muhubiri mpya
Member
- Sep 14, 2019
- 19
- 10
Naomba nianze kwa kuwasalimu, habari za wakati huu
Kwa zaidi ya nusu muongo nimekuwa nikifuatilia mijadala ya huku ndani JF nimekuja kugundua kuwa Taiifa hili na Afrika kwa ujumla tuna hazina kubwa ambayo hatuitumii kabisa
Naomba nianze kwa kusema kuna tofauti kubwa ya mtawala na kiongozi, kiongozi anaweza kuwa mtawala lakini mtawala kwa namna yoyote hawezi kuwa kiongozi
Kuna tofauti nyingi sana kati ya mtawala na kiongozi Ila naomba niseme chache tu, mtawala huona kuwa ni yeye pekee anastahili kushika wadhifa "x" wakati kiongozi huona ana wajibu wa kufanya kitu kwa ajili ya kuandaa watu wa kuchukua wadhifa "x", mtawala huwasaidia watu anaowajua na hao ndio hula nao kwenye wadhifa "x" kiongozi hutafuta watu wote ambao wanaweza kuuboresha kwa pamoja wadhifa "x"
Mtawala hujijenga yeye badala ya wadhifa "x" kiongozi hujenga wadhifa "x" badala ya yeye. Leo hii akiinuka kijana yoyote mwenye uwezo wowote kuliko watawala ujiandae kuishi maisha ya mateso ,hicho ndicho kilichotokea kwa Julius Marema wakati akiwa ndani ya ANC, hicho kinachosababisha mawazo ya Tundu Lissu kutokuchukuliwa
Hicho ndicho kilipelekea kuzaliwa kwa ACT-wazalendo baada ya zito kukabwa kila upande ndani ya chadema, hicho ndicho kinachopelekea Robert Kyagulanyi kuteseka ndani ya nchi yake ya Uganda, ndicho kinapelekea Paul Kagame aamini anaayo hati milki ya Rwanda
Ubinafsi na roho hii ya "utawala" inasababisha watu ambao wangekuwa viongozi kutembea mtaani huku watawala wakijifanya viongozi, hii imepelekea wanasayansi wakubwa ambao wapo afrika kufa wakiwa na mawazo ya kuwa wanasayansi, imepelekea watu wenye mawazo makubwa ya kuibadili Afrika kufa na mawazo yao au kuzuiliwa mawazo yao kuonekana na mtu yeyote
Hii ndio inayopelekea watu kuwaogopa watawala wa kiafrika badala ya kuogopa katiba na Sheria za nchi zao, hii inapelekea watu wenye kulijenga Taifa hili kuwa wanafiki sana wakisaidia kuwajenga watawala badala ya kujenga taifa na mfumo kiujumla. MUNGU ibariki Tanzania MUNGU ibariki afrika
Kwa zaidi ya nusu muongo nimekuwa nikifuatilia mijadala ya huku ndani JF nimekuja kugundua kuwa Taiifa hili na Afrika kwa ujumla tuna hazina kubwa ambayo hatuitumii kabisa
Naomba nianze kwa kusema kuna tofauti kubwa ya mtawala na kiongozi, kiongozi anaweza kuwa mtawala lakini mtawala kwa namna yoyote hawezi kuwa kiongozi
Kuna tofauti nyingi sana kati ya mtawala na kiongozi Ila naomba niseme chache tu, mtawala huona kuwa ni yeye pekee anastahili kushika wadhifa "x" wakati kiongozi huona ana wajibu wa kufanya kitu kwa ajili ya kuandaa watu wa kuchukua wadhifa "x", mtawala huwasaidia watu anaowajua na hao ndio hula nao kwenye wadhifa "x" kiongozi hutafuta watu wote ambao wanaweza kuuboresha kwa pamoja wadhifa "x"
Mtawala hujijenga yeye badala ya wadhifa "x" kiongozi hujenga wadhifa "x" badala ya yeye. Leo hii akiinuka kijana yoyote mwenye uwezo wowote kuliko watawala ujiandae kuishi maisha ya mateso ,hicho ndicho kilichotokea kwa Julius Marema wakati akiwa ndani ya ANC, hicho kinachosababisha mawazo ya Tundu Lissu kutokuchukuliwa
Hicho ndicho kilipelekea kuzaliwa kwa ACT-wazalendo baada ya zito kukabwa kila upande ndani ya chadema, hicho ndicho kinachopelekea Robert Kyagulanyi kuteseka ndani ya nchi yake ya Uganda, ndicho kinapelekea Paul Kagame aamini anaayo hati milki ya Rwanda
Ubinafsi na roho hii ya "utawala" inasababisha watu ambao wangekuwa viongozi kutembea mtaani huku watawala wakijifanya viongozi, hii imepelekea wanasayansi wakubwa ambao wapo afrika kufa wakiwa na mawazo ya kuwa wanasayansi, imepelekea watu wenye mawazo makubwa ya kuibadili Afrika kufa na mawazo yao au kuzuiliwa mawazo yao kuonekana na mtu yeyote
Hii ndio inayopelekea watu kuwaogopa watawala wa kiafrika badala ya kuogopa katiba na Sheria za nchi zao, hii inapelekea watu wenye kulijenga Taifa hili kuwa wanafiki sana wakisaidia kuwajenga watawala badala ya kujenga taifa na mfumo kiujumla. MUNGU ibariki Tanzania MUNGU ibariki afrika