David Goliath
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 926
- 1,790
Habari zenu wakuu,
Bila kupoteza mda niende kwenye hoja yangu, miaka ya hivi karibuni kumekua na utitiri wa radio nyingi za masafa ya FM, kama tunavyojua dhima kubwa ya vyombo vya habari ni kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha jamii.
Kwa upande wa Redio zetu za Tanzania vipindi vya michezo vimepewa kipaumbele kuliko jambo lolote wanajadili michezo kuanzia asubuhi, mchana, jioni, usiku tuseme Taifa nikama halina jambo lingine linalofaa kupewa kipaumbele kujadiliwa zaidi ya michezo.
Wananchi nao muda wote wapo bize kujadili mpira iwe kwenye vyombo vya usafiri, sehemu za biashara, makazini, majumbani Hadi mashuleni, wakati nchi ina matatizo chungu nzima wanafunzi vyuo vikuu wanakosa mikopo.
Hali ya elimu kuanzia shule za msingi hadi vyuoni zinatia huruma, masoko ya wakulima hali ni mbaya, huduma za kijamii kama maji, afya, umeme ni tabu tupu kwenye upande wa mambo ya upatikanaji wa haki masuala ya sheria Bado ni Giza, lakini yote hayo tumeyapa kisogo tumejikita kujadili na kuchambua mpira kana kwamba Taifa halina mahitaji mengine, Kwa upande wangu naona kama hii siyo sawa, kwenu wadau.
Bila kupoteza mda niende kwenye hoja yangu, miaka ya hivi karibuni kumekua na utitiri wa radio nyingi za masafa ya FM, kama tunavyojua dhima kubwa ya vyombo vya habari ni kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha jamii.
Kwa upande wa Redio zetu za Tanzania vipindi vya michezo vimepewa kipaumbele kuliko jambo lolote wanajadili michezo kuanzia asubuhi, mchana, jioni, usiku tuseme Taifa nikama halina jambo lingine linalofaa kupewa kipaumbele kujadiliwa zaidi ya michezo.
Wananchi nao muda wote wapo bize kujadili mpira iwe kwenye vyombo vya usafiri, sehemu za biashara, makazini, majumbani Hadi mashuleni, wakati nchi ina matatizo chungu nzima wanafunzi vyuo vikuu wanakosa mikopo.
Hali ya elimu kuanzia shule za msingi hadi vyuoni zinatia huruma, masoko ya wakulima hali ni mbaya, huduma za kijamii kama maji, afya, umeme ni tabu tupu kwenye upande wa mambo ya upatikanaji wa haki masuala ya sheria Bado ni Giza, lakini yote hayo tumeyapa kisogo tumejikita kujadili na kuchambua mpira kana kwamba Taifa halina mahitaji mengine, Kwa upande wangu naona kama hii siyo sawa, kwenu wadau.