Watanzania wana kiu kikubwa cha kuitoa CCM, Je tatizo ni nini?

Mimi siwezi kuupigia kelele ufisadi. Na wala sijaneemeka na ufisadi. Mwenyezi mungu amenibariki kwa namna moja au nyingine kuweza kupata kipato cha halali kinachotokana na jasho langu
.
Na nimebahatika kusafiri nchi kadhaa na kuishi nchi kadhaa (sio kama najidai, maana mtaanza hizo) na nimeona karibu kila nchi ufisadi upo kwenye siasa tena wa hali ya juu.

Nipo states sasa hivi na ukisikia ufisadi uliopo jeshini la marekani, with evidence unaweza shangaa, ufisadi uliopo wall street, ufisadi unaofanywa na serikali za uingereza, China n.k ni humungous!!... but hey, it is what it is.

Kama wewe BAK ukiiba bilioni mia moja na ukaanzisha shirika lako la reli na kupatia wananchi usafiri wa maana toka Dar mpaka mwanza, mpanda, kigoma etc... mimi wala sitakumind, ni wapuuzi wanaoiba halafu hamna cha maana kinachoendelea ndio labda nitawamind, ila hiyo siyo kazi yangu.

Kama unataka research papers kuhusu democracy and opposition in Tanzania, unaweza kula nondo hii hapa chini, kutoka Georgetown University (kama mvivu wa kusoma just scroll to page 5, halafu nenda kwenye conclussion).

Tanzania's Missing Opposition ---

Utawezaje kuupigia kelele ufisadi na ilhali wewe ni mamluki/fisadi/anayeemeka kupitia migongo ya mafisadi? Huna mapenzi ya kweli na nchi yetu ndio maana madudu yanayofanywa na Serikali ya magamba inayoongozwa na Kikwete huyaoni.

Bahati mbaya sina jadi ya wizi hivyo wazo lako hilo chafu kwamba mimi nitaiba liondoe kichwani mwako. Nakula nguvu yangu na wala sijawahi kumdhulumu mtu au kufanya ufisadi na wala sifikirii kufanya hivyo na nashukuru Mungu kwa kunijaalia maisha mazuri.

Sihitaji kula nondo ya mtu yeyote yule mi Mtanzania banaa!!! Naifahamu vizuri sana nchi yangu. Naona unajibaraguza baraguza tu lakini maswali yangu kuhusu huu utafiti uchwara unayapiga chenga, kama huna majibu ni bora tu useme kwamba sina majibu badala ya kuendelea kuyakwepa.

 
:msela:
Utawezaje kuupigia kelele ufisadi na ilhali wewe ni mamluki/fisadi/anayeemeka kupitia migongo ya mafisadi? Huna mapenzi ya kweli na nchi yetu ndio maana madudu yanayofanywa na Serikali ya magamba inayoongozwa na Kikwete huyaoni.Bahati mbaya sina jadi ya wizi hivyo wazo lako hilo chafu kwamba mimi nitaiba liondoe kichwani mwako. Nakula nguvu yangu na wala sijawahi kumdhulumu mtu au kufanya ufisadi na wala sifikirii kufanya hivyo na nashukuru Mungu kwa kunijaalia maisha mazuri.Sihitaji kula nondo ya mtu yeyote yule mi Mtanzania banaa!!! Naifahamu vizuri sana nchi yangu. Naona unajibaraguza baraguza tu lakini maswali yangu kuhusu huu utafiti uchwara unayapiga chenga, kama huna majibu ni bora tu useme kwamba sina majibu badala ya kuendelea kuyakwepa.
Mkuu, hata hunijui ushaanza kunibambikia kashfa kibao!!... huo ndio ulimbukeni unaowasumbua.Kuhusu wazo langu, wewe chukulia kama mfano tu, hiyo mihasira ni frustrations zako mwenyewe..... ukiweza ipig ngumi screen!!Unaijua nchi yako vizuri?.... lol what a clown!Wanaowaambia mna gesi kiasi fulani au mna uranium kiasi fulani ni nani?.... usione noma babu, kula nondo hizo uache kupayukapayuka kama mlevi wa mataputapu.Mara picha ya Will Smith mara picha ya ya Michael Jordan, who are you fooling, we know you got some fantasies about something!!! just by the look of things.
Later dude!!!:msela:
 
Kwa maoni yangu, japo yataonekana dhaifu, ni kuwa: Tangu awali miaka ya 1992 wakati wa kuanzishwa kwa vyama vingi wananchi weng walitishwa kuwa kukiwa na vyama vingi kutakuwa na vita!! Hali hii ikapelekea watu kuwa na hofu na kupatikana % chache ya wananch ya kuanzishwa vyama ving. Ikabidi serikal ipitishe matakwa ya UN ya kuitaka TZ iwe na mfumo wa vyama ving. Pia tatizo ni kuwa mananch hasa vijjni hatuna uelewa mkubwa juu ya demokrasia. Tena viongozi wanapotosha mawazo ya vyama vya upinzani kana kwamba ni uongo. Tatizo lingine vyama vya upinzani inaonekana kwa wananch ni njaa tu. Kwani hakuna wanacho kifanya. Mfano Mrema. Alituanzishia upinzani kwa mguu mbovu.
 
Vlevle watz ha2na umoja wadhat. Inatokea pale ambapo mtu m1 anapopata nafasi nzuri serikalin anakuwa kinyume na wenzake. Tunahtaj wasomi wawe wa kwanza kuelmisha umma badala ya kutumia ujinga wao kuneemeka.
 
Unafki we2 Watz kama Zawadi Ngoda ndio kwazo kwa upinzani wa dhat. Ambao tunaona jitihada za upinzani nchin si lolote wala chochote. Badala yake tunajitahidi kuwasafisha mafisadi kama EL, ili 2015 ikiwezekana wawe wakuu tena wa nch yetu. Ni kutafuta kasoro tu kutoka upinzani kila uchwao ili mafisadi watakaswe waendelee kurithishiana urais wao kwa wao. Ndiyo maana mnaandika makala ndefu za kudhoofisha wapinzani wanao onekana kujaribu kutetea umma wa Watz. Acheni hivo kwani hawajapewa nafasi ya kufanya tukaona na wao wanatufisadije. Uozo wa ccm uko wazi lakini je wewe Ngoda unaweza kumweleza kiongozi wako anayekulipa mshahara kwa ujasiri wote? Badala ya kusema ukwel unalemba kwa kueleza kuwa ah! kila mwanadamu anamapungufu yake. Kwa hiyo sisi wananch 2endelee kuvumilia mapungufu yao na kuendelea kuwachagua wao?!! HAKUNA.
 
Sikubali kabisa kuwa 54% ya Watanzania hawakupiga kura 2010. Kilichotokea ni kwamba ili Kikwete kupata ushindi, baada ya kushindwa Arusha, Moshi, Mara, Mwanza, ilibidi NEC wapike kura na kuondoa idadi kubwa ya wapiga kura kuonyesha kwamba Kikwete alipata asilimia 61% wakati ukweli ni kwamba alipata asilimia 27% kwenye kura za urais. Musoma mjini Kikwete alipata kura tatu tu. Lakini ikabidi wageuze na kumpa ushindi. Matokeo yake ndiyo tunayoyaona hivi sasa. Hebu waambie NEC watoe matokeo kamili ya uchaguzi wa 2010 kama watakujibu.

Mh Interesting yawezekana ukawa ni ukweli but mie nimechukua namba ya wapiga kura na waliojiandikisha kupiga kura nikapigwa na butwaa. Zaidi soma hapa chini:-

31 October 2010 Presidential Election
Registered Voters
20,137,303
Total Votes (Voter Turnout)
8,626,283 (42.8%)
Invalid/Blank Votes
227,889
Total Valid Votes
8,398,394

Data ya hizi zinapatikana hapa:-

Elections in Tanzania

Clearly, unaona kuwa 57.2% ya wapiga kura wamekula mbizi hawakupiga kura au kwajina lengine kura za marohani. I think theory yako inawezekana kuwa kweli but basi waibe kura zaidi ya milioni 5? Kura milioni 1 zinawezekana but milioni 5 I sincerely doubt it ila sisemi haliwezekani ila kama wameweza kujaza watu milioni 5 basi na vyama vya upinzani vilikuwa vimelala. Wapiga kura zaidi milioni 5 ni wengi mno.
 
Hapo mwisho kuwa vyama vya upinzani vitakufa,bila kuonyesha namna vitakavyokufa,kweli nimesita kuamini utafiti wako! La zaidi ni pale ulipoponda maandamano ya Arusha, ndiyo kabisaa umenifanya nijute kupoteza muda kusoma huo mchiriku,au hadithi inayoitwa utafiti. Ushauri wa bure: subiri 2015,tafiti hizi zinakuwa dili.
 
:msela:Mkuu, hata hunijui ushaanza kunibambikia kashfa kibao!!... huo ndio ulimbukeni unaowasumbua.Kuhusu wazo langu, wewe chukulia kama mfano tu, hiyo mihasira ni frustrations zako mwenyewe..... ukiweza ipig ngumi screen!!Unaijua nchi yako vizuri?.... lol what a clown!Wanaowaambia mna gesi kiasi fulani au mna uranium kiasi fulani ni nani?.... usione noma babu, kula nondo hizo uache kupayukapayuka kama mlevi wa mataputapu.Mara picha ya Will Smith mara picha ya ya Michael Jordan, who are you fooling, we know you got some fantasies about something!!! just by the look of things.
Later dude!!!:msela:

Hahahahah lol! We unachekesha kweli. Kumbe ukweli unauma eh!? :majani7:Eti sikujui!?:majani7: Kwani nahitaji kukufahamu ili kuona kwamba mawazo yako yamepitwa na wakati au ni yale ambayo yanaonyesha wewe ni fisadi au unaneemeka kupitia migongo ya mafisadi?

Kwako wewe hukubali kama kuna mafisadi nchini. EPA, Meremeta, Kagoda, Uuzwaji wa nyumba za Serikali, Mikataba ya uchimbaji wa madini yetu ambayo haina maslahi ya nchi yetu, Wizi uliofanywa na Mkapa wa Kiwira Coal mining na ardhi ya Wananchi kule Kilombero, ununuzi wa ndege ya rais, Richmond/Dowans n.k.

Kuhusu MJ na Willy Smith zisikupe shida hizo ni avatar tu na wala sina fantasy zozote kama unavyodhani na watu wengi hapa ukumbini wanazitumia na hata wewe unayo hiyo ya Tintin na sidhani ni kwa kuwa na hiyo avatar ya :majani7:Tintin:majani7: kunaonyesha kwamba una fantasies zozote kuhusiana na :majani7:Tintin.:majani7:

Kuhusu mataputapu hahahah lol! Mie siyajui hebu nieleze mwenzangu wapi ulikamata hii kitu:majani7: inaitwa mataputapu na hata kuwa na mwazo ya kusadikika eti Tanzania hakuna mafisadi!!! Naona weye ndiye mlevi wa mataputapu maana hizi habari nchini mwetu za miaka chungu nzima sasa kama vile EPA, Meremeta, Kagoda, Uuzwaji wa nyumba za Serikali, Mikataba ya uchimbaji wa madini yetu ambayo haina maslahi ya nchi yetu, Wizi uliofanywa na Mkapa wa Kiwira Coal mining na ardhi ya Wananchi kule Kilombero, ununuzi wa ndege ya rais, Richmond/Dowans n.k inaonekana kwako wewe ni hadithi kama za Sungura na Fisi. Fungua macho uone yanatokea nchini mwako ili uachane na mawazo finyu inaelekea hata 5% yanayotokea nchini kwako huyajui.

By the way my name on this forum is Bubu and not Babu. Next time make sure you use proper spelling for Bubu.


Have a great weekend


tintin-cp-2632484.jpg
:majani7::majani7::majani7:
 
Mfano wa mambo ya upinzani yanayowakatisha tamaa wananchi hata kwenda ku piga kura: Hivi Maalim Seif Shalif Hamad yupo hapa nchini au anaishi nchi za nje?. Tafakari!
 
Watanzania wana uchu mkubwa wa kuiona CCM inahama IKULU, na kukipisha chama kingine kuingia Ikulu. Haya ni majibu ya utafiti wa kile kikundi chetu binafsi "SONGAMBELE" amabacho kina wanachama na wataalam wake toka vyuo vikuu mbali mbali Tanzania.

Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.

Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."

Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.

Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"

Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."

Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.

​Ulisomea wapi propaganda? Unajaribu lakini bado. Rudi tena darasani ukakomae.
 
Watanzania wana uchu mkubwa wa kuiona CCM inahama IKULU, na kukipisha chama kingine kuingia Ikulu. Haya ni majibu ya utafiti wa kile kikundi chetu binafsi "SONGAMBELE" amabacho kina wanachama na wataalam wake toka vyuo vikuu mbali mbali Tanzania.

Aidha katika taarifa hiyo imeonyesha kuwa 70% kati ya watanzania walioshiriki katika utafiti huo ( 1 milioni) wanahitaji chama kingine zaidi ya CCM Kuingia Ikulu. Lakini walipoulizwa ni chama gani kati ya vyama pinzani walipenda kukiona kinaingia Ikulu, 65% walijibu "hakuna". Hii inaonyesha wazi jinsi vyama vya upinzani vilivyowakatisha tamaa watanzania toka katika ndoto yao ya kukiona chama cha upinzani kuingia ikulu.

Nilipomhoji Prof Safari kuhusu matokeo hayo alisema yafuatayo "Sishangazwi wala kushitushwa na taarifa hiyo, angalia kampeni zao ni za kubabaisha tu, hakuna chama kinachokidhi matakwa ya wananchi. Hakuna chama cha upinzani katika vyama vikuu kilichoweza kuonyesha kuliweka wazi swala la umoja wa kitaifa. Vyama hivi aidha vimelaumiwa kwa kuendekeza ukabila au udini, na wameshindwa kujibu tuhuma hizo kwa kiwango ambacho watanzania watawaelewa. Kuwa na viongozi wa vyama ambao walishiriki au wanashiriki katika nyadhifa za taasisi za kidini ni kosa kubwa kwa kipindi hiki, watanzania hawako tayari kwa hilo japokuwa kisheria inakubalika."

Katika utafiti huo CHADEMA iliongoza kati ya vyama pinzani kuingia IKULU kwa kuwa na 16% ikifuatiwa na CUF 14%. Cha kushangaza hata maeneo yale ambayo huhesabika kama ngome yaCHADEMA, ilifanya vibaya. Kwa mfano Arusha ni 35% na Moshi 40% tu ndio waliohitaji kuiona CHADEMA yaingia IKULU. Kwa Arusha wengi walikatishwa tamaa na viongozi wao hasa kwa tukio la hivi karibuni la kuwapeleka wanachama kuandamana bila mipango maalum.

Mh Slaa nilipompigia simu alikataa kusema lolote na kukata simu. Mh Zitto Kabwe, alicheka na kusema "sina uhakika kama hizo namba zinawakilisha hali halisi. Hata hivyo kuwaeleza watu mpaka wakuelewe inachukua muda, chama hakina haraka. Tunachojua sisi ni kuwa tukilinganisha na tulikotoka tunajivuna kuwa chama kinapiga hatua"

Nilipomhoji Julius Mtatiro alisema yafuatayo: "Watanzania wanapenda propaganda, chama chetu hatukujiandaa kwa hilo na wala hatuamini hilo. Namba si tatizo kwa chama chetu, tutaendelea kuwaambia ukweli watanzania na tuna program nzuri inayokwenda hatua kwa hatua. Tumetatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani, sasa nguvu yote tunaielekeza Tanzania bara. Utajionea mwenyewe matokeo ya uchaguzi ujao."

Hali ya vyama vya upinzani ni mbaya, kwani kama haitasikiliza matakwa ya watanzania kuna hatari kwa vyama hivyo kufa. Wakati ni huu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu.


Nimeshawahi kuandika hiki kitu kijuu juu kuhusu kwa nini CCM na kuboronga kwake bado sioni ikishindwa 2015...upinzani utatoka CCM tu kama slaa alitoka na amepandisha chati CDM basi wengine 10 wakitoka itapandisha zaidi upinzani na kuwapa wapinzani sura ya kitaifa zaidi kuliko sasa itawachukua wapinzani angalau miaka 15 angalau kuitoa CCM na hapa kama wapinzani wakiwa wamoja na CCM ikiendelea na upuuzi wao wa sasa
 
Nimeshawahi kuandika hiki kitu kijuu juu kuhusu kwa nini CCM na kuboronga kwake bado sioni ikishindwa 2015...upinzani utatoka CCM tu kama slaa alitoka na amepandisha chati CDM basi wengine 10 wakitoka itapandisha zaidi upinzani na kuwapa wapinzani sura ya kitaifa zaidi kuliko sasa itawachukua wapinzani angalau miaka 15 angalau kuitoa CCM na hapa kama wapinzani wakiwa wamoja na CCM ikiendelea na upuuzi wao wa sasa


Unamaanisha nini unaposema kama wapinzani wakiwa wa moja?hivi cuf,tlp,udp nao ni wapinzani kweli?nyie endeleeni na tafiti zenu nasijui kama huwa mnahoji watu kweli au kuna dili fulani tu.Basi tunataka utafiti kwanini chadema ilifanya vizuri kiasi cha kuibuka na kura 23000 dhidi ya 26000 za ccm kwakufanya kampeni ndani ya mwezi mmoja na bila kuwa na mtandao wowote jimboni igunga na haikuungana na chama kingine cha upinzani?
 
Back
Top Bottom