Watanzania wote; Tuombe Mungu wageni waendelee kubaki ;wef ulikuwa wapi jamani?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Kwa yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika natamani VOLCANO IENDELEE KUTOKEA WAKOSE SAFARI ZA NDEGE WAENDELEE NA MIKUTANO YAO...

Watanzania wote mnaombwa hizi siku 4 ni za kumuomba MUNGU aendelee kuwapa moyo wageni
wetu pale mliman city waendelee kubaki na kila wanachopanga kumaliza kwa siku wasifanikiwe
waweze kuongeza siku hapa nchini kwetu..kwa hotuba ya JK wanajitegemea kila kitu naamini...
hakuna hasara tunayopata kwa jamaa zetu hawa.....,kwa niaaba ya watanzania wenye mapenzi mema kwa nchi yao ewe mtanzania ukiwa nje ya nchi ndan ya Tanzania leo usiku kesho keshokutwa
siku maalumu kuwaombe watu hawa waendelee kula raha na huku na sisi tunakula raha kwa mambo mengi tu tunayotendewa na serikali kwa ujio huu

1),MASHIMO KUFUKIWA YALIOKAA MIEZI ZAIDI YA SITA

2)WATU KUONGEZEKA KUMUABUDU MUNGU IBADA ZA ASBH KWA KUWAHI MAPEMA NA KUSHINDWA KUINGIA KAZINI NA HIVYO KUMKUMBUKA MWENYEZI MUNGU

3)MUNGU AMEWAONYESHA SERIKALI KILIO CHA WATANZANIA CHA MUDA MREFU AMBACHO RAIS KIKWETE AJAWAHI KUKUTANA NACHO CHA FOLEN BARABARAN KWA KUONGOZWA NA KINGORA..HUKU WALIOWAH BARABARAN WAKIKAA PEMBENI....HAKUNA SIKU NILIOFURAH KAMA LEO HII NA SIKU 4 ZIJAZO..JAMANI BARABARA KILA UKIPITA ASKARI WANA JEZI MPYA SIJUI TRAFFIC WAMEPEWA JEZI MPYA AMA WAMEAMUA KUFUA NA BLICHI JAMANI..KILA UKIKARIBIA TRAFFICLIGHT NI UNAITWA NA TRAFFIC NA NIKWAMBIE YAANI KILA JUNCTION N WAWILIWAWILI TU WALA SI WENGI....AMANI MPAKA NYUMBAN KUMRADHI SIJUI UKIWA UNAINGIA KWAKO KAMA YALE MASHIMO YA MVUA YAMEFUKIWA KAMA BADO OMBA MUNGU AWAPITISHE WAGENI HUKO MTAKUMBUKWA KUFUKIWA MASHIMO..KAMA YA BP,LUGALO...KWELI SHETAN HANA ADABU MIEZI ZAIDI YA SITA LEO TUNAFUKIWA MASHIMO ...LOH..KAMA NI PEPO LILIWABANA KUANZIA RAIS MPAKA WAZIRI WA MIUNDOMBINU KWA WADADISI WA MAPEPO SIJUI HILI LINAITWAJE....LABDA TULIITE PEWEF

4)JAMANI JIJI LA DAR LIMEKUWA SAFI..YANI SIAMINI WAZIRI MKUU AMEAMUA KUKAGUA JIJI LA DAR TANGU ACHAGULIWE KISA WEF..JAMA WEF WEWE ULIKUWA WAPI..MBONA TUNAKUTAMANI HIVI
EEE MOLA WAONGEEZEE SIKU WASHINDWE KUMALIZA MIKUTANO YAO WALIVYOPANGA
 
Matrafiic kungaa barabaran na sare zao mpya..yaani kwa kweli tunawapongeza sana kwa hili
ombi langu haya mnayoyafanya laiti mngekuwa mkifanya hata kila sikuu kuu tungewashukuru kama nyerere day,,xmass,pasaka idd zotee.bila shaka akuna angewalalamikia...anyway bado mna miezi 6 kujirekebisha ..
 
Hilo la kusemwa ni Kikwete nakushauri usiliamini maana hanauzoefu wa kusema ukweli, alituambia Sullivan walikua wanaleta hela akaita summit of the decade lakini si tumeyaona? serikali imelipia 50% mpaka leo watu wanalia na wizara yamambo ya nje hawajalipwa wametumika kumuwezesha rais kujikomba kwa wachovu wa Sullivan, eti wawekezaji, si mmeona hata akinda marekani anaokutana nao? wakuu wa mashirika ya UN wanaolipwa mshahara, sullivan weusi wenzenu nao wanaomba pesa za kujikimu ndio katuletea wawekezaji, wanaochangishana dola mia tatu mia tatu, CHEAP STAFF! na bado hebu msomeni mzee genuine wa kitanzania bibi Asha kutoka kisarawe kwenye mwananchi ya May 5, huyo ndio anayestahili kuitwa mzee wa kitanzania sio lile kundi la terere wasiojua kula yao, watoto na wajukuu wao itatoa wapi kesho yake wanakubali kutumiwa kuisaliti nchi hii.
 
Kuna kitu aliniambia zamani kidogo mzee Bomani. Huu ulikuwa wakati wa ziara ya Kissinger Dar-es-Salaam. Alikuwa amefikia hoteli ya Kilimanjaro, wakati huo akiwa balozi wetu Washington. Anasema wakati huo hakuwa na shida ya kupata simu ya kupiga nje, lakini baada ya Kissinger kuondoka tu, laini zote za simu Tanzania zilikuwa hazipatikani. Kwa hiyo mnaosema wageni wetu wa WEF waendelee kubaki Tz naelewa mnachokisema. Lakini hii pia inaonyesha kuwa uwezo wa kufanya tunao. Sasa kitu gani kinatuzuia kuendeleza mazuri haya hata baada ya wageni wetu kuondoka?
 
Kuna kitu aliniambia zamani kidogo mzee Bomani. Huu ulikuwa wakati wa ziara ya Kissinger Dar-es-Salaam. Alikuwa amefikia hoteli ya Kilimanjaro, wakati huo akiwa balozi wetu Washington. Anasema wakati huo hakuwa na shida ya kupata simu ya kupiga nje, lakini baada ya Kissinger kuondoka tu, laini zote za simu Tanzania zilikuwa hazipatikani. Kwa hiyo mnaosema wageni wetu wa WEF waendelee kubaki Tz naelewa mnachokisema. Lakini hii pia inaonyesha kuwa uwezo wa kufanya tunao. Sasa kitu gani kinatuzuia kuendeleza mazuri haya hata baada ya wageni wetu kuondoka?
Wow, Jasusi wewe sasa hivi lazima ni "Senior Citizen".
 
hilo la kusemwa ni kikwete nakushauri usiliamini maana hanauzoefu wa kusema ukweli, alituambia sullivan walikua wanaleta hela akaita summit of the decade lakini si tumeyaona? Serikali imelipia 50% mpaka leo watu wanalia na wizara yamambo ya nje hawajalipwa wametumika kumuwezesha rais kujikomba kwa wachovu wa sullivan, eti wawekezaji, si mmeona hata akinda marekani anaokutana nao? Wakuu wa mashirika ya un wanaolipwa mshahara, sullivan weusi wenzenu nao wanaomba pesa za kujikimu ndio katuletea wawekezaji, wanaochangishana dola mia tatu mia tatu, cheap staff! Na bado hebu msomeni mzee genuine wa kitanzania bibi asha kutoka kisarawe kwenye mwananchi ya may 5, huyo ndio anayestahili kuitwa mzee wa kitanzania sio lile kundi la terere wasiojua kula yao, watoto na wajukuu wao itatoa wapi kesho yake wanakubali kutumiwa kuisaliti nchi hii.
kwa hili naomba nikubaliane na wewe maana kikwete ni muongo sana maana ukienda kufuatilia vizuri si ajabu pesa iliyotoka kwetu kugharamia mkutano huu ni nyingi kuliko mapato anayotaka kutuaminisha kuwa tutayapata.
Si ajabu tunagharimia kila kitu lakini ni "siri kali".
 
Back
Top Bottom