Watendaji wa Maabara ya Taifa ya Tanzania mmeshindwa kazi!

mwehu ndama

JF-Expert Member
Nov 12, 2019
543
1,828
Wakuu,

Baada ya kukaa likizo bongo kwa wiki tatu nilifanya vipimo vya Corona na kulipia ada ya malipo ya Tsh. 230,000 siku ya Jumatano tarehe 4 ili nijiandae na safari yangu iliyokuwa jana siku ya Ijumaa tarehe 6.

Cha ajabu mpaka ilipofikia lisaa limoja kabla ya muda wangu wa safari bado majibu yangu hayakuwa yametoka, hali iliyosababisha nianze kufuatilia na kufanikiwa kupata namba za simu za emergency desk ya MAABARA ya TAIFA.

Nilipopiga na kumueleza shida yangu kwamba mpaka sasa sijapata certificate yangu ya majibu alianza kupaniki na kunifokea bila sababu za msingi huku akiniambia nisipotulia sitoipata.

Jambo hili lilisababisha niamue kufanya rapid test na kutoa pesa nyingine ya ziada tsh 60,000.

Mpaka sasa niko njiani nikisubiri kuunganisha usafiri mwingine kuelekea mwisho wa safari yangu na nikiangalia email naona sijatumiwa hayo majibu bado.

Sina la kusema zaidi ya kuwachukia watumishi wote wa MAABARA ya TAIFA.
 
Na sasa wamepata hili la chanjo ni deal no 2..

Watauza sana vyeti bila kuchanja...
Mimi sina hamu nao,,walinichezesha siku 2..
Nusu nichelewe ndege..

Mafinyango yao.....
 
Husda na Roho mbaya tumeziweka mbele mno! Kuna watu huwa wanaona fulani akipitia mikononi mwangu akafanikiwa inakuwaga kama dhambi vile
 
Tutakuwa wasindikizaji tu
Mtu kupata kazi anajiona ndio dunia yote yake

Hawa wafanyakazi hawana heshima wala utu
Majigambo mengi na majibu ya karaha utafikiri umetembea na wake zao
 
Hakuna watu wanaopiga pesa kipindi hiki kama hukoo rushwa nje nje fastaaa unapewa majibu km ukiwa mbahili umeumia.
 
Hao waliokujibu hivyo hujampiga hata kelb ya mdomo? Kweli una roho ya uvumilivu utakua padre wewe
 
Mi nalia na TAMISEMI mpaka leo sijapata kibali cha kuhama zaidi ya miezi 6.Napolomoka kiuchumi ishu zangu zinafeli,familia yangu ip peke yake.
Nchi ya laana mijitu inaendekeza sana rushwa.
 
Hapo hawajakupa majibu ambayo ni negative (-) lakini ukifika mbele ya safari unapimwa na kukutwa positive (+)! Yaani ni aibu sana. Ndio maana hata mapapai, mbuzi na kwale walipatikana kuwa positive pia.
 
nchi imerudi nyuma imerudi enzi za awamu ya nne
Naam, nimepima hiyo kitu kama mara nane hivi, nikiri kusema majibu yalikuwa yanatoka kwa wakati hata kama kulikuwa na mashaka ya uwezo wa upimaji wenyewe.

Kasheshe imeanza juzi kati tu hapa, watu waliopima tarehe 31/07 niliwasikia wakilalama kuwa wameshindwa kusafiri siku 2 mbele kwa kukosa vyeti na bila maelezo yoyote ya kwanini hawajapata majibu.

Mwingine akasema yeye alipima kabla ya hapo, akapewa cheti kinasema NOT NEGATIVE.

Pia wanasema eti mlungula = NEGATIVE + ON TIME
 
Naam, nimepima hiyo kitu kama mara nane hivi, nikiri kusema majibu yalikuwa yanatoka kwa wakati hata kama kulikuwa na mashaka ya uwezo wa upimaji wenyewe.

Kasheshe imeanza juzi kati tu hapa, watu waliopima tarehe 31/07 niliwasikia wakilalama kuwa wameshindwa kusafiri siku 2 mbele kwa kukosa vyeti na bila maelezo yoyote ya kwanini hawajapata majibu.

Mwingine akasema yeye alipima kabla ya hapo, akapewa cheti kinasema NOT NEGATIVE.

Pia wanasema eti mlungula = NEGATIVE + ON TIME
Sasa kimfano umepewa cheti negative alafu ukafika nchi husika ukapimwa ukawa positive si ni kuchafua nchi
 
Sasa kimfano umepewa cheti negative alafu ukafika nchi husika ukapimwa ukawa positive si ni kuchafua nchi
Ni biashara tu, wachezaji walitoka hapa, wakafika kule wakaambiwa ni +ve ilhalk huku walipimwa wakawa -ve. Na wachezaji wa kule walipimwa kabla ya kuja huku wakawa -ve ila walivyopimwa hapa wakawa +ve😀

Kupima unalipwa dollar 100, kupigwa chanjo unalipwa dollar 100 kwenye fulani.

Hapa kwetu, kipimo ni dollar 100 + pesa ya kituo, kuchanjwa ni bure na hiari.
 
Ni biashara tu, wachezaji walitoka hapa, wakafika kule wakaambiwa ni +ve ilhalk huku walipimwa wakawa -ve. Na wachezaji wa kule walipimwa kabla ya kuja huku wakawa -ve ila walivyopimwa hapa wakawa +ve😀

Kupima unalipwa dollar 100, kupigwa chanjo unalipwa dollar 100 kwenye fulani.

Hapa kwetu, kipimo ni dollar 100 + pesa ya kituo, kuchanjwa ni bure na hiari.
This is tanzania
 
Public servant's wengi ni wazinguaji sana,maana wamepata kazi kwa deal, uwezo hawana kila kitu wanaendesha kujuana juana tu, Rushwa Tz ni sehemu ya kazi
 
Back
Top Bottom