Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,011
- 144,371
Kwa jinsi uchaguzi huu ulivyofanyika,kuna kila dalili Wahisani na Mashirika ya Fedha ya Kimataifa yatatutenga ukizingatia tumepuuza wito wa wahisani wa kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki.
Kwahiyo, kitachofuata ni serikali hii kuanza kukwama katika utekelezaji wa miradi yake mbalimbali na hivyo wataanza kutafuta mahali pa kuelekeza lawama na hapo ndio wapinzani watapoanza kubebeshwa lawama wakati chanzo ni wao wenyewe kushindwa kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki.
Huko Bungeni hata wakiwa ni wao watupu,wataanza kuwajadili wapinzani ambao watakuwa hawamo kwa kuwalaumu na kuwabebesha lawama ambazo haziwahusu kwa.hoja kwamba ndio wanaosababisha serikali ikose mikopo na misaada na kutaka Watanzania wawaone wapinzani kuwa ndio chanzo cha wao kushindwa ku-deliver.
Narudia,baada ya kuwahujumu wapinzani na Bunge lote wakalitawala wao, bado Mbowe, Lissu, Lema, Sugu, Zitto na wapinzani wengine wataendelea kujadiliwa humo Bungeni na kubebeshwa lawama zisizowahusu wakati serikali itakuwa ni yao na Bunge pia litakuwa ni lao.
Hivi sasa kiu yao ni kutaka kuona wapinzani, hasa CHADEMA na ACT , hawaingii Bungeni lakini hilo likitimia, bado wataendelea kuhangaika tu kwani hata nafsi zao zitakuwa zinawasuta huku matatizo ya wananchi yakibaki pale pale na si ajabu hali ikawa mbaya zaidi.
Wataanza kuwaza 2025 tutawaambia mini wananchi kama Bunge lote lilikuwa lao na serikali pia ilikuwa yao hivyo lazima watengeneza propaganda mradi tu waelekeza lawama kwa wapinzani.
Tukumbuke wamekuwa wakiwalaumu wapinzani kupinga kila kitu Bungeni na kukwamisha maendeleo majimboni, hivyo sasa watakuwa ni kibarua cha kuthibitisha kwa vitendo kuwa wapinzani ambao walikuwa hawakusanyi kodi, ndio kweli walikuwa kikwazo kuanzia Bungeni mpaka kwenye majimbo.
Wameshavuruga uchaguzi na kwahiyo Bunge liktakuwa lao ila mjue tu bado wataendelea kusakama wapinzani ambao si tu hawatakuwapo Bungeni, bali pia watakuwa hawaruhusiwi kufanya hata siasa.
Na baada ya kuwaondoa wapinzani wa kweli Bungeni, msishangae wakarudisha na Bunge live, Bunge litalokuwa na kazi ya kusifu na kutukuza kama ilivyo TBC.
Time will tell.
Kwahiyo, kitachofuata ni serikali hii kuanza kukwama katika utekelezaji wa miradi yake mbalimbali na hivyo wataanza kutafuta mahali pa kuelekeza lawama na hapo ndio wapinzani watapoanza kubebeshwa lawama wakati chanzo ni wao wenyewe kushindwa kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki.
Huko Bungeni hata wakiwa ni wao watupu,wataanza kuwajadili wapinzani ambao watakuwa hawamo kwa kuwalaumu na kuwabebesha lawama ambazo haziwahusu kwa.hoja kwamba ndio wanaosababisha serikali ikose mikopo na misaada na kutaka Watanzania wawaone wapinzani kuwa ndio chanzo cha wao kushindwa ku-deliver.
Narudia,baada ya kuwahujumu wapinzani na Bunge lote wakalitawala wao, bado Mbowe, Lissu, Lema, Sugu, Zitto na wapinzani wengine wataendelea kujadiliwa humo Bungeni na kubebeshwa lawama zisizowahusu wakati serikali itakuwa ni yao na Bunge pia litakuwa ni lao.
Hivi sasa kiu yao ni kutaka kuona wapinzani, hasa CHADEMA na ACT , hawaingii Bungeni lakini hilo likitimia, bado wataendelea kuhangaika tu kwani hata nafsi zao zitakuwa zinawasuta huku matatizo ya wananchi yakibaki pale pale na si ajabu hali ikawa mbaya zaidi.
Wataanza kuwaza 2025 tutawaambia mini wananchi kama Bunge lote lilikuwa lao na serikali pia ilikuwa yao hivyo lazima watengeneza propaganda mradi tu waelekeza lawama kwa wapinzani.
Tukumbuke wamekuwa wakiwalaumu wapinzani kupinga kila kitu Bungeni na kukwamisha maendeleo majimboni, hivyo sasa watakuwa ni kibarua cha kuthibitisha kwa vitendo kuwa wapinzani ambao walikuwa hawakusanyi kodi, ndio kweli walikuwa kikwazo kuanzia Bungeni mpaka kwenye majimbo.
Wameshavuruga uchaguzi na kwahiyo Bunge liktakuwa lao ila mjue tu bado wataendelea kusakama wapinzani ambao si tu hawatakuwapo Bungeni, bali pia watakuwa hawaruhusiwi kufanya hata siasa.
Na baada ya kuwaondoa wapinzani wa kweli Bungeni, msishangae wakarudisha na Bunge live, Bunge litalokuwa na kazi ya kusifu na kutukuza kama ilivyo TBC.
Time will tell.