Watanzania wamepoteza matumaini na Bunge

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Hili Bunge linaonekana ni kichekesho na lililojaa miujiza na watetezi wa mafisadi. Sioni cha maana chochote kinachoendelea ndani ya Bunge hili zaidi ya utetezi wa mafisadi na viini macho vya hapa na pale lakini yale ambayo Watanzania tunataka kuyasikia Chama Cha Mafisadi kinafanya juu chini ili tusiyasikie. Sasa hivi wapinzani inabidi waandike uozo wote wa EPA, Richmond, Kiwira n.k. na kusambaza kwenye balozi za nje na mashirika ya Kimataifa kama IMF, WB, UN n.k. kuna haja ya nchi wafadhili na mashirika ya kimataifa kuishinikiza serikali ili iwakamate na kuwafungulia mashtaka mafisadi wote vinginevyo ufisadi utaendelea kupamba moto na watalindana kwa kila hali. Hakuna umuhimu wowote wa kuendelea kufuatilia miujiza inayoendelea ndani ya Bunge Uchwara.
 
Ala!
Ndio umefungua macho sasa?
Nilipowaambia haki inapokwa mkabisha hadi muambiwe na nani?
Yani kuna baadhi ya mambo watu flani flani wakisema ndiyo kweli?
Si niliambiwa mimi ni wa facebook?
Mmeona sasa?
Ndoto ya Tina ya raisi LOWASAA NA MAKAMU CHENGE MNAOINA SASA?
Mkadai nataka kumwaga damu?
 
Nchi ilishauzwa!Tuombe Mungu kwani kina CHENNEY WATAUZA SILAHA ZAO HUKU BUSH AKIPORA MADINI NA MAFUTA!
MMEKWISHA!
 
Hili Bunge linaonekana ni kichekesho na lililojaa miujiza na watetezi wa mafisadi. Sioni cha maana chochote kinachoendelea ndani ya Bunge hili zaidi ya utetezi wa mafisadi na viini macho vya hapa na pale lakini yale ambayo Watanzania tunataka kuyasikia Chama Cha Mafisadi kinafanya juu chini ili tusiyasikie. Sasa hivi wapinzani inabidi waandike uozo wote wa EPA, Richmond, Kiwira n.k. na kusambaza kwenye balozi za nje na mashirika ya Kimataifa kama IMF, WB, UN n.k. kuna haja ya nchi wafadhili na mashirika ya kimataifa kuishinikiza serikali ili iwakamate na kuwafungulia mashtaka mafisadi wote vinginevyo ufisadi utaendelea kupamba moto na watalindana kwa kila hali. Hakuna umuhimu wowote wa kuendelea kufuatilia miujiza inayoendelea ndani ya Bunge Uchwara.

Nilikuwa najua mtafunguka macho baada ya 2010. Post basi hiyo habari au unasubiri niiweke? Nimeshaiweka. Ndugu yangu ulinitukana sana siwezi kukusahau ila unanivyunja nguvu sana unapokata tamaa. Nilikuwa najua wananchi wamepata watetezi wapya na wanatakiwa kuunga mkono. Nadhani tuendelee kuwaunga mkono ili wazidi kututetea. Mwanakijiji naona naye kapotea leo mambo sijui vipi.
 
Ala!
Ndio umefungua macho sasa?
Nilipowaambia haki inapokwa mkabisha hadi muambiwe na nani?
Yani kuna baadhi ya mambo watu flani flani wakisema ndiyo kweli?
Si niliambiwa mimi ni wa facebook?
Mmeona sasa?
Ndoto ya Tina ya raisi LOWASAA NA MAKAMU CHENGE MNAOINA SASA?
Mkadai nataka kumwaga damu?

Ukifuatilia post zangu zote hapa sijawahi kufumba macho hata kidogo, nilisema Kilango apewe muda lakini jambo lilitokea jana la kuzuia hotuba ya Dk Slaa kuonyeshwa LIVE limenifanya nione kwamba hakuna jipya huko bungeni, na mimi siyo mtabiri kwamba ningelijua hili kabla halijatokea. Chama cha mafisadi wanadai kukitetea chama cha MDC dhidi ya manyanyaso, vipigo na mauaji wanayofanyiwa na ZANU PPF wakati wao CCM wanayafanya hayo hayo!!! Kumsemea hovyo Mugabe ni kutaka kujionyesha mbele ya jumuiya ya kimataifa kwamba wao ni tofauti na ZANU PF, kumbe hakuna tofauti yoyote kati ya Chama Cha Mafisadi na ZANU PF.
 
Ukifuatilia post zangu zote hapa sijawahi kufumba macho hata kidogo, nilisema Kilango apewe muda lakini jambo lilitokea jana la kuzuia hotuba ya Dk Slaa kuonyeshwa LIVE limenifanya nione kwamba hakuna jipya huko bungeni, na mimi siyo mtabiri kwamba ningelijua hili kabla halijatokea. Chama cha mafisadi wanadai kukitetea chama cha MDC dhidi ya manyanyaso, vipigo na mauaji wanayofanyiwa na ZANU PPF wakati wao CCM wanayafanya hayo hayo!!! Kumsemea hovyo Mugabe ni kutaka kujionyesha mbele ya jumuiya ya kimataifa kwamba wao ni tofauti na ZANU PF, kumbe hakuna tofauti yoyote kati ya Chama Cha Mafisadi na ZANU PF.
Haijapita hata wiki huo muda uliokuwa unasema ni masaa mangapi? Mnakuwa mnatuchanganya sasa mara tumpe muda mara mnakata tamaa sasa mpaka hatuwaelewi. Mimi nadhani tumpe muda zaidi.
 
Haijapita hata wiki huo muda uliokuwa unasema ni masaa mangapi? Mnakuwa mnatuchanganya sasa mara tumpe muda mara mnakata tamaa sasa mpaka hatuwaelewi. Mimi nadhani tumpe muda zaidi.

Haya mambo huwezi kuyafanya kama Macpolitics, vyakula vya macdonalds unaingia dakika tatu umeshapata fries zako na burger na soda umekula msosi ambao si msosi si chochote ni uchafu tu. Nasema hivyo kwa sababu kunapokuwa na mmoja ndani ya kundi anaongea lugha tofauti na ile wanayoongea wenzake katika kundi hilo na wenzake hawataki kusikia lugha anayoongea (utakumbuka jinsi Mama Anna Abdallah Kawawa Msekwa Mhaville alivyomshambulia Kilango) basi inabidi tumpe muda, lakini haikuhitaji hata wiki kukatika huyo mama kajikanyaga kanyaga mwenyewe sijui kama amefanya hivyo baada ya vitisho alivyopewa toka kwa mafisadi ndani ya chama au alikuwa anatupaka mafuta ya mgongo tu.

Niliandika hapa ukumbini kwamba katika bunge hili la Bajeti lililoanza June 10 tulipe siku 10 tutajua kama kuna mabadiliko ndani ya bunge au ni mambo yale yale ya kutetea maslahi ya chama cha mafisadi na mafisadi wenyewe. Siku hizo 10 zimeshakatika na mimi nimeshahitimisha Bunge hili kama miaka ya nyuma litaendelea kuwakatisha tamaa Watanzania maana liko pale siyo kwa maslahi ya Watanzania bali kwa maslahi ya mafisadi wachache.
 
Haya mambo huwezi kuyafanya kama Macpolitics, vyakula vya macdonalds unaingia dakika tatu umeshapata fries zako na burger na soda umekula msosi ambao si msosi si chochote ni uchafu tu. Nasema hivyo kwa sababu kunapokuwa na mmoja ndani ya kundi anaongea lugha tofauti na ile wanayoongea wenzake katika kundi hilo na wenzake hawataki kusikia lugha anayoongea (utakumbuka jinsi Mama Anna Abdallah Kawawa Msekwa Mhaville alivyomshambulia Kilango) basi inabidi tumpe muda, lakini haikuhitaji hata wiki kukatika huyo mama kajikanyaga kanyaga mwenyewe sijui kama amefanya hivyo baada ya vitisho alivyopewa toka kwa mafisadi ndani ya chama au alikuwa anatupaka mafuta ya mgongo tu.

Niliandika hapa ukumbini kwamba katika bunge hili la Bajeti lililoanza June 10 tulipe siku 10 tutajua kama kuna mabadiliko ndani ya bunge au ni mambo yale yale ya kutetea maslahi ya chama cha mafisadi na mafisadi wenyewe. Siku hizo 10 zimeshakatika na mimi nimeshahitimisha Bunge hili kama miaka ya nyuma litaendelea kuwakatisha tamaa Watanzania maana liko pale siyo kwa maslahi ya Watanzania bali kwa maslahi ya mafisadi wachache.
Bubu usimwandame sam...Kubali uliteleza!
Mbona wengi tu wamekubali?
 
Watu kama mlifanya mistake kubalini tu!
Maana wengine humu ndani si wafuasi wa hoja bali watu!
UNABISHA?
 
Watu kama mlifanya mistake kubalini tu!
Maana wengine humu ndani si wafuasi wa hoja bali watu!
UNABISHA?

Nikiteleza huwa nasema na nimeshafanya hivyo mara nyingi hapa, lakini hapa sikuteleza. Huyu mama ni msanii ama vitisho alivyopewa vimemtikisa maana haiwezekani kabisa in less than a week ukatoa kauli mbili tofauti zinazopingana!! Moja kuna wabunge wa CCM hawasemi chochote ndani ya bunge na hilo ni kweli kabisa, halafu kauli nyingine wabunge wa CCM tuko imara kupambana na ufisadi!!! hili si la kweli hata kidogo na Watanzania tulio wengi tunaujua ukweli halisi.
 
Nikiteleza huwa nasema na nimeshafanya hivyo mara nyingi hapa, lakini hapa sikuteleza. Huyu mama ni msanii ama vitisho alivyopewa vimemtikisa maana haiwezekani kabisa in less than a week ukatoa kauli mbili tofauti zinazopingana!! Moja kuna wabunge wa CCM hawasemi chochote ndani ya bunge na hilo ni kweli kabisa, halafu kauli nyingine wabunge wa CCM tuko imara kupambana na ufisadi!!! hili si la kweli hata kidogo na Watanzania tulio wengi tunaujua ukweli halisi.

Na ukweli huo ukuweke huru moja kwa moja kabla hujasapoti watu kumwaga damu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom