Watanzania Wakati wa Maamuzi Magumu Umefika ama la Kuvua Gamba Kabisa

GHOST RYDER

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
1,025
475

Tumekuwa wepesi sana kuhadaika na wepesi sana kushangilia mambo yasiyokuwa na msingi huku Nchi inatafunwa na ukali wa masiha sasa hausemekani. Awali nilidhani labda ni kwa sababu ya Mfungo wa Ramadhani.

Hivi tunasemaje juu ya Mfumko wa Bei:

  • Ubadhilifu uluiokithiri serikalini
  • Uozo kila Bajeti ya Wizara inayotia Timu Bungeni
  • Giza la Ajabu Nchi Nzima
  • Uhaba wa Maji unaoendana na kukosekana kwa umeme
  • Bei ya Mafuta isiyoeleweka
  • Ubinafsi na Bifu za Viongozi kwa masilahi ya familia zao na mengine mengi name them, hata nacheleea kuandika data maana yamezungumzwa hapa JF mpaka yamechosha
Kama haitoshi watetezi wa mlalahoi wanaitwa Maadui na bado tunashabikia. Hapa ilipofika sasa baasi kama hatuwezi kufanya maamuzi magumu basi tuvue Gamba wenyewe. Nashawishika kuamini kuwa tumejigubika gamba la uzezeta uliopitiliza

My Take:

Honey moon ya Serikali imekwisha

ADIOS
 
Nakumbushwa na Mdau kupitia INBOX ati madini ya Uarani...Mhhhh IMETOSHA
 
Mkuu ukiongelea hayo na nikiangalia life lilivyopanda na mfumuko wa bei ndio usiseme na hakuna kiongozi anayeongea lolote napata kichaa
 
Sijui ni uoga sijui ni ujinga yaani sielewielewi inakuaje tunapigwa dana dana kama kitenesi,wanapasiana tu mara huyu mara yule ili mradi kutuzungusha vichwa tu,JAMANI EEH TUCHUKUE HATUA.
 
"huu ni uchochezi na kukiuka misingi ya amani na utulivu iliyojengwa na waasisi wa nchi hii, na hatutawavumilia kabisa muwahamasishe wananchi kuichukia serikali yao waliyoiweka wenyewe madarakani"

Haya ndio majibu ya viongozi serikalini pamoja na wabunge wa magamba (pamoja na mrema) watakayowajibu wanaotoa hoja hiyo.

Unadhani mabadiliko tutayapata kwa upotoshwaji huu wa hali halisi?
 
Sisi ni wataalamu wa kulalamika kwenye keyboard na keypad tu, hutaiona sura ya mlalamishi huyu barabarani au kwenye geti pale magogoni akishinikiza haki yake.
Ulalamishi huu hausaidii lolote na sanasana tunaonekana tuna gubu tu,
Waislamu tunafundishwa kuliondoa ovu kwa vitendo ambako hapa haonekani mtu,
Ikishindikana option hii basi mtu akemee kwa mdomo ambapo hapa tumejaa wengi sana,
Na kama nayo ni ngumu basi chukia tu moyoni ambapo ni udhaifu wa imani.
Sisi tumegeuza hizi option kwa kuipa kipaumbele option ya kusema sema na kulalamika sana,
Moto unatuhusu tu siku ya kiama!!
 
tatizo la watanzania ni waoga katika kudai haki zetu, inatubidi tuache woga na kudai kile tunachostahili kupewa. haiwezekan mafuta eti yashuke bei siku nne then baada ya kupitishwa bajet ya nishati na madini yanapanda tena, tusifanyane watoto kias hiki. hii nchi inaongozwa kwa maslahi ya wachache tu. Watanzania tuamke jamani
 
Every humanbeing has his breaking point ... and

Every society has the maxmam limt in which you can indulge... !!

Ukiona bado watu wamenyamaza jua kuwa vipimo na mizani haijafikia mahali pake!!
 
Sisi 'watanzagiza' ni watu wa ajabu sana,nahisi Muumba wetu anatushangaa kwa upumbavu wetu!Kila kukicha tumekalia kulalama huku tukijisemea na kuandika 'eti nguvu ya umma'...nguvu gani isiyoweza kusukuma hata kipande cha ukucha wa mtoto mchanga?Ama tuseme kuwa haya machungu na maumivu tunayoyapata yamegeuka kuwa bongo fleva hata kila uchao tuibuke na 'mistari' mipya ya malalamiko?Kwa hakika tunapaswa kujivua gamba la Uzezeta ili tupiganie haki yetu ya maisha bora na usalama wa nchi na rasilimali zetu!
 
Sisi 'watanzagiza' ni watu wa ajabu sana,nahisi Muumba wetu anatushangaa kwa upumbavu wetu!Kila kukicha tumekalia kulalama huku tukijisemea na kuandika 'eti nguvu ya umma'...nguvu gani isiyoweza kusukuma hata kipande cha ukucha wa mtoto mchanga?Ama tuseme kuwa haya machungu na maumivu tunayoyapata yamegeuka kuwa bongo fleva hata kila uchao tuibuke na 'mistari' mipya ya malalamiko?Kwa hakika tunapaswa kujivua gamba la Uzezeta ili tupiganie haki yetu ya maisha bora na usalama wa nchi na rasilimali zetu!
<br /> <br /KWA HALI ILIVYO TZ SASA NA HATUJACHUKUA MAAMUZI YOYOTE HADI SS TUNAISHIA KULALAMIKA MTAANI NA JF NAHISI TUTALALAMIKA HADI YESU ARUDI
 
Mnaosema tumelala si kweli kwani wengi wetu tunasubiri moshi tuwashe moto sio hiyo ni kabla siku ya uhuru 50 tujipange kamavip tutakupa jez barabarani sio wakuu
 
Mnaosema tumelala si kweli kwani wengi wetu tunasubiri moshi tuwashe moto sio hiyo ni kabla siku ya uhuru 50 tujipange kamavip tutakupa jez barabarani sio wakuu
<br />
<br />
Hii haijakaa njema mkuu...yaani tuendelee kusurubika kwa kusubiria 'moshi'?No please...moshi hauwezi kuwepo bila moto,tayari moto upo kinachotushinda ni kuukoleza uwe mkubwa ili uweze kuchoma/kuunguza kila kilicho kichafu!
 
&lt;br /&gt; &lt;br /KWA HALI ILIVYO TZ SASA NA HATUJACHUKUA MAAMUZI YOYOTE HADI SS TUNAISHIA KULALAMIKA MTAANI NA JF NAHISI TUTALALAMIKA HADI YESU ARUDI
<br />
<br />
Duh!mpaka Yesu arudi mbona kimbembe...Tangu arudi kwa baba yake hata wiki hajamaliza!
 

Tumekuwa wepesi sana kuhadaika na wepesi sana kushangilia mambo yasiyokuwa na msingi huku Nchi inatafunwa na ukali wa masiha sasa hausemekani. Awali nilidhani labda ni kwa sababu ya Mfungo wa Ramadhani.

Hivi tunasemaje juu ya Mfumko wa Bei:

  • Ubadhilifu uluiokithiri serikalini
  • Uozo kila Bajeti ya Wizara inayotia Timu Bungeni
  • Giza la Ajabu Nchi Nzima
  • Uhaba wa Maji unaoendana na kukosekana kwa umeme
  • Bei ya Mafuta isiyoeleweka
  • Ubinafsi na Bifu za Viongozi kwa masilahi ya familia zao na mengine mengi name them, hata nacheleea kuandika data maana yamezungumzwa hapa JF mpaka yamechosha
Kama haitoshi watetezi wa mlalahoi wanaitwa Maadui na bado tunashabikia. Hapa ilipofika sasa baasi kama hatuwezi kufanya maamuzi magumu basi tuvue Gamba wenyewe. Nashawishika kuamini kuwa tumejigubika gamba la uzezeta uliopitiliza

My Take:

Honey moon ya Serikali imekwisha

ADIOS
Hapo penkundu: so what next?
 
Hivi kuna any movement ambayo jf ilishawahi kufanya?? I mean any movement ambayo mwananchi wa kawaida hususani mwanakijiji akjua kwamba kuna great thinkers wa kuwatetea. If the answer is NO, then u need new definition of jf
 
Back
Top Bottom