Isanga family
JF-Expert Member
- Feb 25, 2015
- 14,579
- 25,650
Maroli yanayotakiwa kupakia mazao kijijini Kodi ipo juu hayo magari yanayotumika kubeba watalii Kodi ipo juu unawezaje kuchochea uchumi wakati watu wako hawana kipato na hawawezeshwi kufanya hivyo...Nchi imegubikwa na upigaji wa kiwango cha juu mno mwezi January watu walijiongezea Kodi ya magari bila bunge kuhidhinisha leo Mama anataka ukaguzi wa hizo fedha ni kweli ndege zinaweza kuchochea uchumi kukua ila ukinunua kwa mkupuo hivyo hasara utaiona na sijui kama zina route za kueleweka zaidi ya kuambiwa abiria wa chato wamejaa...Nilikuwa nimepanga kutokujihusisha na mijadala ya kisiasa, imebidi nijitokeze katika huu mjadala.
Mjadala huu umechukua sura ya kisiasa hasa baada ya ripoti ya CAG kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara.
Mleta mada kaliweka suala la ATCL kiuchumi zaidi ila wewe Eyce unatafuta majibu ya hoja zako kisiasa.
Tanzania katika awamu mbalimbali za Serikali zimekuwa na mikakati ya msingi ya kiuchumi. Sera ya Kilimo kwanza ilikuwa na inakusudia kujitosheleza kwa kilimo. Sera ya viwanda inakusudia kujitosheleza kwa bidhaa muhimu kwa mahitaji ya kila siku na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Ili kufanikisha hayo imelazimika kuimarisha miundo mbinu dhabiti ya usafirishaji (ardhini, majini na angani) kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Wengi wetu humu JF hatujui vichocheo vya kiuchumi na hata kama tunajua, kwa sababu tunazozijua, tunajitokeza kubeza ununuzi wa ndege. Nina uhakika miaka ijayo faida ya kununua ndege zetu wenyewe leo itakuwa dhahiri.
Kwa mfano, baada ya kujitosheleza chakula na bidhaa, Sera ijayo ni ya uuzaji bidhaa nje ya nchi. Hili haliwezi kufanikiwa kwa faida bila kuwa na usafiri wa anga ulio imara. Kama utakumbuka hadi leo mazao yetu na madini husafirishwa kupitia Kenya, je, tuendelee hivyo hivyo kwa bidhaa za viwanda vyetu vinavyojengwa?