Watendaji wakuu wa ACT Wazalendo mnachomfanyia Zitto Kabwe siyo kitu kizuri, Pia Magufuli anakosea

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Kumekuwa na taarifa kuwa viongozi na watendaji wakuu wa ACT Wazalendo wanapewa nafasi za kiutendaji huku wao wenyewe wakiwa tayari kutumikia nafasi hizo na kuahidi ushirikiano kwa rais Magufuli bila hata ya kiongozi wao mkuu ndugu Zitto Kabwe kupewa taarifa za awali.

Pia rais Magufuli anakosea sana kuwasiliana na viongozi wa ACT Wazalendo na hatimaye kuwapa nyadhifa mbalimbali za kiutendaji bila hata ya kuomba ushauri na mapendekezo kwa kiongozi mkuu wa chama hicho ndugu Zitto Kabwe.

Kumteua mwenyekiti wa chama cha siasa ambacho kinapinga sera za chama tawala kwenda kuwa msimamizi mkuu wa ilani ya chama tawala na kupokea maelekezo ya kiutendaji kutoka kwa mwenyekiti mwenzake wa chama kingine cha siasa ni kitendo cha kudhoofisha siasa za vyama. Rais Magufuli ameonyesha kuwa ACT Wazalendo sii chochote mbele yake na ndiyo maana anajichagulia tu anayemtaka ndani ya chama hicho. Huu ni mtego ambao rais Magufuli anautumia kufuta demokrasia ya vyama vingi nchini. Hivi kweli inaingia akilini kwa mwenyekiti wa chama cha upinzani kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa na hatimaye akasimamie na kuhakikisha utekelezaji wa ilani ya chama tawala ili kukizidishia sifa chama hicho? Mwenyekiti huyo wa chama cha siasa ni pandikizi? Chama cha upinzani kinakuwa na mwenyekiti pandikizi!

Naamini kuwa hata Zitto anaelewa kuwa mama Mghwira hakustahili hata kusubiri kamati kuu ili wajadili uteuzi huo. Alitakiwa kuukataa palepale kutokana na hali halisi ilivyo.
 
Sisi ACT tukipata fursa ya kueatumikia wananchi tunawatumikia kea kwenda mbele . Aidha, tunakuwa viongozi wa mfano ili wengine waige.
 
Angekuwa anakwenda kutekeleza ilani za CCM ingekuwa bora kwa kuwa ilani za vyama vyote vinalenga kuleta maisha bora kwa mwananchi, tofauti ni katika utekelezaji,kibaya zaidi ni pale ambapo atalazimika kuwa kada wa CCM ambaye atalazimika kukipigania chama hicho na mambo yake yote.
 
Mimi sioni shida hapa, Mama Mghwira alimpa Magufuli ilani ya ACT. Sasa kama kaamua kuwapa jukumu la kutekeleza ilani waliyompa shida inatoka wapi?!
 
Acha kutuchezea akili. Hao wateule humpa taarifa kiongozi wao kabla ya kurudisha jibu kwa rais.

Zitto alikubali na ameendelea kukubali teuzi hizo kufanyika.
 
Hujui kuwa wafanyakazi wote serikali wanatimiza Ilani ya Uchaguzi ya CCM?

Hujui kuwa wabunge wanatimiza Ilani ya Uchaguzi wa CCM kwa kupitisha sera za CCM na kuwa sheria za nchi.
 
Je, kabla ya ACT kuundwa alikuwa mwanachama wa chama cha siasa? Kama ndio, alikuwa chama gani?
 
Wala hamna ubaya maana ACT ni Ccm ndani ya upinzani. Ifahamike hiki chama kilianzisha kama mbeleko ya Ccm. Hivuo ni wakimbizi wanarudi nyumbani
 
Kumekuwa na taarifa kuwa viongozi na watendaji wakuu wa ACT Wazalendo wanapewa nafasi za kiutendaji huku wao wenyewe wakiwa tayari kutumikia nafasi hizo na kuahidi ushirikiano kwa rais Magufuli bila hata ya kiongozi wao mkuu ndugu Zitto Kabwe kupewa taarifa za awali.

Pia rais Magufuli anakosea sana kuwasiliana na viongozi wa ACT Wazalendo na hatimaye kuwapa nyadhifa mbalimbali za kiutendaji bila hata ya kuomba ushauri na mapendekezo kwa kiongozi mkuu wa chama hicho ndugu Zitto Kabwe.

Kumteua mwenyekiti wa chama cha siasa ambacho kinapinga sera za chama tawala kwenda kuwa msimamizi mkuu wa ilani ya chama tawala na kupokea maelekezo ya kiutendaji kutoka kwa mwenyekiti mwenzake wa chama kingine cha siasa ni kitendo cha kudhoofisha siasa za vyama. Rais Magufuli ameonyesha kuwa ACT Wazalendo sii chochote mbele yake na ndiyo maana anajichagulia tu anayemtaka ndani ya chama hicho. Huu ni mtego ambao rais Magufuli anautumia kufuta demokrasia ya vyama vingi nchini. Hivi kweli inaingia akilini kwa mwenyekiti wa chama cha upinzani kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa na hatimaye akasimamie na kuhakikisha utekelezaji wa ilani ya chama tawala ili kukizidishia sifa chama hicho? Mwenyekiti huyo wa chama cha siasa ni pandikizi? Chama cha upinzani kinakuwa na mwenyekiti pandikizi!

Naamini kuwa hata Zitto anaelewa kuwa mama Mghwira hakustahili hata kusubiri kamati kuu ili wajadili uteuzi huo. Alitakiwa kuukataa palepale kutokana na hali halisi ilivyo.


Mbona Mbowe kaSex na Wema Sepetu bila ya kuomba ruhusa kutoka kwa Mke wake wa ndoa? Tena mtoto wa Muanzilishi wa chadema Mzee Mtei, kuna usaliti zaidi ya huo Dunia hii? Hivyo ziba kwanza Paa la nyumba yako kwanza kabla ya kuhamia kwa jirani!
 
Back
Top Bottom