Ranks
JF-Expert Member
- Oct 21, 2012
- 2,583
- 1,097
Ama kweli tangu kushambuliwa kwa Tundu Lissu na Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu kuamua kumnusuru na mauti mtetezi huyu wa kweli kwa wanyonge siasa ya bongo imebadilika sana.
Mioyo ya watesi wetu imeamua kujianika dhahiri shahiri mfano mzuri ni ukatili waliouonyesha kwenye uchaguzi wa marudio uliopita karibuni, ukatili na najisi waliyofanya ukijiuliza ni uchaguzi wa madiwani tu watu wauwawe, watu wapigwe na kuachwa na vilema kisa udiwani tu.
Sasa huu wa marudio kwa majimbo ya ubunge utakuwaje? Wa urais nao si ndio tutazalisha hadi wakimbizi na wengine kwenda kuuzwa huko Libya wakawe watumwa? Tunaipeleka wapi Afrika yetu?
Ni kweli tumekubali kurudi miaka 60-70 nyuma? Hebu pitia hoja ziso mashiko za hao wanaojiuzulu nafasi walizoaminiwa na wananchi na kutuletea gharama kubwa na hasara za marudio ya chaguzi.
Ukitazama kwa makini nguvu kubwa inayotumika kuwahadaa na kisha kuwanunua kwa fujo wale wa kusimama pamoja na Lissu unagundua kitu kimoja ya kwamba "WATESI WA WATANZANIA WANAOGOPA IMPACT YA KUREJEA KWA LISSU". Ni kweli pasi na shaka wanaogopa Lissu kurejea na kukuta ngome imara kwa hiyo wanachofanya ni kuvunja ngome ili arejeapo akute makamanda wamesambaratika.
Swali ni je watafanikiwa kuvunja ngome hii imara iliyojengeka kwenye mioyo ya wanyonge kwa kuwanunua wawakilishi wa wanyonge?
Mioyo ya watesi wetu imeamua kujianika dhahiri shahiri mfano mzuri ni ukatili waliouonyesha kwenye uchaguzi wa marudio uliopita karibuni, ukatili na najisi waliyofanya ukijiuliza ni uchaguzi wa madiwani tu watu wauwawe, watu wapigwe na kuachwa na vilema kisa udiwani tu.
Sasa huu wa marudio kwa majimbo ya ubunge utakuwaje? Wa urais nao si ndio tutazalisha hadi wakimbizi na wengine kwenda kuuzwa huko Libya wakawe watumwa? Tunaipeleka wapi Afrika yetu?
Ni kweli tumekubali kurudi miaka 60-70 nyuma? Hebu pitia hoja ziso mashiko za hao wanaojiuzulu nafasi walizoaminiwa na wananchi na kutuletea gharama kubwa na hasara za marudio ya chaguzi.
Ukitazama kwa makini nguvu kubwa inayotumika kuwahadaa na kisha kuwanunua kwa fujo wale wa kusimama pamoja na Lissu unagundua kitu kimoja ya kwamba "WATESI WA WATANZANIA WANAOGOPA IMPACT YA KUREJEA KWA LISSU". Ni kweli pasi na shaka wanaogopa Lissu kurejea na kukuta ngome imara kwa hiyo wanachofanya ni kuvunja ngome ili arejeapo akute makamanda wamesambaratika.
Swali ni je watafanikiwa kuvunja ngome hii imara iliyojengeka kwenye mioyo ya wanyonge kwa kuwanunua wawakilishi wa wanyonge?