Watesi wa watanzania wanaogopa kurejea kwa Lissu, sasa wanasambaratisha ngome

Ranks

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
2,583
1,097
Ama kweli tangu kushambuliwa kwa Tundu Lissu na Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu kuamua kumnusuru na mauti mtetezi huyu wa kweli kwa wanyonge siasa ya bongo imebadilika sana.

Mioyo ya watesi wetu imeamua kujianika dhahiri shahiri mfano mzuri ni ukatili waliouonyesha kwenye uchaguzi wa marudio uliopita karibuni, ukatili na najisi waliyofanya ukijiuliza ni uchaguzi wa madiwani tu watu wauwawe, watu wapigwe na kuachwa na vilema kisa udiwani tu.

Sasa huu wa marudio kwa majimbo ya ubunge utakuwaje? Wa urais nao si ndio tutazalisha hadi wakimbizi na wengine kwenda kuuzwa huko Libya wakawe watumwa? Tunaipeleka wapi Afrika yetu?

Ni kweli tumekubali kurudi miaka 60-70 nyuma? Hebu pitia hoja ziso mashiko za hao wanaojiuzulu nafasi walizoaminiwa na wananchi na kutuletea gharama kubwa na hasara za marudio ya chaguzi.

Ukitazama kwa makini nguvu kubwa inayotumika kuwahadaa na kisha kuwanunua kwa fujo wale wa kusimama pamoja na Lissu unagundua kitu kimoja ya kwamba "WATESI WA WATANZANIA WANAOGOPA IMPACT YA KUREJEA KWA LISSU". Ni kweli pasi na shaka wanaogopa Lissu kurejea na kukuta ngome imara kwa hiyo wanachofanya ni kuvunja ngome ili arejeapo akute makamanda wamesambaratika.

Swali ni je watafanikiwa kuvunja ngome hii imara iliyojengeka kwenye mioyo ya wanyonge kwa kuwanunua wawakilishi wa wanyonge?
 
sasa hivi ni ubabe njenje na watu wanashangilia kabisa,inashangaza mno,mimi kuna mijitu huku kitaa ukikutana nayo inakuambia huyu jamaa anachapa kazi halafu likimaliza hapo linaomba buku ya kula siku hizi wala sina muda wa ku explain nawaambia kavu sina kitu halafu wananikuta grocery nakula balimi
 
sasa hivi ni ubabe njenje na watu wanashangilia kabisa,inashangaza mno,mimi kuna mijitu huku kitaa ukikutana nayo inakuambia huyu jamaa anachapa kazi halafu likimaliza hapo linaomba buku ya kula siku hizi wala sina muda wa ku explain nawaambia kavu sina kitu halafu wananikuta grocery nakula balimi
Ni ombaomba balaa hao.,ni wakuogopa na kukaa nao mbali kama ukoma.
 
"WATESI WA WATANZANIA WANAOGOPA IMPACT YA KUREJEA KWA LISSU".Ni kweli pasi na shaka wanaogopa Lissu kurejea na kukuta ngome imara kwa hiyo wanachofanya ni kuvunja ngome ili arejeapo akute makamanda wamesambaratika.
Swali ni je watafanikiwa kuvunja ngome hii imara iliyojengeka kwenye mioyo ya wanyonge kwa kuwanunua wawakilishi wa wanyonge?
Chanzo cha umasikini wa nchi zetu ni wanasiasa. Hawamjali yeyote, bali wao wenyewe na wanaoamua kuwa nao kwa maslahi ya kujinufaisha. Hakuna cha mnyonge wala mlalahoi.
Kwanza kuwepo kwa umasikini na ujinga ndio mtaji wa wao kuchaguliwa, hivyo hawajali kama kodi za walalahoi zinatumika aje, kama ndio hongo za kuzusha kujiuzulu kwa wapinzani au kurudia uchaguzi, na bado nyingine zinachotwa tu kufadhili mikutano yao.
 
Tumbo mbele ndiyo changamoto ya siasa za Africa; Tanzania ikiwemo. Wanasiasa wanajiangalia wao na watakachopata na siyo wewe unayejiita mnyonge.

Usituhumu serikali au CCM tatizo ni njaa ya wawakilishi wameshindwa kujitambua.

Kila mtu , apambane na hali yake na siyo kuwalaumu wapinzani kwa kuhama vyama vyao bali ; na wao ndiyo wameamua kupambana na hali zao kwa style hiyo.
 
Aabh huna point za maana
Hii ni outcome ya ALBADRI, mlizani inautani?? RISASI mumpige nyinyi hao hao halafu mseme ni serikali?? Kwahiyo serikal haina wapigaji wazuri wa risasi mpk mtu atumie risasa 32 kwa mpigoo???
Bro fanyakazi ili uokoe maisha yako na familia yako
Huna ulijualo kweny SIASA
 
Ukweli ni kuwa chadema ijenge mfumo wa chama sio MTU, ndio maana MTU akitoka mnaliona pengo wakati chama sio MTU ni watu.
 
Aabh huna point za maana
Hii ni outcome ya ALBADRI, mlizani inautani?? RISASI mumpige nyinyi hao hao halafu mseme ni serikali?? Kwahiyo serikal haina wapigaji wazuri wa risasi mpk mtu atumie risasa 32 kwa mpigoo???
Bro fanyakazi ili uokoe maisha yako na familia yako
Huna ulijualo kweny SIASA
Swali, kwanini mnakataa wachunguzi wa kimataifa kama kweli hamkuhusika? Waleteni wale watasema ni upinzani au serikali, mnaogopa nini, halafu ndugu zetu waliouwawa nje ya tz mnadai mnaomna UN ifanye uchunguzi wa kina, wa ndani hamtaki, kubalini waje wafanye yao muondoe lawama
 
Swali, kwanini mnakataa wachunguzi wa kimataifa kama kweli hamkuhusika? Waleteni wale watasema ni upinzani au serikali, mnaogopa nini, halafu ndugu zetu waliouwawa nje ya tz mnadai mnaomna UN ifanye uchunguzi wa kina, wa ndani hamtaki, kubalini waje wafanye yao muondoe lawama
Tukiruhusu maa a yake hatuna uwezo wa kufanya sisu wwnyew ila uwezo upoo
 
Mods wangeweka na kile kitufe cha 'thumbs down' ingekuwa pouwa sana!
tapatalk_1512797752204.jpeg
 
Hawa wanaohama hama ndiyo maadui wakubwa wenye kiwango sawa na CCM,tuwaonyeshe hasira zetu kwenye kura na kulinda,jicho kwa jicho.
Hawa wakisimamishwa tena hatuwapi hata kura za mama zao.
 
Tukiruhusu maa a yake hatuna uwezo wa kufanya sisu wwnyew ila uwezo upoo
Hatuna ndio uwezo mpaka sasa kinachoshindikana ni nini, hatuendi kwenye mfumo wa analojia maotaka nyie sasa ni dijitali ili kwenda na muda, waleteni hili suala liishe, la sivyo mtaendelea kulaumiwa, au pesa iliyopo ni ya kununua wapinzani, kateni huu mzizi, tusonge mbele, tujenge viwanda mnavyosema,
 
Back
Top Bottom