Watanzania waisubiria kwa hamu kauli ya Dr Slaa au JK juu ya mchakato wa katiba mpya

JIULIZE KWANZA

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
2,569
499
Ndugu wana jamvi nimekuwa katika pita pita zangu nyingi na kushuhudia watu wengi wakilalama kuwa wanataka kauli dhabiti kutoka kwa JK kuhusu mchakato wa katiba mpya na msimamo wake yeye baada ya kushuhudia msimamo wa wabunge wa ccm, Lakini sakata hili haliishii hapo kwani aslimia 80% wanaamani JK atakuwa kimya bila kuongelea chochote na hata akilazimishwa kujibu atasema ameachia muhimili wa bunge ndio uamue hivyo basi wananchii hapo ilipofikia na sio vinginevo. Hapo apo na katika hao hao wanaosubiria kauli ya JK wanatamani mtu kama Dr slaa atangaze rasmi msimamo wa chama na hatua za kuchukua ikiwa ni pamoja na kupinga mchato uliopitishwa na bunge la ccm awape moyo muda dakika na mahali pa kuanzia, nililazimika kujua itikadi zao za ki vyama niligundua kuwa watanzania kwenye swala la katiba mpya hawana chama hali ni mbaya kwenye ma bar, vyombo vya usafiri makanisani, misikitini kwenye viwanja vya michezo na hata mikusanyiko mingine hadithi ni katiba mpya na kila niliyemsikia walikuwa wakilalamikia wabunge wa ccm kutumia ubabe ilihali wanajua hawaja usoma na kuuelewa muswada vizuri mbali na kungolewa meno kichama pia wabunge wengi hawajausoma muswada na kuuelewa ndio maana walienda njee ya hoja nakujikuta wakiongelea majungu na ubabe...amini usiamini wako watu bado wanaipenda sana ccm ila wanakerwa sana na uongozi ukichukulia tena hili la katiba ndio wengi wao wameamua kuacha siasa na kuangalia maslahi ya bibilia mpya ya Tanganyika.

Nawakilisha.

Mmoja wa mdau wa ccm nae hayuko nyuma kwenye social media mcheki facebook.

Shy-Rose Bhanji-Mwanaharakati

My love for my party CCM remains intact on condition that the party remains
true to its manifesto. Unfotunately there are clear symptoms of abundaning
the manifesto and embracing the socio-political misfortunes at the behest of
the corrupt clique (kikundi). As such i have no reason to be loyal to CCM because
i am in dilemma...As of now ahadi nyingi kwenye ilani hazijatekelezwa, ajira kwa vijana, uwezeshaji wa kinamama, kushuka kwa thamani ya shillingi, kupanda
kwa gharama za maisha....
TUNAKWENDA WAPI? WHERE ARE WE GOING? JE TUTAFIKA?!
 
Back
Top Bottom