Watch Out; Tigo Pesa, M-Pesa ni Janga Kuu, wengi Wameumia!!

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,423
29,084
Ujio wa Hizi huduma za kifedha kupitia simu za Mikononi ukiacha kurahisisha uchukuaji, utumaji, uhifadhi na uwekaji wa Fedha, pia umetengeneza Ajira kwa watu wengi tu ambao labda kabla yake wangekua vijiweni tu.

Lakini pia ujio huu wa hizi huduma umekuja pia na utapeli wa aina ya juu, na wengi wamelizwa kupitia hizi huduma. Labda tu tupeane tahadhari jinsi huo utapeli unavyofanyika ili angalau tuweze kujikinga.

1)KUSEVU NAMBA KAMA TIGOPESA/M-PESA
Utapeli huu unafanyika kwa anaejifanya Mteja kuchukua simu ya muuzaji kisha akaisevu namba yake kama Tigo-Pesa kwenye simu ya muuzaji. Haya yanaweza kufanyika pale ambapo mteja feki anajifanya anataka kutengeneza mawasiliano zaidi na muuzaji.
Kinachofuata ni yeye kutuma msg kwa muuzaji kwamba "Umehamishiwa kiasi cha Tshs...... Kutoka kwa...." ambapo msg hiyo itajionyesha imetoka Tigopesa na mteja/tapeli kuchukua mzigo.

2)CANCEL TRANSACTION THROUGH CUSTOMER CARE
Hii inafanyika kwa mtumaji hela kununua mzigo na kutuma Tigopesa halali, kinachofuata ni kua mkiachana tu mnunuaji/tapeli anapiga simu Customer Care na kusema kua ametuma wrong number hivyo anaomba a-cancel transaction huku akiwa kshaondoka na mzigo.

3) HAMISHA HELA KUPATA JINA KISHA FREEZE NAMBA
Mbinu hii inatumika kwa Tapeli kuhamisha japo alfu 2 mradi tu apate jina la mtumiaji wa hiyo namba baada ya kuhamisha.
Kinachofuata ni Tapeli kwenda kwenye kibanda cha tigopesa na kujifanya yeye ndio mwenye namba hiyo nmba Na jina lake ndilo hilo na kaipoteza hivyo anaomba kui-freeze ili afunguliwe ingine.
Baada ya hapo, tapeli akiwa na laini ya wizi anaanza kutuma msg kujifanya amekwama hivyo anaomba asaidiwe.
Mbinu hii ili ifanikiwe inabidi amlainishe sana mwenye kibanda, ikiwezekana hata kumhonga ili aweze kupata namba mbalimbali zilizowasiliana na hiyo laini.

Wakuu wangu ni haya tu ningependa tu-share kwa leo.
Shark
 
Umefanya utafiti au unaropoka tu kwa kuchafua mpango mzima wa kuwarahisishia wananchi huduma hizi hasa kusikokuwa na Benki yaani huko vijijini??
 
Umefanya utafiti au unaropoka tu kwa kuchafua mpango mzima wa kuwarahisishia wananchi huduma hizi hasa kusikokuwa na Benki yaani huko vijijini??
Mkuu hayo yote yanatokea na hii ni challenge kwa watoa huduma (voda, tigo et al) kuweza kuziba hizi loopholes hususan issue ya watu kununua bidhaa alafu kupiga simu customer care..., I have seen it happening
 
Umefanya utafiti au unaropoka tu kwa kuchafua mpango mzima wa kuwarahisishia wananchi huduma hizi hasa kusikokuwa na Benki yaani huko vijijini??

Mkuu mbona naona kama umekwazika? Mdau ametoa tahadhari kwa wadau wengine, tena kwa nia njema tu. which is good.
 
Umefanya utafiti au unaropoka tu kwa kuchafua mpango mzima wa kuwarahisishia wananchi huduma hizi hasa kusikokuwa na Benki yaani huko vijijini??

Naona kama wewe ndio Unaropoka, nimetoa advantages za hizi huduma kama vile kurahisisha utumaji, upokeaji pamoja na uhifadhi wa hela, pia ajira.
Pia nikatoa na tahadhari na namna mbalimbali watu wanavyolizwa.
Au mkuu wewe ni mojawapo ya hao Walizaji so nimegusa anga zako nin??
 
Umakini unahitajika sana katika kutumia na kutunza kumbukumbu zetu kwa huduma hizi. Shukrani mdau
 
naona kama wewe ndio unaropoka, nimetoa advantages za hizi huduma kama vile kurahisisha utumaji, upokeaji pamoja na uhifadhi wa hela, pia ajira.
Pia nikatoa na tahadhari na namna mbalimbali watu wanavyolizwa.
au mkuu wewe ni mojawapo ya hao walizaji so nimegusa anga zako nin??

hata mimi nahisi umegusa interest zake otherwise sioni kwa nini amekereka!
 
Namba moja sijaielewa vyema inavyofanyika
Nakuja kama mteja kwako na kuanza kusifia products zako,
Kukupa kichwa zaidi nakuambia ningependa tupeane contacts hivyo nachukua simu yako ili ni-save namba yangu kwako, na hapo ndipo keusi-kekundu inapofanyika.
Kwani badala ya kujisevu jina, naji-save kama "tigopesa".
Nkishachukua mzigo na-draft msg kama zile za tigopesa za " Umepokea kiasi cha tshs .... kutoka kwa...." na kukutumia,
Hiyo msg nkikutumia itaandika imetoka " tigopesa" kwani ndivyo nlivyoji-save kwako.
 
yote tahadhari nzuri sana ila pia kuna wakala wanakuwa ktk tinted rooms na akipokea pesa anadrop kiasi na kusema haitosh
 
Ujio wa Hizi huduma za kifedha kupitia simu za Mikononi ukiacha kurahisisha uchukuaji, utumaji, uhifadhi na uwekaji wa Fedha, pia umetengeneza Ajira kwa watu wengi tu ambao labda kabla yake wangekua vijiweni tu.

Lakini pia ujio huu wa hizi huduma umekuja pia na utapeli wa aina ya juu, na wengi wamelizwa kupitia hizi huduma. Labda tu tupeane tahadhari jinsi huo utapeli unavyofanyika ili angalau tuweze kujikinga.

1)KUSEVU NAMBA KAMA TIGOPESA/M-PESA
Utapeli huu unafanyika kwa anaejifanya Mteja kuchukua simu ya muuzaji kisha akaisevu namba yake kama Tigo-Pesa kwenye simu ya muuzaji. Haya yanaweza kufanyika pale ambapo mteja feki anajifanya anataka kutengeneza mawasiliano zaidi na muuzaji.
Kinachofuata ni yeye kutuma msg kwa muuzaji kwamba "Umehamishiwa kiasi cha Tshs...... Kutoka kwa...." ambapo msg hiyo itajionyesha imetoka Tigopesa na mteja/tapeli kuchukua mzigo.

2)CANCEL TRANSACTION THROUGH CUSTOMER CARE
Hii inafanyika kwa mtumaji hela kununua mzigo na kutuma Tigopesa halali, kinachofuata ni kua mkiachana tu mnunuaji/tapeli anapiga simu Customer Care na kusema kua ametuma wrong number hivyo anaomba a-cancel transaction huku akiwa kshaondoka na mzigo.

3) HAMISHA HELA KUPATA JINA KISHA FREEZE NAMBA
Mbinu hii inatumika kwa Tapeli kuhamisha japo alfu 2 mradi tu apate jina la mtumiaji wa hiyo namba baada ya kuhamisha.
Kinachofuata ni Tapeli kwenda kwenye kibanda cha tigopesa na kujifanya yeye ndio mwenye namba hiyo nmba Na jina lake ndilo hilo na kaipoteza hivyo anaomba kui-freeze ili afunguliwe ingine.
Baada ya hapo, tapeli akiwa na laini ya wizi anaanza kutuma msg kujifanya amekwama hivyo anaomba asaidiwe.
Mbinu hii ili ifanikiwe inabidi amlainishe sana mwenye kibanda, ikiwezekana hata kumhonga ili aweze kupata namba mbalimbali zilizowasiliana na hiyo laini.

Wakuu wangu ni haya tu ningependa tu-share kwa leo.
Shark

good work! it happens
 
Tahadhari ni nzuri lakini kitendo cha kumpa mtu simu yako asevu namba yake ni mtindo wa zamani au itokee kwa mtu mnayefahamiana naye sana, na hata hivyo bado utaitwa mzembe kwa kuwa hiyo namba yako kwa kawaida ni kama benki hivyo ni sawa na kutoa taarifa za account yako ya benki kwa stranger bila sababu za msingi.

Ushauri:Kwenye masuala ya pesa kuaminiana ni mwanzo wa matatizo! Hivyo kila mtu anapaswa kuchukua tahadhari ili mambo yasiyotazamiwa yasitokee.
 
Nilishitushwa kidogo wakati nipipoanza kutumia hizo huduma hapo juu sana sana upande wa namba ya siri yaani password. Kikawaida kabisa hata computer iliyotoka miaka ya 70 ikikuambia uingize password ni huwa hiyo password haitokei kwenye screen, kinachotokea ni **** , lkn cha kushangaza wakati natumia hizo huduma hapo juu inakuambia ingiza number ya siri, Ukiingiza mfano 7888 inatokea kama ilivyo kwenye screen, hii ni hatari sana, kwa sababu hapa hakuna usiri tena. Ninawasifu airtel money kwa sababu wakikuambia ingiza password huwa inatokea * na sio number,
Kuna kitu kimenisukuma niandike hivi, jizu nilikuwa kwenye duka moja akaja dada mmoja akawa anafanya transaction na wote tulikuwa tumesimama sehemu moja, sasa wakati anaandika no ya siri nikaiona kabisa na tena nikawa nimeikariri ni number nne tuu ambazo mtu anaweza kuzikariri,
Kama no unaandika na inatokea kwenye screen nadhani hiyo siyo no ya siri tena.
Yule dada alivyoondoka nikawa ninaongea na yule muuza duka, yeye alichoniambia ni kwamba anajua password karibia zote za wateja wake sana sana wa TIGO-PESA NA M-PESA, lakini wa Airtel Money ni ngumu kukariri, akasema wateja wake wengi huwa wanampa simu zao na kisha wanamwambia awatolee shilingi ngapi! Yeye anadai wakati unaandika no ya siri na ikatokea kwenye screen ni rahisi zaidi kuikariri kuliko ikitokea ****.
USHAURI
-Ni vema hayo makampuni hapo juu ya kuangalia ni jinsi gani ya kuficha no ya siri ya mteja wake! No ya siri kutokea kwenye screen sio standard kabisa
-Vile vile kuwe na utaratibu wa lazima wa kubadilisha passowrd kila baada ya muda fulani. Hii itasaidia sana watu kutokariri passowrd za watu
 
Du hao watu wa IT na masystem wa hayo makampuni watakuwa vilaza yani hakuna kabisa encription of data?
 
Hapo umenena mkuu,hawezi kusema ni NO ya siri,halafu wao wanashindwa kuzificha,mbaya zaidi maduka tuendayo kutoa hela.ndiyo hayo hayo tulio wengi tunaenda kuchaji simu zetu.hatari sana.
 
Hapo umenena mkuu,hawezi kusema ni NO ya siri,halafu wao wanashindwa kuzificha,mbaya zaidi maduka tuendayo kutoa hela.ndiyo hayo hayo tulio wengi tunaenda kuchaji simu zetu.hatari sana.

Tumia PIN ili isiwe rahisi kufungua simu yako mtu asiyeijua hiyo PIN.Vinginevyo bila kuwa makini utaibiwa sana.
 
Hapo
umenena mkuu,hawezi kusema ni NO ya siri,halafu wao wanashindwa
kuzificha,mbaya zaidi maduka tuendayo kutoa hela.ndiyo hayo hayo tulio
wengi tunaenda kuchaji simu zetu.hatari sana.

kibaya zaidi wengi hutumia mwaka wa kuzaliwa kama namba ya siri!
 
Naona kama wewe ndio Unaropoka, nimetoa advantages za hizi huduma kama vile kurahisisha utumaji, upokeaji pamoja na uhifadhi wa hela, pia ajira.
Pia nikatoa na tahadhari na namna mbalimbali watu wanavyolizwa.
Au mkuu wewe ni mojawapo ya hao Walizaji so nimegusa anga zako nin??

ha! Ha! Ha! Umemwaribia deal lake
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom