Watanzania wahimizwa kujitokeza Uwanja wa Uhuru kumuaga Rais Mstaafu Mkapa leo kutokana na ugumu wa ratiba ya kesho

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Hassan Abbas amehimiza Watanzania kujitokeza kwa wingi kuaga mwili wa Rais mstaafu, Benjamini Mkapa leo.

Aliwataka mawaziri na manaibu wao, wakuu wa mikoa na watumishi wote wa umma, sekta binafsi na wananchi wengine waende kumuaga Mkapa leo kwa kuwa kesho muda hautatosha.

Akizungumza na vyombo vya habari kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, Dk Abbas alisema ni vema wananchi wakajitokeza leo kwa kuwa ratiba ya kesho Jumanne itakuwa ngumu kwao kupata nafasi kutokana na muda.

Hii inatokana na ratiba inayoonesha kwamba Rais John Magufuli ataongoza waombolezaji wa kitaifa na kimataifa kuaga mwili wa mzee Mkapa na baadaye mwili utasafirishwa mchana kupelekwa kijijini Lupaso, Mtwara kwa ajili ya maziko.

Dk Abbasi alisema serikali inaendelea kupokea salamu za rambirambi na pole na kwamba viongozi wa kimataifa wamethibitisha kuja kuaga na hivyo kutokana na ratiba hiyo inawezekana muda usiwe rafiki kwa viongozi na wananchi wote kupata nafasi siku hiyo.

“Nirudie tena kusema bado tunaendelea kupokea salamu za pole kutoka ndani na nje ya nchi, tunategemea kupata wawakilishi na viongozi wa kimataifa watakaoshiriki kuaga hiyo kesho, sasa muda hautakuwa rafiki kwa sababu baadaye siku hiyo, mwili wa mzee wetu utasafirishwa kwenda Lupaso kwa mazishi,” alisema Dk Abbasi.

Chanzo: Habari Leo
 
Wasiyempenda kaja!

Tupo Buguruni hapa tunamalizia supu murua kabisa, tunasubiri mkombozi atue tukampokee, tukishampokea mkombozi tutaangalia kama muda unaruhusu tuje hapo uhuru
 
Serikali haipendwi mpaka inahimiza watu waende?

It means wanatumia coercive force of some sort?

Tushafika sehem mbaya sana...

Mambele watu wanaalikwa kwa kadi kabisa.

I remember mazishi ya serikali za nyuma wananchi wanaambiwa wapungue wasiende kwa wingi maana walikua wanapenda sana hizo serikali.

That can not be said to this one...what a shame!
 
Kizalendo kabisa na kitaifa ilipaswa apelekwe Dodoma kuagwa, kama sio kuzungushwa mikoa kadhaa.
 
Tukija mipolisi na migambo yenu itatupiga mikwara.... Nipo zangu manzese napiga supu ya mbuzi na chapati sita. Nina mgeni toka mkoani kagera nahitaji kumshughulikia kwanza.
 
Serikali haipendwi mpaka inahimiza watu waende?

I remember mazishi ya serikali za nyuma wananchi wanaambiwa wapungue wasiende kwa wingi maana walikua wanapenda sana hizo serikali..

That can not be said to this one...what a shame!

Kabisa mlamu!
 
Nakumbuka neyerere alipo kufa, serikali ilipata kazi sana kuhakilisha watu wanazuiliwa kufurika barabarani kwa ajili ya kiona mwili wa Baba wa taifa.

Hakuna mtu ambaye alihimizwa kwenda kuona mwili, ila wananachi waliacha makazi yao na kwenda kujazana barabarani hadi polisi kuwazuia baadhi ya wananchi.


Sasa huu utaratibu wa sasa nadhani serikali iuangalie maana baadae tutalazikishwa kwa fimbo kwenda kuwaona viongozi.

Pia ji wakati wa kutafakari viongozi wawapo madarakani kuhakikisha wananchi wote wanawatendea sawa..

Mfumo wa vyama vingi unaotumika kutugawa wananchi ndio unao zuia umoja katika matukio kama haya.

Viongozi lazima waheshimu wananchi kama watakavyo hitaji kuheshimiwa.


Nyerere na Mkapa walikua viongozi wa Watanzania wote na hawakubagua mtu, lakini tunako kwenda kuna viongozi tutapata kazi sana kuwaaga kwa sababu ya matendo yao ya kibaguzi.

RIP jembe letu Mkapa.. kamwe kazi zako na upendo wako havita sahaulika.

20200725_231327.jpeg
 
Nakumbuka neyerere alipo kufa, serikali ilipata kazi sana kuhakilisha watu wanazuiliwa kufurika barabarani kwa ajili ya kiona mwili wa Baba wa taifa.

Hakuna mtu ambaye alihimizwa kwenda kuona mwili, ila wananachi waliacha makazi yao na kwenda kujazana barabarani hadi polisi kuwazuia baadhi ya wananchi.
Mkuu umeuliza swali halafu ukajijibu mwenyewe. Kuna WAPENDWA na wapendwa.
 
Back
Top Bottom