Watanzania wamepoteza imani na serikali yao

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Watanzania wamepoteza kabisa imani na serikali iliyo madarakani kufuatia kashfa nyingi zinazowakabili watendaji wakuu wa awamu ya tatu na ya nne. Kashfa hizi zinahusiana na kusaini mikataba feki ya uchimbaji wa madini isiyo na maslahi kwa Tanzania, ufisadi wa mabilioni ya shilingi uliofanywa na viongozi mbali mbali, kujipatia kampuni na migodi ya madini yaliyo chini ya serikali (KCM) kwa njia za haramu, kuzembea na hatimaye kutoroka kwa mhusika mkuu wa kashfa ya Rada.

Kinachotushangaza Watanzania pamoja na kashfa zote hizi hakuna aliyepoteza ajira yake(Ballali alijiuzulu kabla ya kutenguliwa kwa uteuzi wake) hakuna aliyetiwa ndani ili kuvisaidia vyombo vya dola katika uchunguzi, hakuna ambaye mali zake zimeshikiliwa na serikali ili kujua kama zimepatikana kihalali.

Kwa mantiki hiyo basi tuna wasi wasi mkubwa kwamba serikali iliyo madarakani haina uwezo wa kupambana na kashfa nzito zilizowashtua Watanzania labda kwa kuwaogopa wahusika au kwa watendaji waliomo serikalini kuhusika kwa namna moja au nyingine na kashfa hizo.

Hivyo tunaomba serikali ijiuzulu ili kutoa nafasi ya uchaguzi mpya utakaoinusuru nchi yetu kwa janga kubwa linaloinyemelea Tanzania.
 
Mkuu Bubu nakusoma vizuri. Lakini naweza kukusahihisha kidogo kuwa jamaa aliyehusika na Radar hakupotea, zilikuwa ni deliberate efforts za watu, walijua wanafanya nini.
Hakuna atakayefukuzwa kazi na wala hakuna atakaye adhibiwa kwa hii issue. Hiyo miezi sita aliyotoa JK ni kuwapa jamaa six months head start.
Wanaoadhibiwa ni kama kina kubenea, Tega na wengine wadgowadogo watakaofuata, the real ones will not be touched.
My worry ni kuwa hata hiyo 2010 sidhani kama kuna lolote kubwa litafanyika, mimi ninachoana 2010 itakuwa ndio real test ya kama watanzania tuna akili au hatuna akili. Sasa hivi mambo mengi yako wazi, kwa mtu mwenye akili timamu withall what happened in, 2010 sio ya CCM kushinda. Nina wasiwasi we will prove Mkapa right, kuwa sisi ni wavivu wa kufikiri!
 
Sio kweli Watanzania wamepoteza imani.
Watanzania wamepoteza serikali yao.
Ni imani kuwa Serikali imewapoteza Watanzania , kwa Imani zao?
 
Sio kweli Watanzania wamepoteza imani.
Watanzania wamepoteza serikali yao.
Ni imani kuwa Serikali imewapoteza Watanzania , kwa Imani zao?

BUBU Je Imani yako imerudi baada ya lolongo ndefu?
'Baraza jipya la Mwaziri', Je hili imerudisha Watanzania kwa Serikali yao?

Asante
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom