Watanzania waishio nchi za Shirikisho la Urusi kuzindua jumuiya (TANCORU)

Tanzania Russia

New Member
Nov 27, 2011
4
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wajumbe wa kamati maalumu ya watanzania waishio Urusi, Jumamosi ya Novemba 26, 2011, walikutana ,ikiwa ni mfululizo wa vikao vya kujadili azma na mchakato wa Uzinduzi rasmi wa Jumuiya ya Watanzania Urusi .The Tanzanian community in Russia(TANCORU).

Katika kikao hicho kilichofanyika Jijini Moscow,na kuhudhuriwa na wawakilishi toka miji mingine ,ambapo pamoja na mambo mengine , wajumbe walipata nafasi ya kujadili kifungu kwa kifungu Mapendekezo na Muundo wa Uongozi na Rasimu ya Uanzilishi wa Jumuiya ya TANCORU.

Katika kuweka kumbukumbu sahihi,JUMUIYA YA WATANZANIA URUSI, (TANCORU) ni jumuiya inayowaunganisha Watanzania wote waishio na kufanya kazi katika nchi zote za lililokuwa Shirikisho la Urusi .

Ni jumuiya ISIYO ya Kisiasa, kidini, Kikabila au Kijinsia ambayo inaheshimu mawazo mbalimbali ya wanajumuiya wake yanayolenga kujenga na kuimarisha umoja wa Jumuiya nzima.

Ni jumuiya itakayowaunganisha watanzania waishio Urusi na asasi za Serikali na taasisi Binafsi nchini Tanzania na Afrika kwa Ujumla.
Lengo na madhumuni ya TANCORU pamoja na mambo mengine ni Kuyapa kipaumbele mambo muhimu yanayohusu maendeleo ya nchi yetu katika nyanja mbalimbali kama vile Elimu, Afya,Uwekezaji,Utalii,na Ustawi wa jamii ya watanzania .

Katika majadiliano hayo, wajumbe wa kamati hiyo, wamekubaliana kuipitisha rasimu ya awali ya Uanzilishi wa Jumuiya na Muundo wa Uongozi wake.
Wajumbe wameafikiana uwepo wa mawasiliano na watanzania wote kupitia mtandao wa jamii wa facebook na email ili kuendelea kukusanya maoni ya wadau katika kuboresha Rasimu ya Uanzilishi wa Jumuiya ya TANCORU.

Mwisho kamati maalumu ya Uanzilishi inatarajia kufanya Mazungumzo na Mheshimiwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Urusi Kapten Mstaafu JAKA MWAMBI mapema juma lijalo kwa lengo la utambulisho wa Jumuiya ya TANCORU ,na majadiliano ya mchakato wa Uzinduzi unaokusudiwa kufanyika katika kilele cha miaka ya 50 ya uhuru wa Tanzania bara.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano,
TANCORU. 144 leninskii Praspect . Email: tancoru@yahoo.com. MOSCOW–RUSSIA.
27 Novemba, 2011.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wajumbe wa kamati maalumu ya watanzania waishio Urusi, Jumamosi ya Novemba 26, 2011, walikutana ,ikiwa ni mfululizo wa vikao vya kujadili azma na mchakato wa Uzinduzi rasmi wa Jumuiya ya Watanzania Urusi .The Tanzanian community in Russia(TANCORU).

Katika kikao hicho kilichofanyika Jijini Moscow,na kuhudhuriwa na wawakilishi toka miji mingine ,ambapo pamoja na mambo mengine , wajumbe walipata nafasi ya kujadili kifungu kwa kifungu Mapendekezo na Muundo wa Uongozi na Rasimu ya Uanzilishi wa Jumuiya ya TANCORU.

Katika kuweka kumbukumbu sahihi,JUMUIYA YA WATANZANIA URUSI, (TANCORU) ni jumuiya inayowaunganisha Watanzania wote waishio na kufanya kazi katika nchi zote za lililokuwa Shirikisho la Urusi .

Ni jumuiya ISIYO ya Kisiasa, kidini, Kikabila au Kijinsia ambayo inaheshimu mawazo mbalimbali ya wanajumuiya wake yanayolenga kujenga na kuimarisha umoja wa Jumuiya nzima.

Ni jumuiya itakayowaunganisha watanzania waishio Urusi na asasi za Serikali na taasisi Binafsi nchini Tanzania na Afrika kwa Ujumla.
Lengo na madhumuni ya TANCORU pamoja na mambo mengine ni Kuyapa kipaumbele mambo muhimu yanayohusu maendeleo ya nchi yetu katika nyanja mbalimbali kama vile Elimu, Afya,Uwekezaji,Utalii,na Ustawi wa jamii ya watanzania .

Katika majadiliano hayo, wajumbe wa kamati hiyo, wamekubaliana kuipitisha rasimu ya awali ya Uanzilishi wa Jumuiya na Muundo wa Uongozi wake.
Wajumbe wameafikiana uwepo wa mawasiliano na watanzania wote kupitia mtandao wa jamii wa facebook na email ili kuendelea kukusanya maoni ya wadau katika kuboresha Rasimu ya Uanzilishi wa Jumuiya ya TANCORU.

Mwisho kamati maalumu ya Uanzilishi inatarajia kufanya Mazungumzo na Mheshimiwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Urusi Kapten Mstaafu JAKA MWAMBI mapema juma lijalo kwa lengo la utambulisho wa Jumuiya ya TANCORU ,na majadiliano ya mchakato wa Uzinduzi unaokusudiwa kufanyika katika kilele cha miaka ya 50 ya uhuru wa Tanzania bara.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano,
TANCORU. 144 leninskii Praspect . Email: tancoru@yahoo.com. MOSCOW–RUSSIA.
27 Novemba, 2011.

Doh! Sielewi mliwasiliana vp na watz nje ya moscow. Si tunasoma ryazan, mwendo wa 2hrs kwa gari toka moscow lkn hatukupata hii news.
 
Pamoja sana, Harashoo. Sasa ni kwenda kujichana Vodka na Kalubasa kwa saaana tu mara baada ya kufungua. Na zdrove, SPASIBA :)
 
Back
Top Bottom