwa viwembe mgongo aliowabebea.Akawaonyesha kuwa mjiini mmemkuta,mbadala wake mtoto wa shamba,usipokwenda shamba hakuna kula na mboko utapata.Ukikulia mtaani huchagui cha kusema wala mahali pa kusemea,ukilelewa vema unachagua cha kusema na mahali pa kusemea.

Nitawakumbusha tena kauli ya waliotutawala mnaoamini kuwa ni kielelezo cha demokrasia "what matters is not what you say but how you say it"
Sasa wewe unasema kampeni ni wakati wa uchaguzi, mbona Mwenyekiti wenu wa CCM Taifa kila siku anafanya mikutano na kufanya kampeni ya chama chake cha CCM huku akitumia mwamvuli kuwa yupo kwenye ziara za kiserikali?
 
Sasa wewe unasema kampeni ni wakati wa uchaguzi, mbona Mwenyekiti wenu wa CCM Taifa kila siku anafanya mikutano na kufanya kampeni ya chama chake cha CCM huku akitumia mwamvuli kuwa yupo kwenye ziara za kiserikali?

Ninajua Rais wa nchi yangu anazunguka kutueleza anafanya nini kutekeleza aliyoyaahidi na kutuagiza tufanye nini ili kuisogeza mbele Tanzania.Kwa sasa wimbo wake ni kazi halali kwanza porojo 2020.
 
Ninajua Rais wa nchi yangu anazunguka kutueleza anafanya nini kutekeleza aliyoyaahidi na kutuagiza tufanye nini ili kuisogeza mbele Tanzania.Kwa sasa wimbo wake ni kazi halali kwanza porojo 2020.
Sasa kama Rais wetu anafanya kampeni nchi nzima kwa mwamvuli wa ziara za kiserikali na kama anaamini kuwa Umma wa watanzania unawaunga mkono CCM kwa sasa na kuwa vyama vya upinzani vimeishiwa sera na vimekosa mvuto, ni kwanini basi anaogopa kuviruhusu vyama vya upinzani navyo vinadi sera zake vikiwa huru?

Kwa kuwa kuna msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza......

CCM na vyama vya upinzani viwe na uwanja sawa wa kufanya shughuli zao za siasa na baada ya hapo sisi wananchi ndiyo tutakaochambua kujua MCHELE ni upi na PUMBA ni ipi..........
 
Ccm imebaka madaraka haitaki kuondoka, wapinzani bila ya kupigania haki yao na kuwa pamoja na wananchi wao. Ccm itabaki madarakani mpaka wapinzani watakapo amka kutoka usingizini.




Ndukiiiii

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
It is true.....

TZ haina uwanja sawa wa kisiasa.

Kuna chama dola, ambacho ni CCM ambacho kinapewa upendeleo wote na serikali na vyama vya upinzani ambavyo vinakuwa treated kama 'vibaka' hapa nchini
 
Raisi anateua civil servants na ndio watu wanaoendesha mataifa ya wenzetu.

Kikawaida hawa wanalelewa mpaka kuwa makatibu wa wizara. Ukiielewa uo mchezo ungetaka madaraka ya teuzi za raisi yapunguzwe kawaida usalama wa wenzetu hadi mtu afikie nafasi ya kuwa influential kuendesha nchi kuanzia nafasi za katibu mkuu you have to prove your self.
 
Mfano mwingine wa wazi wa namna hawa wateule wa Rais wanavyowanyanyasa viongozi wa vyama vya upinzani na wanavyojiona wako above law na kuwa watakachofanya chochote hawataguswa na mkono wa sheria ni namna yule DC wa Hai alivyokwenda kuharibu kwa makusudi miundo mbinu ya shamba la Kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni, Mheshimiwa Mbunge Freeman Mbowe.

Huu utendaji wa kazi wa wateule wa Rais wa kutaka tu kuwakomoa viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani. utakuja kulifikisha Taifa hili mahali pabaya.
 
Kwanza binadamu hawana shukrani kipindi kilichopita rais alikua tofauti na Huyu wakamwita dhaifu na wakasema wanataka mtu mkali,wamempata anafanya kazi eti wanamwita muimla.Mungu hadhihakiwi km wanavyodhani.Kila zama Kuna aina ya uongozi unaofaa kwa wakati huo,na kwetu huu uongozi uliopo ndiyo unaohitajika kwa wakati huu.Asiyetaka yuko huru kuhama nchi aende atakako.

Sent from my Lenovo A606 using JamiiForums mobile app
 
Mliaji mwingine huyu hapa. Kweli mtaji wa MACCM ni ZERO BRAINS.



Wenye akili wameachamlie lie tu,mkieleweshwa akili zenu zinagoma.Mpuuzi mmoja kasema ya Kibiti chanzo chake ni kama ya mjadala huu.Huyu ni mpuuzi.

Nawauliza je kwa kuwa nchi ni ya vyama vingi ni halali wapinanzani kusema chochote mahali popote ila i haramu kwa watawala kusema chochote mahali popote? Wabunge ukumbi wao ni bungeni,madiwani mahali pao ni baraza la madiwani na kampeni ni kipindi cha uchaguzi.

Mnataka nini wana kudeka? Jakaya aliwabeba kwa mbereko mkamdhihaki na kuchana mbereko hamkutosheka mkaanza na kumchana kwa viwembe mgongo aliowabebea.Akawaonyesha kuwa mjiini mmemkuta,mbadala wake mtoto wa shamba,usipokwenda shamba hakuna kula na mboko utapata.Ukikulia mtaani huchagui cha kusema wala mahali pa kusemea,ukilelewa vema unachagua cha kusema na mahali pa kusemea.

Nitawakumbusha tena kauli ya waliotutawala mnaoamini kuwa ni kielelezo cha demokrasia "what matters is not what you say but how you say it"
 
Kwanza binadamu hawana shukrani kipindi kilichopita rais alikua tofauti na Huyu wakamwita dhaifu na wakasema wanataka mtu mkali,wamempata anafanya kazi eti wanamwita muimla.Mungu hadhihakiwi km wanavyodhani.Kila zama Kuna aina ya uongozi unaofaa kwa wakati huo,na kwetu huu uongozi uliopo ndiyo unaohitajika kwa wakati huu.Asiyetaka yuko huru kuhama nchi aende atakako.

Sent from my Lenovo A606 using JamiiForums mobile app
Hoja yako ni dhaifu.

Hata kama Taifa lilikuwa linataka Kiongozi wa awamu hii awe mkali zaidi kulinganisha na JK wa awamu iliyopita, lakini haikuwa inamaanisha tupate Kiongozi ambaye hataki kufuata Katiba ya nchi na sheria nyingine za nchi na badala yake atutawale kibabe!
 
Back
Top Bottom