Watetezi wa Lowasa: Ni kweli ni jasiri, mchapakazi lakini je umepima uzito wa upande wa pili

JUST

JF-Expert Member
Dec 10, 2010
552
234
Kumekuwa na watu mbali mbali hap JF wakimueleze Mh. Lowasa kuwa ni Jasiri, Mchapakazi na Mwenye upeo kufananisha na waliopo sasa.


mimi nasema mtazamo huo unatokana na mfumo wa CCM uliopo ambao hauwapi watu wengine kuonyesha uwezo na ufanisi wao bali unawaacha walewale kutokea uhuru pamaoja na watoto na wajuu wao. hivyo basi ndo maana wengi wanaona katika lili kundi la wanaoongoza Lowasa ndio anafaa. kwa hilo sipingani nao.

Ila ukweli ni kwamba viongozi wote walioko CCM kwa sasa hawafai kwasababu wote wanamapungufu makubwa ya kiungozi na kimaadili kiasi kwamba ni bora wapishe waje watu wenye uwezo wa kuongoza nchi.

kwa mantiki hiyo kashfa ya Lowassa ndiyo inayowapa wakati mgumu wa kumuona kama ni mtendaji mzuri maana hata waswahili wanasema huwezi mkabidhi fisi akulindie bucha.
 
sasa wewe tuambie ndani ya hiyo CCM kati ya wale wanaotwajwatajwa 2015 nani mchapa kazi kama Lowassa pamoja na maufisadi yake???
 
Kumekuwa na watu mbali mbali hap JF wakimueleze Mh. Lowasa kuwa ni Jasiri, Mchapakazi na Mwenye upeo kufananisha na waliopo sasa.


mimi nasema mtazamo huo unatokana na mfumo wa CCM uliopo ambao hauwapi watu wengine kuonyesha uwezo na ufanisi wao bali unawaacha walewale kutokea uhuru pamaoja na watoto na wajuu wao. hivyo basi ndo maana wengi wanaona katika lili kundi la wanaoongoza Lowasa ndio anafaa. kwa hilo sipingani nao.

Ila ukweli ni kwamba viongozi wote walioko CCM kwa sasa hawafai kwasababu wote wanamapungufu makubwa ya kiungozi na kimaadili kiasi kwamba ni bora wapishe waje watu wenye uwezo wa kuongoza nchi.

kwa mantiki hiyo kashfa ya Lowassa ndiyo inayowapa wakati mgumu wa kumuona kama ni mtendaji mzuri maana hata waswahili wanasema huwezi mkabidhi fisi akulindie bucha.

Usichanganye mambo, hapa iko hivi ... ili ccm waweze kumpata mgombea lazima atoke kwenye kundi la vigogo ambao kimsingi kwa level ya chini ni NEC kama sio CC, sasa katika kundi hilo hoja nikwamba hakuna mchapa kazi kama Lowasa kwahiyo wanaopinga wanapaswa kusema ni nani katika kundi hilo anaweza kuzidi record ya utendaji ya Lowasa, hakika wote ni mafisadi hakuna haja ya kuwashindanisha ila uchapaji kazi nani zaidi??

Wana mageuzi ili kutegua hichi kitendawili tupiganie katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu ujao na hatimaye mkuu wa kaya asitokane na magamba ila awe mwanamageuzi, la sivyo ufisadi utakuwa kama kawa yawezekana na utendaji ukawa sifuru pia
 
sasa wewe tuambie ndani ya hiyo CCM kati ya wale wanaotwajwatajwa 2015 nani mchapa kazi kama Lowassa pamoja na maufisadi yake???

Mbona mnampamba sana huyo mtu. Allisha jichafua hasafishiki huyo bado ana ari ileile ya ufisadi na kujitajirisha.
Hasafishiki!
 
Kumekuwa na watu mbali mbali hap JF wakimueleze Mh. Lowasa kuwa ni Jasiri, Mchapakazi na Mwenye upeo kufananisha na waliopo sasa (Hoja zilizotolewa recently zinamlinganisha Lowassa na Pinda, siyo "waliopo sasa" kama ulivyoweka hapa!! Na kwa vigezo mbalimbali, uchangamfu, umakini wa kazi, uelewa wa kazi, kutoa maamuzi, ukali kwa watumishi, ufuatiliaji wa kero etc utaona Lowassa kamuacha Pinda mbali sana)

mimi nasema mtazamo huo unatokana na mfumo wa CCM uliopo ambao hauwapi watu wengine kuonyesha uwezo na ufanisi wao bali unawaacha walewale kutokea uhuru pamaoja na watoto na wajuu wao (Si kweli kwa sababu Pinda ni mmojawapo wa viongozi waliopewa nafasi kuonyesha ufanisi wao, Kuna jipya uliloliona? Ukiacha JK Nyerere, marais wote waliofuatia wamekaa madarakani kwa kipindi cha miaka si zaidi ya 10, hii ni ushahidi kuwa nafasi zipo na uongozi unabadilika! Angalia ndani ya CCM kuna viongozi vijana kibao, wamepewa nafasi kuonyesha uwezo wao...Makamba, David Mathayo, Lawrence Marsha, Ngeleja etc...hawa wameingia katika mfumo baada ya kupewa nafasi ndani ya Chama kuonyesha uwezo wao...wapo kina Nape, Ridhiwani na wengine wengi?? Swali ni je wameweza?? Simply NO, tatizo si nafasi, tatizo ni lack opf patriotism.....)hivyo basi ndo maana wengi wanaona katika lili kundi la wanaoongoza Lowasa ndio anafaa. kwa hilo sipingani nao.

Ila ukweli ni kwamba viongozi wote walioko CCM kwa sasa hawafai kwasababu wote wanamapungufu makubwa ya kiungozi na kimaadili kiasi kwamba ni bora wapishe waje watu wenye uwezo wa kuongoza nchi.
(Ambao ni....??)
kwa mantiki hiyo kashfa ya Lowassa (For your information hadi leo hakuna aliyeweza ku-prove kwamba Lowassa yupo liable, in my opinion alionewa!! Wengi wamekuwa wakisema ana husika na ufisdi na kadhalika, lakini bor akipi?? Kuwa na fisadi mchapakazi anayelet amaendeleo kwa taifa, au asiyekuwa fisadi lakini hana uwezo wa kuongoza?? Be honest to yourself) ndiyo inayowapa wakati mgumu wa kumuona kama ni mtendaji mzuri maana hata waswahili wanasema huwezi mkabidhi fisi akulindie bucha.

My blue text explains it all...
 
Usichanganye mambo, hapa iko hivi ... ili ccm waweze kumpata mgombea lazima atoke kwenye kundi la vigogo ambao kimsingi kwa level ya chini ni NEC kama sio CC, sasa katika kundi hilo hoja nikwamba hakuna mchapa kazi kama Lowasa kwahiyo wanaopinga wanapaswa kusema ni nani katika kundi hilo anaweza kuzidi record ya utendaji ya Lowasa, hakika wote ni mafisadi hakuna haja ya kuwashindanisha ila uchapaji kazi nani zaidi??

Wana mageuzi ili kutegua hichi kitendawili tupiganie katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu ujao na hatimaye mkuu wa kaya asitokane na magamba ila awe mwanamageuzi, la sivyo ufisadi utakuwa kama kawa yawezekana na utendaji ukawa sifuru pia

Hivi hakuna lingine la kujadili zaidi ya huu utumbo wenu kila siku? Mchukue akawe kiongozi wa ukoo wenu, kama una upungufu wa uongozi. Tumechoka kusikia kibaka akizungumzwa tena kwa vitu hivyo hivyo vya kibwege kila siku. Your hands off us please!
 
Kumtetea Lowasa inabidi uwe na roho ya mwenda wazimu, jamani huyu mtu ni sawa na zigo la mavi habebeki.
 
kumkubali lowasa ni kukataa maneno ya baba wa taifa '.............lowasa ni mwizi...........'
 
(Soma makala hii hadi Mwisho uwajue na ujihadhari nao)

Na Jacob Malihoja

WAKATI Mhe.Edward Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu na hata katika nafasi zingine alizoshika hakupenda uzembe, hakupenda vitu vilale,hakupenda madudu mbali mbali yafanyike, hakuwa na mzaa .. hiyo ndio hulka yake kwasababu hiyo aliwashughulikia viongozi na watendaji wazembe wasiotekeleza wajibu wao vizuri, waliofanya madudu katika maeneo yao ya kazi.

Kwasababu watu walikuwa wakifanya kazi kwa mazoea jambo hili lilikuwa geni na kuona wanaonewa. Watu waliotafuna makaa ya moto wa Lowassa wamejenga chuki kubwa sana.

Kundi Lingine ni lile la kisiasa ambalo pengine Mheshimiwa Edward Lowassa hakuwaunga mkono wakati wa vinyang’anyiro Mbali Mbali na Labda aliwaunga mkono washindani wao.

Makundi haya yanaungana “sio rasmi” yanatema chuki kwa watu wanaowazunguka, marafiki, familia zao na jamaa wengine mbali mbali walio karibu nao.

Makundi haya yamekuwa kwa muda sasa yakitengeneza uongo wa aina mbali mbali. Kwa bahati Mbaya kuna makundi madogo ya watu ambao kimsingi wanamhitaji sana Lowassa, bila kujua wameingia kuwaunga mkono watu hao ambao wanadhani ni watetezi wa wananchi kumshambulia mtetezi wa kweli wa wananchi.

Wanatunga uongo ama kuuamini uongo uliotungwa kwa chuki binafsi. Kila kukicha uongo fulani unatungwa, watu hawa hata hofu ya Mungu hawana, kazi ni kutunga uongo tu kila siku na bila aibu kung’ang’ana na neno moja tu ambalo halina ushahidi na ni la kufikirika.

Wanapambana wakijifanya kuwatetea wananchi kumbe wao ndio maadui wakubwa wa wananchi wa tanzania kutokana na madudu yao na uzembe wao uliosababisha watafune makaa ya moto wa Lowassa. Watu hawa wanajaribu kufanya juhudi ili fikra zao zipolewe na viongozi wakuu wa chama na wafanya maamuzi mazito ili kumuanguasha Mheshimiwa Lowassa.

Mimi Siamini kama Wapanga maamuzi ni wepesi kiasi hicho cha kusikiliza kauli za watu waliotafuna makaa ya moto wa Lowassa kwasababu ya uzembe wao, wala siamini kama Viongozi hawa wafanya maamuzi ya juu watakuwa tayari kumezwa na chuki za kisiasa za kutoungwa mkono la Lowassa wakati wa vinyang’anyiro mbali mbali.

Watanzania wanatakiwa kuelewa kuwa vita dhidi ya Mhe. Edward Lowassa si vita dhidi ya Lowassa bali ni vita dhidi ya Watanzania masikini wanaohitaji mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuongeza kasi ya kupapamba na umasikini, ni vita dhidi ya vijana wote ambao leo wapo wanasoma katika shule za kata, ni vita dhidi ya vijana ambao leo wanasoma vyuo vikuu kikiwemo UDOM waliopita katika shule za kata na hata wengine pia.

Ni vita dhidi ya wananchi wa miji ya Shinyanga, Kahama ambao leo Janga la maji kwao imekuwa historia. Ni Vita dhidi ya vijana ambao hawana ajira ambao kwao Lowassa ni mtu mwenye vision ya kupanua kasi ya kukabili tatizo hilo.

Ni Vita dhidi ya Rais Dr. Jakaya Kikwete ambaye kimsingi anahitaji kupata mrithi mwenye nguvu kubwa ya kuendeleza Kazi Kubwa mno aliyoifanya.

Kwa Muono wangu Mhe. Edward Lowassa ndio mtu pekee atakayeweza kuendeleza kazi kubwa mno aliyoifanya Dr. Jakaya Kikwete na kulifanya deni la Taifa kuwa Tamu badala ya Chungu.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Edward Lowassa.

Tunakuombea Dr. Jakaya Mrisho Kikwete umpate mtu huyu Kuwa mrithi wako.
 
Hakuna maasai mjinga sana kiasi hiki!!!
Ungeweza kutumia akilia yako kuandika kitu positive zaid kuliko hili juu ya huyo chaguo lako!!

Aarbo menye. . . . .!!!!
 
Back
Top Bottom