Watanzania waishio nje ya nchi (Tanzania Diaspora) waanza kuandamana

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
1604247251018.png


Watanzania tuishio nje ya nchi (TANZANIA DIASPORA) tumeanza kuandamana kupinga UCHAFUZI uliofanyika juzi hapo nyumbani Tanzania!

Hawa ni ndugu zetu kutoka Ulaya ya Kaskazini (Sweden 🇸🇪, Norway 🇳🇴 na Denmark 🇩🇰) ambao tayari wameanza maandamano yao nje ya Ubalozi wetu uliopo Stockholm, Sweden.

Watanzania tuishio nchini hapa Ufaransa 🇫🇷 tunaandaa maandamano hayo kesho Jumatatu, November 2, 2020 nje ya Ubalozi wa Tanzania 🇹🇿 nchini Ufaransa 🇫🇷.

Maandamano yataanza saa 2 asubuhi na kumalizika saa 6 mchana!

Baada ya maandamano, WAZANZIBARI tuishio nchini hapa, kwa kuongozwa na Balozi wetu (BABU MZANZIBARI), tutazindua Ubalozi wetu (Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar nchini Ufaransa) Ofisi za Ubalozi wetu zipo mitaa ya TROCADÉRO, karibu sana na mnara wa EIFFEL, jijini hapa PARIS.

Kwa niaba ya Wazanzibari wote waishio nchini hapa Ufaransa, mimi, BABU MZANZIBARI, Balozi wa Zanzibar nchini Ufaransa, natumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zetu Watanzania waishio nchini hapa, katika uzinduzi wa Ubalozi wetu!

Usafiri, kula, kunywa ni kwa gharama yangu mwenyewe!

Kwa kauli moja, tumekubaliana kuwa hatuitambui serikali haramu ya John Pombe Joseph Magufuli! Hatuitambui serikali haramu ya Hussein Ali Hassan Mwinyi!

Rais wa Zanzibar tunayemtambua ni Maalim Seif Sharif Hamad aliyechaguliwa na wananchi wa Zanzibar!... Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunayemtambua ni Tundu Antipas Lissu, aliyechaguliwa na Watanzania!

Mungu ibariki Zanzibar yenye mamlaka kamili, Mungu ibariki Tanzania! 🙏🏾
 
Teh teh teh teh, wasitukoromee, Kama wanna ubavu waje waandamane Huku. Kwanza watu wenyewe kura hawakupiga kihere here sijui Cha nini.Sisi tuliopiga kura ndiyo tunajua tulimpigia Nani kura. Waache kimbele mbele. Halafu hao sio Watanzania. Waende wakaandamane kwao Oman huko!
 
Nimehesabu hapo mpo moja mbili tatu nne tano sita saba nane tisa kumi kumi na moja na mshika camera kumi na tatu. MWISHO.

Kweli mmeamua madiaspora msicheke cheke sasa onyesheni sura za maandamano,au mnaandamana mnataka nini maana meno nnje.
 
Back
Top Bottom