Wateja TTCL Mobile/BroadBand

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Tumekuwa tunasikia malalamiko mengi sana kutoka kwa wadau wanaotumia huduma za ttcl mobile na broadband kwamba pesa zao zinaenda sana wakitumia mtandao haswa wale waliounganishwa moja kwa moja angalau hawa wenye kudial .

Wengi wa watu hawa wakienda ttcl kwenyewe nafikiri wanashindwa kupewa msaada wa uhakika jinsi ya kutumia computer zao uzuri ili wasipoteze pesa nyingi zaidi .

Kama wewe ni mmoja wa wadau na unasikitika kwa kutumia hela nyingi kwa ajili ya kutumia mtandao tu , fuata hatua nitakazosema hapo chini nina uhakika itapunguza gharama hizo kwa kiasi kikubwa .

AUTOMATIC UPDATES .
Kila siku katika mtandao kuna kuwa na maongezeko ya patches kadhaa zinazotakiwa kuwekwa katika computer yako , sasa unapojiunga tu kama unatumia windows basi itajiunga moja kwa moja na mtandao wa Microsoft ili kupata hizi updates .

Unachotakiwa ni kudisable automatic updates

1- Right Click My Computer

Ondoa hiyo tiki halafu apply – ok , wakati mwingine unaweza kutumia programu ya autopatcher ambayo inakuwa na update hizi au unakuwa na programu maalumu kwa ajili ya updates .

Kumbuka sio update zote ni muhimu kwa ajili ya matumizi yako ya kila siku ya computer .

ANTIVIRUS UPDATE
Antivirus nyingi zinahitaji updates za moja kwa moja mfano Norton definition yake kwa sasa ni mb 18 mcafee ni mb 23 na zinazidi kuongezeka kila kukicha ili kuweka computer yako salama zaidi , sasa ufanye nini ?

Kama unataka updates za antivirus ni bora uende katika internet cafes , watoa huduma wengi wanakuwa na hizi updates au wanajua njia za kuzichukulia , unabeba na flash kisha unaenda kuweka katika computer yako .

Ukisema utumie hiyo ttcl kudownload unakazi kubwa kwa sababu spidi yake ni ndogo sana pesa zako zote zitaisha na hautapata hiyo update unayoitaka .

Mfano mb 1 unalipa shilingi 70 sasa unataka mb 23 x 70 = 1670 , ukichanganya na mwendo wa kudownload utaona unatumia zaidi ya alfu 4 hapo bila kupata kitu .

Hiyo ni vitu viwili vinavyomaliza pesa zaidi ingiwa kuna programu zingine ambazo nazo zinahitaji updates za mara kwa mara kwahiyo wewe kama mtumiaji unatakiwa uweke zile programu unazofanyia kazi tu katika computer yako zile ambazo hazihusiani na shuguli zako unatakiwa uzifute .

Au unaweza kudisable zisiwe zinafanya kazi mpaka pale unapoamua wewe kuzitumia

1 – Start – Run – andika msconfig

Kuna kitu kama hichi kitakuja – system configuration utility



Programu zinazoonekana zote ziko katika taskbar kwahiyo ondoa pata katika programu zote ambazo hupendi zifanye kazi kama huna kazi nazo kama acrobat reader , nero , na programu zingine ambazo huwa zinastart moja kwa moja .

TTCL MOBILE WENYEWE
Ni vizuri ttcl mobile wenyewe waweke mirror katika tovuti zao au link maalumu ambazo wateja wao wanaweza kudownload baadhi ya hizo updates kwa urahisi zaidi ili kuwapunguzia wateja hawa gharama kubwa na ufanyaji kazi wao uwe rahisi zaidi .

Huo ni ushauri wangu tu , wewe kama mtumiaji una haki ya kutokufuata ushauri na mawazo yangu kama unaona hauna manufaa au hauwezi kubadilisha gharama katika matumizi yako ya mtandao .

ONYO :
Unatakiwa uonane na mtaalamu wa mambo hayo anaweza kukusaidia zaidi usijaribi kitu ambacho hujui au huna uhakika nacho haswa katika hatua ya pili ya startup unaweza kuleta madhara kwa programu zingine katika utendaji wake wa kazi .

Nakaribisha maswali zaidi kutoka kwa wadau mbali mbali , naamini tunaweza kuboresha huduma hizi kama tukiamua kushirikiana na kupashana habari hizi kwa uwazi zaidi

Andika kwa email hapo juu au simu +255 784 360204 lakini kumbuka sifanyi kazi TTCL wala sina uhusiano wowote ule na TTCL mimi ni mdau kama wadau wengine wengi .
 
Mtandao wa TTCL (Broadband) bado ni ghali sana. Nafikiria kubadili. Natafuta alternative internet connection.
 
Mtandao wa TTCL (Broadband) bado ni ghali sana. Nafikiria kubadili. Natafuta alternative internet connection.

Kama ungekuwa unatumia TTCL mobile (wengi huziita Broadband) basi ningekushauri uigeuze kuna sehemu kwa nyuma ina kijinafasi cha kuchomeka line (sim card) then ondoa na jaribu kuweka ya Zantel Data (inauzwa Tshs 10,000/=) kisha angalia kama inaweza kusomeka. Ikiweza kusomeaka YOU ARE DONE! Hapo utakuwa na urahisi wa kuhamia Zantel kirahisi na speed ya Zantel kwa maelezo niliyopata kwa wengi ni kuwa iko nzuri kulinganisha na TTCL mobile.

Siwapigii debe lakini anayestahili na apewe!
 
AUTOMATIC UPDATES .
Kila siku katika mtandao kuna kuwa na maongezeko ya patches kadhaa zinazotakiwa kuwekwa katika computer yako , sasa unapojiunga tu kama unatumia windows basi itajiunga moja kwa moja na mtandao wa Microsoft ili kupata hizi updates .

Unachotakiwa ni kudisable automatic updates


..shy,ushauri ulioutoa utapunguza gharama,lakini,kumbuka usalama wa pc au mac utakuwa hatarini!

..labda,kwa kuchangia,...anaweza fanya hivyo kama anafahamu wapi atapata updates za uhakika na zilizo salama na si loaded with malware!na akumbuke kuwa hii anatakiwa kufanya mara kwa mara!

..kuepuka gharama hii kuna costs zake kubwa zaidi!what i'll advise is, for him/her not to download large files[movies,programs,pdf catalogs,etc]on that pc!labda atumie nyingine kama ataweza,either kwenye cafe au ofisini[kama hawajali mtu kutumia pc zao kwa mambo binafsi]!

Kumbuka sio update zote ni muhimu kwa ajili ya matumizi yako ya kila siku ya computer.

..seconded!

ANTIVIRUS UPDATE
Antivirus nyingi zinahitaji updates za moja kwa moja mfano Norton definition yake kwa sasa ni mb 18, mcafee ni mb 23 na zinazidi kuongezeka kila kukicha ili kuweka computer yako salama zaidi , sasa ufanye nini ?

..kama ana-connect mara kwa mara si lazima,kwani updates za kila siku ni ndogo na hazichukui muda mwingi!na mara nyingi hazizidi 900 kb!akiwa ana-connect mara moja lets say kwa wiki mbili,obvious file litakuwa nene!


Ukisema utumie hiyo ttcl kudownload unakazi kubwa kwa sababu spidi yake ni ndogo sana pesa zako zote zitaisha na hautapata hiyo update unayoitaka.

..are you using ttcl mobile[cdma modem] or ttcl broadband[dsl modem]. mobile kwasasa ina-speed nzuri kidogo,zamani ilikuwa slow!. broadband ni kama jina lenyewe linavyojielezea!hivyo ku-download si kazi!na hasa katika broadband its a breeze!

..kwasasa,broadband is the cheapest,95tshs bila kodi kwa 1mb!na mobile ni 260tshs bila kodi kwa 1mb! zantel mobile ni cheap[kitu kama 50tshs kwa 1mb]but is coverage limited!

..ushauri wangu ni kuwa,kama mtu hayuko mobile sana out of dar or any city for that matter na anakaa katika nyumba for at least two years or so,hata mwaka,aweke ttcl broadband!


ONYO :
Unatakiwa uonane na mtaalamu wa mambo hayo anaweza kukusaidia zaidi usijaribi kitu ambacho hujui au huna uhakika nacho haswa katika hatua ya pili ya startup unaweza kuleta madhara kwa programu zingine katika utendaji wake wa kazi.

..zingatia ushauri huu!

Nakaribisha maswali zaidi kutoka kwa wadau mbali mbali , naamini tunaweza kuboresha huduma hizi kama tukiamua kushirikiana na kupashana habari hizi kwa uwazi zaidi

..neno la busara!
 
Kama ungekuwa unatumia TTCL mobile (wengi huziita Broadband) basi ningekushauri uigeuze kuna sehemu kwa nyuma ina kijinafasi cha kuchomeka line (sim card) then ondoa na jaribu kuweka ya Zantel Data (inauzwa Tshs 10,000/=) kisha angalia kama inaweza kusomeka. Ikiweza kusomeaka YOU ARE DONE!

..una maanisha ruim card!itabidi ai-reset hiyo modem halafu afanye settings za zantel,of which aende kwenye website yao au pale ofisini kwao!

..ila hatopata coverage kama anayopata kwenye ttcl mobile!kwa miji yote mikubwa!



Siwapigii debe lakini anayestahili na apewe!

..tutajuaje!lol!
 
Sawa Wakuu,
Naelekea kuwaelewa,
Sasa nahitaji ufafanuzi hapa;kwa sisi tunaotumia ile ya mezani lakini wireless wenyewe wanaita mobile (TTCL) ghalama hapa na kuepuka kwake hizo hgalama sijaelewa vizuri eti tuziuze..?
 
Ingekuwa vizuri wataalamu mkafanyia kazi na kutengeneza matrix ya gharama za connection na utumiaji wa mtandao mbali mbali eg TTCL, Simbanet, BOL etc na kushauri watumiaji. This information is lacking kwa sisi watumiaji.
 
Sawa Wakuu,
Naelekea kuwaelewa,

..shukrani!

Sasa nahitaji ufafanuzi hapa;kwa sisi tunaotumia ile ya mezani lakini wireless wenyewe wanaita mobile (TTCL) ghalama hapa na kuepuka kwake hizo hgalama sijaelewa vizuri eti tuziuze..?

..kuna mawili!moja ni kuuza[ila si busara sana,kwani ipo siku utaihitaji at least kwa dharura au ukienda likizo kwenu musoma!]

..pili,na hii ni muhimu,ni kuunganisha ttcl broadband!ila usipende kuangalia sana flash presentations on websites na youtube videos kama unataka kupunguza gharama!ukweli ni kuwa,u can't have your cake and eat it too!

..ooh,bila kusahau ku-download large files!.ila kusoma post jf haigharamu sana,ni punje katika kikombe cha mchele!hivyo unashawishiwa ku-spend muda zaidi jf!
 
Ingekuwa vizuri wataalamu mkafanyia kazi na kutengeneza matrix ya gharama za connection na utumiaji wa mtandao mbali mbali eg TTCL, Simbanet, BOL etc na kushauri watumiaji. This information is lacking kwa sisi watumiaji.

..dotori,gharama za ttcl @ ttcl.co.tz. za zantel @ zantel.co.tz.

..simbanet,bol,etc sitozijadili kwa kuwa mada inaongelea gharama nafuu na wao hawa-fit kwenye hilo!

..wazo la matrix ni zuri,ila linaitaji muda!si unajua,wengine tu wavivu kufanya kazi!
 
..shukrani!



..kuna mawili!moja ni kuuza[ila si busara sana,kwani ipo siku utaihitaji at least kwa dharura au ukienda likizo kwenu musoma!]

..pili,na hii ni muhimu,ni kuunganisha ttcl broadband!ila usipende kuangalia sana flash presentations on websites na youtube videos kama unataka kupunguza gharama!ukweli ni kuwa,u can't have your cake and eat it too!

..ooh,bila kusahau ku-download large files!.ila kusoma post jf haigharamu sana,ni punje katika kikombe cha mchele!hivyo unashawishiwa ku-spend muda zaidi jf!



Ni mekusoma Mkuu,Thanks.
 
Mimi ni mmoja wa waathirika wa TTCL mobile kwani waliingia sokoni kijanja sana , mwanzo walikuwa wanatucharge Tsh 50 kwa MB moja ila sasa ni TSH 264 kwa 1mb imebidi niache kutumia ttcl niende cafe kwani ukiweka 10,000 ndani ya masaa 2imeisha mwanzo nilidhani kuna mtu anatumia simu vibaya ila baada ya kuwapigia ttcl ndio wakanieleza kwa kweli ttcl wametukatili sana.
 
Mimi ni mmoja wa waathirika wa TTCL mobile kwani waliingia sokoni kijanja sana , mwanzo walikuwa wanatucharge Tsh 50 kwa MB moja ila sasa ni TSH 264 kwa 1mb imebidi niache kutumia ttcl niende cafe kwani ukiweka 10,000 ndani ya masaa 2imeisha mwanzo nilidhani kuna mtu anatumia simu vibaya ila baada ya kuwapigia ttcl ndio wakanieleza kwa kweli ttcl wametukatili sana.

..pole!

..wakati mwingine kwenda i cafe si solution ya gharama,kama utaangalia usumbufu unaoupata na kuwa limited na wakati gani u-surf net!

..ttcl broadband itasaidia zaidi!
 
Nimejaribu kuunga mobile yangu kwa Infrared, usb cable & bluetooth, kwa line ya Celtel "internet.tz.celtel.com" lakini gharama ni juu saaaana. Sijajua kama nikitumia hiyo ya zantel itaconnect. nataka kujua kama kuna ambaye amejaribu akafaulu
 
Guys..Mimi natumia zantel..It is damn cheap...I used to have a TTCL na Vodacom 3G modems..but ..Unaweza kufa maskini...Watch out...!
 
Mimi ni mmoja wa waathirika wa TTCL mobile kwani waliingia sokoni kijanja sana , mwanzo walikuwa wanatucharge Tsh 50 kwa MB moja ila sasa ni TSH 264 kwa 1mb imebidi niache kutumia ttcl niende cafe kwani ukiweka 10,000 ndani ya masaa 2imeisha mwanzo nilidhani kuna mtu anatumia simu vibaya ila baada ya kuwapigia ttcl ndio wakanieleza kwa kweli ttcl wametukatili sana.

Kwa wateja wa TTCL na Zantel, kina kitu ni lazima mfaahamu.

Kuna RETAIL na BUNDLE prices - na hizi bei zake ni tofauti sana.

Kama unataka unafuu wa huduma, basi uwe unanunua bandwidth ya kukutosheleza kila mwanzoni mwa mwezi. Kwa wale wanaopenda kuweka vocha wanapokuwa na mwahitaji kama mkuu hapo juuu, gharama zitakuumiza sana. Kwa mfano, kwa wireless broadband ya TTCL, bundle price ni 50Tsh/MB na retail ni 160Tsh/MB - nadhani tofauti ipo wazi hapa ni zaidi ya mara tatu.

Wireless Broadband ya TTCL bei zake ni kama ifuatavyo:

500MB - 40,000Tsh = 80Tsh/MB

1GB - 70,000Tsh = 70Tsh/MB

2GB - 100,000Tsh = 50Tsh/MB

Kitu kingine cha kuelewa ni kwamba, hizi internet za TTCL, Zantel Vodacom e.t.c zinalenga wafanya biashara na mabosi maofisini ambao wanahitaji internet sana kwa mawasiliano. Kwa mfanya biashara 100,000Tsh kwa mwezi ni hela ndogo sana. Ila kama wewe ni mfanyakazi wa kawaida tu au mwanafunzi, hii internet itakuumiza!
 
Kuna RETAIL na BUNDLE prices - na hizi bei zake ni tofauti sana.

Kweli, Watu wengi bado hawaja lielewea hili somo. (Kama una uwezo) Ni bora mtu ulipie bundle- kifurushi ili upate discount.
Lakini ukinuna voucher kama 500tsh, 1000tsh watakukata kwa bei ya retail

E.g. Sasatel
Ukingiza voucher 500tsh ,1000tsh..etc - Watakukata TSH 120/MB

Lakini:
Ukiingiza Voucher 40,000/- watakukata TSH 66.7/MB
Ukiingiza Voucher 120,000/- watakukata TSH 39.1/MB

Kwahiyo mimi mahesabu yangu ni 120/MB - 39.1/MB = nimesave 80.9TSH. Alafu it expires after 6 months na sio kila mwezi lazima niweke fedha tena.

B.P
 
Kweli, Watu wengi bado hawaja lielewea hili somo. (Kama una uwezo) Ni bora mtu ulipie bundle- kifurushi ili upate discount.
Lakini ukinuna voucher kama 500tsh, 1000tsh watakukata kwa bei ya retail

E.g. Sasatel
Ukingiza voucher 500tsh ,1000tsh..etc - Watakukata TSH 120/MB

Lakini:
Ukiingiza Voucher 40,000/- watakukata TSH 66.7/MB
Ukiingiza Voucher 120,000/- watakukata TSH 39.1/MB

Kwahiyo mimi mahesabu yangu ni 120/MB - 39.1/MB = nimesave 80.9TSH. Alafu it expires after 6 months na sio kila mwezi lazima niweke fedha tena.

B.P
Hi to all!
Say me please which provider will be better fo me , if I want just download 1 file 5 gb - which provider will be cheaper???
 
Back
Top Bottom