Watanzania wenzangu, biashara ya usafiri wa anga (ndege) sio kama Uber jamani

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
244
312
Tunapoambiwa ATCL imepata hasara tusibeze sana. Kuna American Express na Delta Lines wanachungulia kaburi! Na Amar hapo UK British Airways imegubikwa madeni nusura izame! Tatizo lenu ni uzungu pori? Ni mashirika ya wenye mafuta kina EMIRATES, QATAR na wenzao Serikali zao zimenunua madeni. Baadhi ya matukio yaliyotikisa biashara ya usafiri wa anga duniani kwa kipindi Cha miaka 15 iliyopita:

1. Global Economic and financial crisis (mtikisiko wa kiuchumi na kifedha ulioikumba dunia).
2. Marubani, wahudumu na watumishi viwanjani kugoma Mara kwa mara nchini Marekani, UK, France na Italy.
3. Kodi mpya (carbon tax) kugharamia uchafuzi wa anga.
4. Covid 19 restrictions on travel (masharti ya covid 19)
5. Gharama za utengenezaji ndege kuongezeka mno kutokana na ushindani Kati ya Airbus na Boeing kufuatia mahitaji ya usalama wa abiria.
6. Nchi kunyimana route (protectionism policies).
7. Uendeshwaji mbaya wa airline
8. Kubadilika kwa sura ya utalii. Mfano watalii wengi kuanza kujikita kutembelea nchi au eneo lao, kushuka ari ya kuona wanyama au milima n.k.

Hizi ndio sababu ya mashirika mengi duniani kuendeshwa kwa hasara. Sio lazima éti hasara pawepo na wizi

Licha ya mashirika kufanya vibaya hakuna nchi imefunga shirika lake. KLM ilitaka ijiuze kwa AIR FRANCE wananchi wakaandamana! Serikali ikalazimika kubeba madeni.

Alitalia ya Italy ilitangazwa imefilisika Papa akamwandikia barua Prime Minister kwamba Vatican hairidhii uamuzi! Serikali ikabeba Madeni. Mpaka leo Alitalia ipoipo tu. Ukipatiwa ticket ya Alitalia jiandae for cancellation wakati wowote. Mara nyingi watakuhalishia Easy Jet au Ryan Air.

Sasa kuna mijitu inadhani biashara ya ndege sawa na biashara ya kuuza mashokishoki Darajani!
😊
 
Ohh ndio maana nilisikia nchi nyingi hazijihusishi directly zaidi ya kuachia mashirika binafsi kama precision air na fastjet wafanye hiyo biashara ili fedha za serikali zifanye mambo mengine yanayoleta impact kubwa kiuchumi.

By the way, Ningeomba unipe uelewa, je kama nchi tunapata faida gani kubwa mbali na "national pride" , inayotufanya tuservice hilo deni kuliko kuwekeza katika sekta nyingine.
 
Wewe unaongea nini?. Mtu yoyote anapofungua biashara anategemea faida. Sasa kama biashara inajiendesha kwa hasara kuna haja gani ya wewe kuendelea kuifanya hiyo biashara au kuingia kwenye hiyo biashara?

Mimi nilifikiri wewe utakuja na ufafanuzi kwamba kwa nini lazima tuendelee kufanya hii biashara,hata kama inajiendesha kwa hasara. Sio sawa na kuuza mashokishoki pale darajani,lakini tupe faida yake katika hizo hasara. Je, tuendelee kufanya biashara inayoingiza hasara?
 
Tunafahamu vizuri sana kuwa kuendesha biashara ya usafiri wa anga ni ngumu sana hadi wazungu huwa wanasalimu amri,lakini swali la kujiuliza ni kwamba ilikuwa vipi mtu mwenye PhD akabadilika kuwa bumunda na kuanza kuwekeza hela nyingi sana katika biashara hiyo badala ya kupeleka hela kwenye maji,barabara,umeme,afya,elimu na kadhalika ambayo bado ni matatizo sugu ndani ya miaka zaidi ya 50 ya uhuru?
 
Ila marehemu alijua kucheza na akili za watu sijui aliwaroga kuna siku watuvl wataenda chato kupiga fimbo kaburi
 
Na ndiyo Watanzania wengi tulichokisema kwamba kununua ndege si KIPAUMBELE cha Watanzania. Kwanza wenye uwezo wa kusafiri na ndege nchini ni asilimia ndogo sana kutokana na gharama kubwa za usafiri huo na hata nje ya Nchi competition ni kubwa sana na mashirika yaliyokuwepo kabla ya ATCL kuanza rasmi kama vile Kenya Airways na Rwanda Airlines yalikuwa yanaingiza hasara kubwa sana wakati ule na hadi hii leo. Dikteta angesikia ushauri wa Watanzania asingethubutu kununua ndege hata moja, sasa inakula kwetu.
 
Mkuu hatukatai kuwa biashara ya Ndege ina hasara. Tunachoshangaa ni hivi:
1.Kwanini tuongopewe kwa miaka 5 mfululizo???
2.Kwanini ndege inunuliwe kama biashara ya machungwa???
3.Kwanini Alhaj Assad alifukuzwa aliposema ukweli???
4.Je, Huoni kuwa hata miradi mingine ya st.John Pombe tumepigwa???
5.Hao wanaofilisika huwa na ndege chache kama zetu???
Majibu yako ni muhimu
 
Mbona kama unawaelewesha watu ambao tayari wameshaelewa na hakuna sababu ya argument nadhan kwa ATCL case yake hipo hapo kwenye no 7 hilo halina ubishi hayo mengine yote ni ziada tu!!!!!!
 
Back
Top Bottom